Huduma za Afya Musoma Vijijini: Zahanati Mpya 17 Zinaendelea Kujengwa

Huduma za Afya Musoma Vijijini: Zahanati Mpya 17 Zinaendelea Kujengwa

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

HUDUMA ZA AFYA MUSOMA VIJIJINI: ZAHANATI MPYA 17 ZINAENDELEA KUJENGWA

Huduma za Afya ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini, lenye Kata 21 zenye vijiji 68, zinaendelea kuboreshwa kwa ushirikiano mzuri kati ya Wananchi na Serikali yetu.

Vijiji 17 vya Jimboni mwetu vimeamua kujenga zahanati za vijiji vyao, na baadhi ya vijiji hivyo tayari vimeanza kupokea michango ya ujenzi wao kutoka Serikalini.

Huduma za Afya Jimboni mwetu:

(i) Hospitali mpya ya Halmashauri/Wilaya (1):
+Imejengwa kwenye Kitongoji cha Kwikonero, Kijiji cha Suguti, Kata ya Suguti

(ii) Idadi ya Vituo vya Afya (6):
+Vimejengwa kwenye Kata za Bugwema, Etaro (Kisiwa cha Rukuba), Kiriba, Makojo, Mugango na Murangi

(iii) Idadi ya Zahanati (28):
(a) 24 za Serikali
(b) 4 Binafsi
Zahanati za Serikali 24 ziko vijijini Bugoji, Bugunda, Bukima, Busungu, Bwai, Chitare, Etaro, Kiemba, Kigera Etuma, Kiriba, Kome, Kurugee, Kwikuba, Mkirira, Mmahare, Mwiringo, Nyakatende, Nyambono, Nyegina, Rusoli, Seka, Suguti, Tegeruka na Wanyere

Vijiji vinavyojenga zahanati mpya (16):
+Zinajengwa vijijini Bulinga, Burungu, Butata, Chimati, Chirorwe, Kaburabura, Kakisheri, Kataryo, Kwikerege, Kurukerege, Kurwaki, Mabuimerafuru, Maneke, Nyabaengere, Nyambono na Nyasaungu

WITO: UCHANGIAJI
Wadau wa Maendeleo, wakiwemo Wazaliwa wa Musoma Vijijini, wanaombwa wachangie ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya huduma za afya vijijini mwetu, ukiwemo ujenzi wa zahanati mpya - karibuni tuchangie sote!

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Jumatano, 18.9.2024
 
Back
Top Bottom