Huduma ya usafiri - unyanyasaji wa abiria

Huduma ya usafiri - unyanyasaji wa abiria

HAKUNA

Senior Member
Joined
Mar 12, 2012
Posts
133
Reaction score
66
YAH: UNYANYASAJI WA ABIRIA

Nimekuwa nikisafiri na mabasi yaendao mikoani na mara kwa mara nimekuwa nikishuhudia unyanyasaji wa abiria kwa namna moja au nyingine kutoka kwa wahudumu wa mabasi hayo, pamoja na lugha chafu; kwa sasa kumekuwa na tabia kwamba makondakta ndiyo wenye mamlaka juu ya basi husika kuliko dereva ambaye kwa mtazamo wangu naona kama ndio ana dhamana kubwa juu ya abiria.


Tarehe 06/08/2013, Mimi na mke wangu na mtoto wetu wa umri wa miaka mitatu (3) tulikuwa tunasafiri kutoka Dodoma kuelekea Mbeya Mjini kwa basi la Hood, ambapo tulipofika eneo la mbuyuni basi liliingia na kusimama katika mgahawa ujulikanao kwa jina la al-jazera na mhudumu wa basi alitaarifu abiria wote kwamba tuna muda wa dakika kumi (10) kwa ajili ya kupata chakula.


Abiria wengine walianza kushuka, nami pamoja na mtoto wangu tulivhukua uamuzi wa kushuka vile vile; lakini eneo la kupita abiria lilikuwa limejaa mizigo (vifurushi) hivyo kufanya zoezi la kushuka kwenye basi kuchukua muda mrefu, ukizingati mimi nilikuwa kwenye kiti namba 49 na 50.


Baada ya kushuka, nilielekea chooni na huko kulikuwa na foleni; tulirejea kwenye gari kwa kupitia sehemu iliyokuwa inauzwa vinywaji baridi (soda na juice), lakini cha kusikitisha nilipofika eneo ambalo basi lilikuwa limeegeshwa nilikuta basi limeondoka, nilipoangaza barabara kuu niliona basi likiondoka kwa umbali wa takribani mita 500; nilijaribu kutafuta usafiri wa pikipiki kwa lengo la kufuatilia basi hilo, nikitarajia wahudumu watapewa taarifa za kutokuwepo kwangu kutoka kwa mke wangu (ambaye nimwacha ndani ya basi) na abriria wengineo. Lakini hatukufanikiwa kulikuta basi hilo na kuamua kurejea pale katika hotel ya aljazera, nilielekezwa kumuona mtu mmoja (ambaye nafikiri ni mmoja kati ya wamiliki au watumishi wa hotel), nilimweleza kwamba nimeachwa na basi; hivyo nilitaka kufahamu uwezekano wa kupata usafiri mwingine; lakini mtu huyu alishangazwa na tabia hiyo ya basi la hood kuacha abiria katika hotel hiyo, kwani alidai ktk siku za karibuni takribani mara tatu wameacha abiria.


Nilifanikiwa kupata basi la Abood na kulipa nauli nyingine kuelekea mbeya. Nikiwa njiani nilifanikiwa kuwasiliana na mke wangu na kumshauri anisubiri katika ofisi la basi la hood kwani alikuwa mgeni kabisa ktk mji huo na hatukuwa na mwenyeji, kwani lengo la safari yetu ilikuwa kushiriki katika maonyesho ya Nanenane-Kanda ya kusini.


Nilifika Mbeya Mjini majira ya saa 3 usiku na kuelekea ofisi za Hood na kukutana na mke wangu ambaye alinitaarifu kwa kulikuwa na abiria takribani 6 ambao tuliachwa wakiwemo mama wenye watoto wachanga amba tulikaa nao jirani ndani ya basi hilo; pamoja na taarifa aliyotoa kwa wahudumu wa basi hilo juu ya kuacha abiria wengine, wahudumu hao hawakujali na walisema watapanda mabasi mengine. Kuna abiria mwingine ambaye alipanda basi jingine na walifanikiwa kulikuta basi la hood kabla ya kufika Iringa na walijaribu kulisimamisha basi hilo bila mafanikio, mpaka walipolikuta tena eneo la makambako; ambapo abiria huyu alikuwa na mtoto mchanga na aliacha kila kitu ndani ya basi la hood yakiwemo mahitaji ya muhimu kwa mtoto.


Mimi nilikuwa na mtoto wangu ambaye chakula chake kilikuwa ndani ya basi la hood, hivyo hakuweza kupata chakula na kulazimika kumpatia soda tu mpaka tulipofika Mbeya.


Nilipofika Mbeya nilikuta ofisi za basi la hood zimefungwa na kumkuta mke wangu nje ya ofisi hizo.


