Humphrey Polepole: Tume ya katiba yashupalia pendekezo la kuundwa kwa serikali tatu

Humphrey Polepole: Tume ya katiba yashupalia pendekezo la kuundwa kwa serikali tatu

K-Boko

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2013
Posts
697
Reaction score
218
Bw. Humphrey Polepole, mjumbe wa Tume ya Katiba, leo ameibua siri ya Tume kushupalia pendekezo la kuundwa kwa serikali tatu. Amesema Wazanzibar walikuja na Katiba Mpya mwaka 2010 yenye mabadiliko mengi dhidi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano yakiwemo yale yanayobainisha Zanzibar ni nchi kamili na ina Rais wake!

Mwanajopo katika kipindi cha cha Hoja cha Star TV, Bw. Joseph Leonard Mkinga akamjibu Polepole kuwa Katiba hiyo ya Zanzibar ilikuja kutokana na udhaifu wa viongozi wa Serikali ya Muungano kuwaacha viongozi wa Zanzibar kuja na Katiba hiyo yenye kuidhoofisha Katiba ya Muungano.

Mkinga pia alimhoji Polepole kuhusu idadi ya Watanzania waliopendekeza serikali tatu ambapo kwa kweli Polepole alijikanyaga tu! Suala zito kama la kupendekeza serikali tatu litatolewaje na wananchi 18,000 tu?

Hoja zote za Mkinga zina mashiko mazito na ukijumlisha na onyo la Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kuhusu kuuchezea muungano--ni wazi kabisa Tume ya Katiba inataka kutuletea majanga ya 'ukabila' utakaoigawa nchi vipande na kutuletea vurugu kubwa itakayoishia sio tu kutugawa Watanzania kati ya Zanzibar na Tanganyika, lakini pia hata hao Watanganyika na Wazanzibar hawatabaki salama kama alivyoonya Mwalimu!!

Alionya kuwa dhambi ya ubaguzi itaendelea kututafuna!!! Watanzania tuwe makini, ina maana udhaifu wa viongozi wa serikali ya muungano uliosababisha viongozi wa Zanzibar kuja na katiba ya mwaka 2010 yenye kuivuruga Katiba ya Muungano iwe ndio sababu ya kuibuka na serikali tatu ambazo hatimaye muundo huo utaivunja Tanzania?

Hasira dhidi ya viongozi wa Zanzibar ndio upelekee kuivunja nchi? Ina maana tumeshindwa kabisa kuzungumza na viongozi wa Zanzibar au Wazanzibar ili kuirekebisha katiba yao ya 2010 na tukarudi kuiheshimu Katiba ya Muungano ambayo hadi sasa inaonyesha wazi Zanzibar ni sehemu ya Tanzania? Je tumeshindwa kuzungumza na sasa suluhisho ni kuibuka na serikali tatu?

Tukumbuke sababu ya lile kundi la 45 miaka ile ya 90 kuwa ilikuwa ni hasira dhidi ya viongozi wa Zanzibar kuichokonoa Katiba ya Muungano. Hoja ile iliuawa na Mwalimu kwa uwezo wake binafsi (single handedly) na nchi ikatulia! Yaani sababu sasa ya kuibuka na serikali tatu ni kukosekana kwa 'Mwalimu' wa enzi hizi?

Tujifunze kutokana na misemo ya wahenga--hasira hasara!! Samahani kwa 'mkeka' huu--nimeshindwa kabisa kuifupisha hoja hii.

Nawasilisha!!
 
Boraa tu hawa wajumbe wa Tume wamemaliza muda wao. sasa ni zamu ya bunge la katiba
 
Acha kutaka kupotosha watu Hoja juu ya serikali tatu si hoja ya Tume ya Katika mimi ni mmoja wa niliohudhuria baadhi ya mikutano waliyokuwa wakiifanya Tume katika maeneo mbalimbali ya nchi hii ni wananchi wengi hususani wale wasio wanaCCM walikuwa wakitoa mapendekezo ya muundo wa Serikali Tatu, kwa hiyo tambua haya ni maoni ya Watanzania wengi ambao kwa sasa ndio wengi kuliko wanaCCM ambao wao wananchojali ni matakwa ya CCM tu hata kama hayana manufaa na msingi wowote kwa ustawi na afya ya Taifa hili.
 
