Huenda Feisal anataka kumtikia nje, Azam inahusishwa ili kupoteza maboya!

Huenda Feisal anataka kumtikia nje, Azam inahusishwa ili kupoteza maboya!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Mjadala wa sasa ni kuhusu Feisal kuondoka Yanga, huku akihusishwa kutaka kuhamia Azam FC. Sio yeye Feisal wala Azam Fc waliosema kuhusu Feisal kuhamia Azam Fc bali ni tetesi za mitandaoni za mashabiki.

Kwa udadisi wangu nahisi huu ni mchezo tu ili kutupoteza maboya, lakini lengo halisi la Feisal ni kutimkia nje ya nchi hususani Afrika kusini, Afrika kaskazini au Uarabuni.

Haya yote yanatokea kwa sababu viongozi wa Yanga wameendelea kumng'ang'ania Feisal bila kuwa na mpango bora wa maisha yake ya kisoka na kimaisha.

Nyuma ya pazia Azam FC inahusishwa kama plan B tu, yaani akiwa dili la Feisal kwenda nje litakwama au kuchelewa basi atatua Azam kwa mpito.

Upande wa pili, wakala wa Feisal kufanikisha hili deal huenda anahusishwa na mmoja wa kiongozi wa Yanga au Azam Fc.

Kilichotokea kwa George Mpole akiwa na klabu ya Geita Gold Mining huenda kinakwenda kutokea kwa Feisal.

Muda utatoa majibu.
 
Aende tu tunataka vijana wafike mbali waachane na timu za simba na yanga maneno maneno meeengi huku maslahi duni
 
Sio rahisi kwenda nje, hii ishu imefanywa na Azam wenyewe sema wameamua kukaa kimya na kuacha pesa iongee

Dickson Job tayari zishaanza tetesi tena huyu pesa itatolewa kwenye kidosho haina haja ya kwenda benki

Mayele naye yupo kwenye radar, huyu ndio mzito mzito na ndio silaha ya mwisho kwa Yanga

Baada ya hapo tutashuhudia kuiona ile Yanga ambayo tunaijua
 
Sio rahisi kwenda nje, hii ishu imefanywa na Azam wenyewe sema wameamua kukaa kimya na kuacha pesa iongee

Dickson Job tayari zishaanza tetesi tena huyu pesa itatolewa kwenye kidosho haina haja ya kwenda benki

Mayele naye yupo kwenye radar, huyu ndio mzito mzito na ndio silaha ya mwisho kwa Yanga

Baada ya hapo tutashuhudia kuiona ile Yanga ambayo tunaijua
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niko upande wa Feisal

Huwezi mlipa makambo milioni 10 halafu FEI mil 3

Fei nenda katafute majani mabichi

Na ukizipata fanya maendeleo yenye akili Soka huwa linaisha
 
Back
Top Bottom