Tilkwenda kituo cha polis kwa ajili ya kutoa taarifa na tulielekezwa kwenda ofisi za trafic, ambapo tulipofika pale mapokezi baada ya kueleza kwa ufupi mkasa huo, walituomba kuonana na oSS - Ndimbo ili kumpatia maelezo hayo na ndipo OSS alipowapa maelekezo askari waliopo maelekezo kuchukua maelezo na kufungua jalada la unyanyasaji wa abiria.


Baada ya kuchukuliwa maelezo, tumeahidiwa kupigiwa simu kwa siku inayofuata (07.08.2013).

Ningependa kufahamu zaidi juu ya sheria husika na kama naweza kupata msaada wa kisheria zaidi; kulikuwa na chama cha kutetea haki za abiria, bali sifahamu wanatendaje kazi zao na wanapatikana wapi.

Wakati umefika wa kuchukua hatua badala ya kulalamika, nategemea michango ya mawazo yenu
 
Kwanza pole sana kaka,kampun ya hood kwa miaka ya nyuma ilikua inaaminika sana ila kwa sasa imekua hopeless kabisa,nadhan ni usimamizi tu mbovu,ila kingine unapaswa kwenda makao makuu ya hood morogoro,pale hakikisha unaonana na top wao au mzee suleiman hood,
sidhan kama ukituma e-mail swala lako lutafanyiwa kaz,lakin e-mail yao ni hood@morogoro.net
pia hili suala nadhan SUMATRA linawahusu hasa
 
Nakushukuru Mkoroshokigoli, nitatuma email hood; bali nashindwa kuelewa kwanini kwa muda mrefu tunashindwa kupata kampuni la usafirishaji lenye huduma za uhakika na endelevu; kwani makampuni mengi hutoa huduma nzuri kwa muda mfupi haswa mabasi yanapokuwa mapya.
 
YAH: UNYANYASAJI WA ABIRIA

Nimekuwa nikisafiri na mabasi yaendao mikoani na mara kwa mara nimekuwa nikishuhudia unyanyasaji wa abiria kwa namna moja au nyingine kutoka kwa wahudumu wa mabasi hayo, pamoja na lugha chafu; kwa sasa kumekuwa na tabia kwamba makondakta ndiyo wenye mamlaka juu ya basi husika kuliko dereva ambaye kwa mtazamo wangu naona kama ndio ana dhamana kubwa juu ya abiria.


Tarehe 06/08/2013, Mimi na mke wangu na mtoto wetu wa umri wa miaka mitatu (3) tulikuwa tunasafiri kutoka Dodoma kuelekea Mbeya Mjini kwa basi la Hood, ambapo tulipofika eneo la mbuyuni basi liliingia na kusimama katika mgahawa ujulikanao kwa jina la al-jazera na mhudumu wa basi alitaarifu abiria wote kwamba tuna muda wa dakika kumi (10) kwa ajili ya kupata chakula.


Abiria wengine walianza kushuka, nami pamoja na mtoto wangu tulivhukua uamuzi wa kushuka vile vile; lakini eneo la kupita abiria lilikuwa limejaa mizigo (vifurushi) hivyo kufanya zoezi la kushuka kwenye basi kuchukua muda mrefu, ukizingati mimi nilikuwa kwenye kiti namba 49 na 50.


Baada ya kushuka, nilielekea chooni na huko kulikuwa na foleni; tulirejea kwenye gari kwa kupitia sehemu iliyokuwa inauzwa vinywaji baridi (soda na juice), lakini cha kusikitisha nilipofika eneo ambalo basi lilikuwa limeegeshwa nilikuta basi limeondoka, nilipoangaza barabara kuu niliona basi likiondoka kwa umbali wa takribani mita 500; nilijaribu kutafuta usafiri wa pikipiki kwa lengo la kufuatilia basi hilo, nikitarajia wahudumu watapewa taarifa za kutokuwepo kwangu kutoka kwa mke wangu (ambaye nimwacha ndani ya basi) na abriria wengineo. Lakini hatukufanikiwa kulikuta basi hilo na kuamua kurejea pale katika hotel ya aljazera, nilielekezwa kumuona mtu mmoja (ambaye nafikiri ni mmoja kati ya wamiliki au watumishi wa hotel), nilimweleza kwamba nimeachwa na basi; hivyo nilitaka kufahamu uwezekano wa kupata usafiri mwingine; lakini mtu huyu alishangazwa na tabia hiyo ya basi la hood kuacha abiria katika hotel hiyo, kwani alidai ktk siku za karibuni takribani mara tatu wameacha abiria.