"GIVE PEOPLES WHAT THEY WANTS"70th politics cant have a chance today! PEOPLES ARE AWAKE! YOU SHALL NEVER BRUT,BULLING OR KIDDING ALL THE TIME,IT'S TIME NOW TO ENDURE CCM BRUTALLITY AND GIVE A NEW PROSPERITY TO ALL OF US TANZANIANS
 
Hoja za Mkinga zinapwaya kidogo kwani uchambuzi wake unatumia nguvu ya kufoka na kidogo mantiki. Anaelezea mapungufu ya serikali tatu kwasabau tuu inavunja hati ya muungano na kwamba idadi ya watu waliosema wanataka serikali tatu katka repoti ya ziada ya warioba bni wacache. hakiaka nimeshangaa huyu mwanasayansi ya siasa wmenzangu uelewa wake wa mbinu za utafit ni finyu kiasi hicho.

Mimi nadhani waTanzania tujadili hoja bila kuanza kujikita kwenye kudumisha fikra tuu. Hoja ya kwamba serikali tatu itakuwa na gharama kubwa ilijibiwa na Pole pole kwa utulivu na uelewa mkubwa kushinda ufokaji wa bwana Mkinga. demokrasis ya kweli na inayolenga kujenga ustawi wa watu inagharima. Mifumo mizuri ya uwajibikaji iliyowekwa katika rasimu ya pili ya katiba kama itatekelezwa vizuri itapanua ushiriki wa wananchi katika uchumi, siasa na jamii na hivyo kuongeza pato la taifa litakalo gharamia mifumo hii mipya ya demokrasis ikijumlisha mfumoa wa seikali tatu. Kukataa mifuomo mizuri ya demokrasis kwa kutumia kigezo cha gharama ni sawa na kuogopa mtoto wako asikue eti ataongeza ghrama maana atavaa gauni ama suruali ya bei kubwa. Gharama ya kuendelea na mfumo wa serikali mbili ambayo kila pande inavizia na kutegea mwingine ni kubwa kwa ustawi na maendelea ya pande zote hivyo tukatae wale wanaotupotosha kwa maslahi ya kulinda ukubwa na mamlaka hewa yanayotolewa na serikali mbili.

Polepole amenukuu vifungu vya katiba zote mbili vinavyodhoofisha Muungano. Zanibar ni nchi ndani ya nchi, huwezi kuwa na Muungano ambapo moja nii nchi na nyingine si nchi bali muungano. Polepole alinukuu utafiti wa mapato na jinsi mgawanyo kwa kuendesha serikali mbili unagandamiza nyingine. Mkinga aliacha domo wazi tuu a kurudia kufoka bila sababu. Tunahitaji staha katika kuchangia mada ili wananchi waelewe tofauti ya kelele na hoja.

Nimechoka zaidi Mkinga pale anaposema ama serikali mbili au moja. Serikali moja haiwezzekanai, kwasababu Zanzibar ni nchi huru na iheshimiwe kwa hilo. Serikali mbili tumeishi nayo miaka hii yote na imeturudisha nyuma kimaendelea kwasisa za kutegeana, kutegemeana, kulaumiana na kuviziana. Pili hoja ya Mkinga kwamba hati ya Muungano ifuatwe jamani yeye alikuwa haelewi manung'uniko ya pande zote kuhusu Muungano? Ofcourse Mkinga anahoja kwamba Bunge la Katika halitapisha hoja ya serikali tatu kwasababu ya uwing wao katika bunge la Katiba. Labda sisi wanaharakati tuendelee kuwaelimisha wabunge wa CCM kwamba hatima ya nchi yetu iko mikononi mwa na wapige kura wakiiweka nchi mbele maana vyama vinakufa lakini nchi ikilindwa haifi.

Mwisho, tuenedelee kujielemisha kuhusu swala la Muungano pasi kufuata ushabiki wa watu wenye mawazo ya kizamani kiasi kwamba hoja yao kubwa ni kuwatuhumu kina Jaji warioba kwamba mbona hawakusema naneno hayo wa serikali 3 wakati Malimu akiwa hai. Sasa jamni wakati ndo huu wa kusema kwa hiyo jaji Warioba na sisi waTanzania wengine tufiche mawazo yetu eti tuu hatukusema Mwalimu akiwepo. Nani asiyejua kwamba wakati na mahali ni vgezo muhimu katika kutoa mmamuzi kwa mwanadamu? leo hii tunazungumzi haki za watoto, kina mama na nk lakini mpaka miaka ya 1978 nhci nyingine wanawake na watoto hawakuwa watu na hivyo hawakustahili kupika kura katika nchi zao. sasa kwavile hatukusema haki za akina Mama miaka ya 70 hivyo sasa tusiseme? Jamani tupanuke mafikira yetu
 
