Huenda tukaacha ufugaji

Huenda tukaacha ufugaji

mwanyaluke

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2015
Posts
704
Reaction score
2,435
Nimekuwa nafuga kwa miaka mingi sasa , kiufupi nimerithi hii shughuli , kinachoshangaza ni kunishitua ni gharama za ufugaji zinapanda hadi sio vizuri hapa nazungumzia ufugaji wenye akili sio ule wa kisukuma na kimasai 1.bei ya mifugo mfano bei ya ndama dume wa kisasa mwenyew wiki Moja ni elfu 50000 to laki Moja , then bei zinaenda juu kutegemea na umri na hali yake kiafya 2. Bei ya ndama jike ni laki nne huyo ni mwenye miezi mitatu kwenda juu kutegemea na umri na hali yake kiafya,. 3 jichanganye kutafuta mitamba na ngombe wa maziwa bei zinakatisha tamaa, mfano mzungu pale iringa Philips anauza hadi Milion Tano. Hizo bei za mifugo then let's turn kwenye malisho , lipa mfanyakazi , nunua pumba , nunua mashudu, nunua madini, pelaka maji , na kibaya kuliko vyote serikali imeruhusu watu kutoka nje kununua hizo supplement mfano ukingia sasa mbeya, mbarali , tunduma wamejaa maa agents wanakusanya pumba wanapatia wakenya , na mbaya zaidi product za mifugo yetu zinapata ushindani toka nje yaani Tanzania wanagiza maziwa, nyama za kopo etc matokeo yake tunauza na kupata faida kidogo sana, yaani unaweka Milion hamsini unapata faida Milion mbili na kama ununuzi wa concentrate kama pumba, mashudu utaendelea hivi wengi tunaenda kimbia
 
Nimekuwa nafuga kwa miaka mingi sasa , kiufupi nimerithi hii shughuli , kinachoshangaza ni kunishitua ni gharama za ufugaji zinapanda hadi sio vizuri hapa nazungumzia ufugaji wenye akili sio ule wa kisukuma na kimasai 1.bei ya mifugo mfano bei ya ndama dume wa kisasa mwenyew wiki Moja ni elfu 50000 to laki Moja , then bei zinaenda juu kutegemea na umri na hali yake kiafya 2. Bei ya ndama jike ni laki nne huyo ni mwenye miezi mitatu kwenda juu kutegemea na umri na hali yake kiafya,. 3 jichanganye kutafuta mitamba na ngombe wa maziwa bei zinakatisha tamaa, mfano mzungu pale iringa Philips anauza hadi Milion Tano. Hizo bei za mifugo then let's turn kwenye malisho , lipa mfanyakazi , nunua pumba , nunua mashudu, nunua madini, pelaka maji , na kibaya kuliko vyote serikali imeruhusu watu kutoka nje kununua hizo supplement mfano ukingia sas mbeya, mbarali , tunduma wamejaa maa agents wanakusanya pumba wanapati wakenya , na mbaya zaidi product za zinazorishwa.na mifugo yetu zinapata ushindani toka nje yaani Tanzania wanagiza maziwa, nyama za kopo etc matokeo yake tunauza na kupata faida kidogo sana

Pumba kwenda Kenya ni pasua kichwa
 
Pumba kwenda Kenya ni pasua kichwa
Sijui wanawaza nini , Huwa sielewi mchango wa serikali ni nini kwenye mifugo ,gari imetoka Malawi Nimeamua kuja na pumba ACHa dereva wangu wabishane na watu wa mpakani hadi uwape kitu chochote,
 
nipende kukuambia changamoto yako inaanzia hapa..... usije kamwe ukaona mwenzako anachofanya ni ujinga hao unaosema wamasai na wasukuma kila siku wanapeleka mifugo mjini inauzika vizuri ww fuga hapo na masapulimenti utacheka kijapani
Sikejeli ila inawaumiza sana , ngombe kumi za msukuma sawa na ngombe moja wa kisasa, huyu wa kisasa anakupa muda wa kufanya na shughuli nyingine. Yule una mchunga porin anakula muda wako unaelewa nini wanaposema time is money
 
Unachoongea ni ‘Fallacy’, wewe kama ni mfugaji kweli, kwanini ulalamike bei ya ndama na mitamba kuwa juu? Hii ni sawa na mkulima kulalamika bei ya mahindi kuwa juu. Wewe sio mfugaji, ni mnunuzi wa mazao ya ufugaji, acha wafugaji wapige pesa kuuza ndama na mitamba kwa bei kubwa, maana bei ikishuka watakuja kulia huku kama wewe..
 
Sikejeli ila inawaumiza sana , ngombe kumi za msukuma sawa na ngombe moja wa kisasa, huyu wa kisasa anakupa muda wa kufanya na shughuli nyingine. Yule una mchunga porin anakula muda wako unaelewa nini wanaposema time is money
ukijikuta mtu wa nahesabu sana utabaki kulalamika kila siku wenzako wanapiga pesa na mfugaji hahitaji mambo mengine ndio maana muda wote anatembea na mali zake nyie mnaojidai wa maofisini na mnataka kufuga endeleeni kupambana sana mkifika mmechoka
 
Unachoongea ni ‘Fallacy’, wewe kama ni mfugaji kweli, kwanini ulalamike bei ya ndama na mitamba kuwa juu? Hii ni sawa na mkulima kulalamika bei ya mahindi kuwa juu. Wewe sio mfugaji, ni mnunuzi wa mazao ya ufugaji, acha wafugaji wapige pesa kuuza ndama na mitamba kwa bei kubwa, maana bei ikishuka watakuja kulia huku kama wewe..
mkuu una pointi nzuri sana hawa jamaa wanaojidai wafugaji wa kisasa na hawana mitaji lazima walalamike ila wale wanaowaona wanafuga kishamba kila siku wanaingiza pesa sasa najiuliza mleta mada na hao wasukuma nani ataachwa nyuma
 
Kama umeamua kufunga kisasa jikite kwenye misingi ya ufugaji wa kisasa, tafuta eneo la kutosha, zalisha chakula mwenyewe, Kuna shamba la serikali Kibaha wanauza mbegu za malisho nunua otesha. Kuwa na maji ya kutosha mwisho tafuta masoko.
Usifuge Ng'ombe 4 ukajiita mfugaji wa kisasa
 
Back
Top Bottom