Nilifanikiwa kupata basi la Abood na kulipa nauli nyingine kuelekea mbeya. Nikiwa njiani nilifanikiwa kuwasiliana na mke wangu na kumshauri anisubiri katika ofisi la basi la hood kwani alikuwa mgeni kabisa ktk mji huo na hatukuwa na mwenyeji, kwani lengo la safari yetu ilikuwa kushiriki katika maonyesho ya Nanenane-Kanda ya kusini.


Nilifika Mbeya Mjini majira ya saa 3 usiku na kuelekea ofisi za Hood na kukutana na mke wangu ambaye alinitaarifu kwa kulikuwa na abiria takribani 6 ambao tuliachwa wakiwemo mama wenye watoto wachanga amba tulikaa nao jirani ndani ya basi hilo; pamoja na taarifa aliyotoa kwa wahudumu wa basi hilo juu ya kuacha abiria wengine, wahudumu hao hawakujali na walisema watapanda mabasi mengine. Kuna abiria mwingine ambaye alipanda basi jingine na walifanikiwa kulikuta basi la hood kabla ya kufika Iringa na walijaribu kulisimamisha basi hilo bila mafanikio, mpaka walipolikuta tena eneo la makambako; ambapo abiria huyu alikuwa na mtoto mchanga na aliacha kila kitu ndani ya basi la hood yakiwemo mahitaji ya muhimu kwa mtoto.


Mimi nilikuwa na mtoto wangu ambaye chakula chake kilikuwa ndani ya basi la hood, hivyo hakuweza kupata chakula na kulazimika kumpatia soda tu mpaka tulipofika Mbeya.


Nilipofika Mbeya nilikuta ofisi za basi la hood zimefungwa na kumkuta mke wangu nje ya ofisi hizo.


Tilkwenda kituo cha polis kwa ajili ya kutoa taarifa na tulielekezwa kwenda ofisi za trafic, ambapo tulipofika pale mapokezi baada ya kueleza kwa ufupi mkasa huo, walituomba kuonana na oSS - Ndimbo ili kumpatia maelezo hayo na ndipo OSS alipowapa maelekezo askari waliopo maelekezo kuchukua maelezo na kufungua jalada la unyanyasaji wa abiria.


Baada ya kuchukuliwa maelezo, tumeahidiwa kupigiwa simu kwa siku inayofuata (07.08.2013).

Ningependa kufahamu zaidi juu ya sheria husika na kama naweza kupata msaada wa kisheria zaidi; kulikuwa na chama cha kutetea haki za abiria, bali sifahamu wanatendaje kazi zao na wanapatikana wapi.

Wakati umefika wa kuchukua hatua badala ya kulalamika, nategemea michango ya mawazo yenu

Nenda SUMATRA Mbeya ipo uhindini eneo la Benki kwenye jengo la Benki ya Posta Tanzania. Mungu akutangulie
 
Nakushukuru Mkoroshokigoli, nitatuma email hood; bali nashindwa kuelewa kwanini kwa muda mrefu tunashindwa kupata kampuni la usafirishaji lenye huduma za uhakika na endelevu; kwani makampuni mengi hutoa huduma nzuri kwa muda mfupi haswa mabasi yanapokuwa mapya.

mzee hood ni katibu wa chama cha wamiliki wa mabasi tanzania(TABOA) na miez michache iliyopita nilimuona kwenye taarifa ya habar ITV akilalamika kuwa serikali inawaruhusu wawekezaji toka nje kuja kuwekeza Tanzania,wakat wao (TABOA) wana uwezo wa kuendesha huduma hiyo,sasa uzi wako unadhihirisha kuwa mzee hood analia tu kwakua hali imekua mbaya kwao,na miaka ya nyuma HOOD alikua ni bus operator wa east and central afrika,kwa sasa ukiondoa hayo mabas ya masafa ya mbali,hana mabas mazuri let say kwa Dar-Moro,
na waarabu wana tabia ya dharau sana hilo nalo ni tatizo,
 
HUDUMA BORA KWA MTEJA ni ngaja la kitaifa katika kuinua uchumi wa ndani, biashara nyingi zinazoendeshwa na sisi watz hazina mazingira rafiki kwa wateja wake; tunahitaji mabadiliko makubwa katika mfumo wa uendeshaji biashara zetu, vinginevyo tutabaki kulalamika kwamba wawekezaji kutoka nje wanachukua fursa ambazo tungeweza kutenda wenyewe.
 
Nasikitika kwamba mpaka siku naondoka Mbeya, tarehe 09.08.13 polisi hawajafanikiwa kuwasiliana nami kama walivyahidi; siku moja kabla ya kuondoka nilikwenda kituoni na kuuliza juu ya kinachoendelea na askari aliyepo hapo alinitaka kuwasiliana na OSS, niliwasilina nae na kunieleza kwamba nimpe muda kidogo na atawasiliana nami, bali mpaka leo sijapata kusikia kutoka kwake.

