Hukumu ya kesi inayowatuhumu Watu wanaodaiwa kutaka kuchoma Soko la Karume kusomwa Julai 19, 2024

Hukumu ya kesi inayowatuhumu Watu wanaodaiwa kutaka kuchoma Soko la Karume kusomwa Julai 19, 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Glory Nkwera ameiahirisha hukumu aliyotaka kuisoma leo Juni 28, 2024 katika kesi ya tishio la kuchoma Soko la Karume Jijini inayomkabili Christina Elisha na mwenzake, Mashauri Ulomi.

Glory ameahirisha kusoma hukumu hiyo kwa maelezo kuwa uandaaji wa hukumu hiyo haujakamilika na hivyo hukumu hiyo hiyo imepangwa kusoma Julai 19, 2024.

Katika kesi hiyo Namba 313 ya Mwaka 2023, Christina na mwenzake, Mashauri Ulomi wanashtakiwa na Jamhuri, Mahakamani hapo kwa tishio la kuchoma Soko la Karume mapema Mwaka 2023, tukio ambalo liliibuiliwa na walinzi wenye mbwa waliokuwa lindo sokoni hapo.

Pia soma
~ CCTV Camera zafungwa Soko la Mchikichini Karume (Dar) kubaini wanaochoma moto masoko
~ Amos Makalla: Chanzo cha moto wa soko la Karume ni mshumaa uliowashwa na mateja
 
Back
Top Bottom