Huenda Tanzania ya sasa chini ya Rais Magufuli ikawa imepata Waziri bora wa Elimu Ndalichako tokea Uhuru wake

Huenda Tanzania ya sasa chini ya Rais Magufuli ikawa imepata Waziri bora wa Elimu Ndalichako tokea Uhuru wake

Mzukulu

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2020
Posts
1,401
Reaction score
2,641
Yaani Watoto wamekaa karibia Miezi Mitatu bila Masomo, huku wengi Wao wakiwa tayari wameshaathirika Kisaikolojia kulingana na Hofu iliyokuwepo na bila shaka wengine hata Topiki zao hawakumaliza anatokea Mtanzania Mmoja anasema watafanya Mtihani yao Wiki chache zijazo.

Hivi hawa Watoto walitakiwa wajengwe Kwanza Kisaikolojia kutokana na Janga lililopo huku wakipewa muda wa Kujiandaa angalau hata Mwezi Mmoja ua Miwili au Waharakishwe Kufanya Mitihani yao kwa Shinikizo tu la Siasa na Maandalizi yetu ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kwa haya Maamuzi yaliyofanywa hivi leo nayaona mambo mawili Makuu ambapo kuna uwezekano Wanafunzi hawa Wakafeli kuliko ilivyowahi kutokea katika Historia ya Elimu (Taaluma) nchini au Wakafaulishwa (Wakabebwa) ili mradi tu Kuwahi muda na Kumfurahisha Mheshimiwa Rais JPM.

Taratibu sasa naanza Kuwadharau Wasomi Wetu wenye Doctorates (PhD's) zao na wenye Dhamana Kisiasa Nchini Tanzania.
 
Kwenye ile taarifa nakumbuka waliambiwa kidato cha sita watumie muda huo kujiandaa...,halafu mitihani wameambiwa watafanya juni 30,mwezi mmoja na masiku mbele....Sasa sijui wewe ulitaka mambo yaweje
 
Unataka niambia watoto wamemaliza miezi 3 nyumbani?

Lakini mkuu mbona serikali walitoa mwongozo watoto waendeleee na vipindi wakiwa nyumbani, pia kwa siku walizopewa kujiandaa kabla ya mthiani wao naona zinawatosha sana

Corona ilishaharibu utaratibu hatuna budi kukubali mabadiliko


It is never too late to begin. Start now
 
Kwenye ile taarifa nakumbuka waliambiwa kidato cha sita watumie muda huo kujiandaa...,halafu mitihani wameambiwa watafanya juni 30,mwezi mmoja na masiku mbele....Sasa sijui wewe ulitaka mambo yaweje
Tulitaka wanafunzi wapewe masomo za ziada kwa namna yeyote ile. Mfano mbunge wa Kenya Babu Owino amefanya tuition kadha online kuwasaidia wanafunzi. Hapa Babu anatiririka organic chem.
 
Toka Kabudi aseme katolewa jalalani kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Niliamini PhD katika taifa hili hazina maana yoyote
 
Kwenye ile taarifa nakumbuka waliambiwa kidato cha sita watumie muda huo kujiandaa...,halafu mitihani wameambiwa watafanya juni 30,mwezi mmoja na masiku mbele....Sasa sijui wewe ulitaka mambo yaweje
karudie kusoma utaelewa Alitaka wafanyaje
 
Ila kiukweli muda uliotolewa ni mdogo sana,, mitihani inatakiwa maandalizi ya kutosha.. Kuna wanafunzi wanasoma mbali na mazingira ya kwao.. So inabid watumie mda kusafiri hadi shule.. Sasa kabla hata ya kuzoea tena mazingira ya Shule mara paaap pepa hilo..
Poleni sana form 6 mkapambane tu
 
Unajua hawa wanafosi waendane na ratiba iliyozoeleka, kitu ambacho hakiwezekani kiukweli miezi miwilinna nusu tuliyopoteza ni mda mwingi kiukweli..
Ilipaswa watoto wapewe atleast 1.5 month then wapige pepa..
Kwa mwaka huu ulivyo hata mda was kuomba vyuo utasogea mbele na hata mda was kuingia vyuo vikuu utasogea mbele..
 
Tulitaka wanafunzi wapewe masomo za ziada kwa namna yeyote ile. Mfano mbunge wa Kenya Babu Owino amefanya tuition kadha online kuwasaidia wanafunzi. Hapa Babu anatiririka organic chem.

Yaani A level uifundishe hivyo Utube!!! Ulipita Advance?
 
Niamini tu kuwa uko kwenye sekta ya Elimu kuhoji hivyo, la sivyo umekurupuka.

Hata vile, hongera kwa hisia zako hizo zichukuliwe na Wizara kama changamoto inapojiandaa kuwarudisha wanafunzi wa kidato cha sita, kama alivyoelekeza Rais Magufuli.
 
Back
Top Bottom