Napata shida na utendaji wa jeshi letu la polisi katika kushughulika na mambo mbalimbali, kwa kweli unapofika katika kituo cha polisi unaweza kuhisi kwamba hakuna system. Jeshi la polisi limekuwa likitoa wito kwa wanachi katika kutoa taarifa juu ya makosa mabalimbali yanayotokea barabarani.
 
Nasikitika kwamba mpaka siku naondoka Mbeya, tarehe 09.08.13 polisi hawajafanikiwa kuwasiliana nami kama walivyahidi; siku moja kabla ya kuondoka nilikwenda kituoni na kuuliza juu ya kinachoendelea na askari aliyepo hapo alinitaka kuwasiliana na OSS, niliwasilina nae na kunieleza kwamba nimpe muda kidogo na atawasiliana nami, bali mpaka leo sijapata kusikia kutoka kwake.

Napata shida na utendaji wa jeshi letu la polisi katika kushughulika na mambo mbalimbali, kwa kweli unapofika katika kituo cha polisi unaweza kuhisi kwamba hakuna system. Jeshi la polisi limekuwa likitoa wito kwa wanachi katika kutoa taarifa juu ya makosa mabalimbali yanayotokea barabarani.

polisi hawana system mdau,we fikiria hadi leo wanaandika taarifa kwenye daftari,hawana hata desktop,nenda ofisi ya upelelez sasa,hata pale central,utashangaa hawana hata keyboard,me huwana najiuliza hivi polis hii inafanyaje kazi??na je haiwezekani kuwa na miundombinu ya KISASA??hapo washachukua kitu kidogo,,,
 
Nilifanikiwa kuwasilina na SUMATRA - MBEYA na wametoa ushirikiano wa hali ya juu, kwani waliwasiliana na Manager wa HOOD - Mbeya naye alichukua uamuzi wa kunitafuta ambapo kwa sasa nilisharudi Dodoma, alitaka kufahamu kilichojiri na baadae aliniomba msamaha na kuwa tayari kunirejeshea gharama nilizopata na usumbufu; aliwasiliana na manager wa ofisi za hood hapa Dodoma naye aliniomba kufika ofisini kwao jioni ambapo ningeweza kukutana na kondakta wa basi nlilosafiri nalo. Nilifanikiwa kufika ofisini za hood Dodoma na manager alitoa ushirikiano na kusikitishwa na tukio hilo na waliweza kunirejeshea Tsh. 70,000/= ikiwa ni gharama za kulipa nauli ya basi na usumbufu.

WITO:

Tunaposafiri na kupata shida na watoa huduma hii, muhimu kutoa taarifa haswa kwa sumatra na polisi; kwani kuendelea kukaa kimya na kulalamika kunaendeleza tatizo badala ya kupunguza.
 
Nilifanikiwa kuwasilina na SUMATRA - MBEYA na wametoa ushirikiano wa hali ya juu, kwani waliwasiliana na Manager wa HOOD - Mbeya naye alichukua uamuzi wa kunitafuta ambapo kwa sasa nilisharudi Dodoma, alitaka kufahamu kilichojiri na baadae aliniomba msamaha na kuwa tayari kunirejeshea gharama nilizopata na usumbufu; aliwasiliana na manager wa ofisi za hood hapa Dodoma naye aliniomba kufika ofisini kwao jioni ambapo ningeweza kukutana na kondakta wa basi nlilosafiri nalo. Nilifanikiwa kufika ofisini za hood Dodoma na manager alitoa ushirikiano na kusikitishwa na tukio hilo na waliweza kunirejeshea Tsh. 70,000/= ikiwa ni gharama za kulipa nauli ya basi na usumbufu.

WITO:

Tunaposafiri na kupata shida na watoa huduma hii, muhimu kutoa taarifa haswa kwa sumatra na polisi; kwani kuendelea kukaa kimya na kulalamika kunaendeleza tatizo badala ya kupunguza.

pole sana na asante kwa kutufungua.tatizo ni kujua wap unaweza pata mawasiliano ya SUMATRA hasa unapopita kwenye miji midogo kama mafinga makambako au ipogolo.polisi nahisi wengi si msaada tena
 
mkuu HAKUNA pole sana kwa yaliyokukuta. Nashauri ufike wakati ambapo abiria ndo wawe na nguvu ya gari gani wanapaswa kutumia. Kwa kuwa umeshaeleza kinaga ubaga nini kimejiri katika safari yako na hakika watu wamekusoma tayari huu ni mwanzo mzuri wa kuelezea kero za huduma hizi za usafiri. Buyer beware.
Itasaidia kuwafanya watu wachague haya mabasi kwa umakini wanaposafiri. Natumai watatekeleza.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom