Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 239
Pale ninapowaona kwenye kupitia luninga wakiilalamikia serikali kero mbali mbali wakati wakitafuta elimu kero kama huduma duni vyuoni/mashuleni, ukosefu wa chakula cha kutosha, ukosefu wa walimu, vifaa vya kujisomea kama vile maabara na vitabu na kero zao nyingi nyingine. Na hasa pale tunaona wanasiasa na viongozi wa serikali hii ya CCM wakifuja pesa, wakiiba na kujitajirisha, wakipokea milungula na kuweka mabilioni huko Uswisi na kwingineko kutokana na mikataba mibovu nay a siri isiyokuwa na masilahi kwa taifa. Halafu hapo hapo wanajaribu kutafuta visababu vya kushindwa kuboresha elimu na mazingira yake. Ndiyo, huwa nabubujika machozi na kuilaani sana serikali ya CCM.