Mwanzisha huu uzi Ndg. K-boko una agenda ya siri otherwise unge- declare interest before. Unaituhumu tume kuwa inashupalia serikali tatu, nå kwamba inaleta mgawanyiko katika Muungano. Wakati awali unasema katiba ya Zanzibar ya 2010, ndiyo chimbuko la madai ya serikali tatu. Huoni kama hoja yako inajichanganya yenyewe? acha kupotosha Umma kwamba tume inalazimisha serikali tatu. Watanganyika wakati umefika sasa nå.tunajua nini tunataka. Nå hakuna chama cha siasa kitakachoamua mustakabali wa hili, bali ni sisi Watanganyika. Kwa kuwa Wanzibar walianza kutubagua hadharani toka 2010. Viva Tanganyika
 
ndugu polepole nimemsikiliza amefafanua hoja zote kwa weledi mkubwa sana,na kwa kuwa CCM walishakalilishwa kuwa ni serikali 2 hawana hoja zaidi ya kumtumia mwalimu nyerere kama ni ngao yao mimi nadhani kama kweli ccm wana upenda na kuunga mkono muungano wao wangesema serikali 1 hapo ndipo wangekuwa kweli ni wapigania muungano lakini kwa kungangania serikali 2 ni vyeo tu na madaraka wanangangania
 
Mkinga pia alimhoji Polepole kuhusu idadi ya Watanzania waliopendekeza serikali tatu ambapo kwa kweli Polepole alijikanyaga tu! Suala zito kama la kupendekeza serikali tatu litatolewaje na wananchi 18,000 tu?


Huyu bwana Mkinga nae upeo wake wa kutafakari ni wakutiliwa shaka. Kwani tume iliweka limitations za idadi ya wananchi kutoa maoni? Hao 18,000 ndiyo proportion kubwa kati ya watoa maoni waliochangia kuhusu muungano.

Halafu mbona anashangaa idadi hiyo ndogo kutoa maoni juu ya katiba na hashangai uchaguzi wa rais kujumuisha takribani watu 8mil pekee kati ya raia walioandikishwa zaidi ya 20mil? Hata ingelikuwa tume imepewa miaka 10 kukusanya maoni si kila raia angekuwa interested kutoa maoni. Na hata tuseme tuanze tu na kura ya maoni kuhusu muungano still utakuta less than 50% ya eligible voters ndiyo watakaopiga kura hiyo, hiyo ni social behaviour ya binadamu popote pale.
 
Mwanzisha huu uzi Ndg. K-boko una agenda ya siri otherwise unge- declare interest before. Unaituhumu tume kuwa inashupalia serikali tatu, nå kwamba inaleta mgawanyiko katika Muungano. Wakati awali unasema katiba ya Zanzibar ya 2010, ndiyo chimbuko la madai ya serikali tatu. Huoni kama hoja yako inajichanganya yenyewe? acha kupotosha Umma kwamba tume inalazimisha serikali tatu. Watanganyika wakati umefika sasa nå.tunajua nini tunataka. Nå hakuna chama cha siasa kitakachoamua mustakabali wa hili, bali ni sisi Watanganyika. Kwa kuwa Wanzibar walianza kutubagua hadharani toka 2010. Viva Tanganyika

Unajibu hoja yangu bila ku-declare interest zako lakini mimi unataka ni-declare interest--binadamu bana kwa kujipenda! Kwanza kabisa lazima niseme hiyo headline sio yangu--mods wameibadili headline yangu iliyokuwa ikisema hivi: "Wariobana na wenzako; hasira hasara!" hata sielewi nini mantiki ya kuibadili headline yangu!! Anyway, nirudi kwenye hoja yako--je kama Wazanzibar wameibuka na katiba ya mwaka 2010 hatuna njia nyingine ya kuwadhibiti Wazanzibar wasivunje katiba ya Muungano ila kwa kuanzisha serikali tatu? Mantiki ya hoja yangu ni kwamba muungano wa serikali tatu hauna mashiko kiutawala na ni rahisi mno kuuvunja--unless tuseme wazi kwamba hatuutaki muungano--lakini huwezi kusimama imara mbele za watu wazima wenye akili ukasema muungano wa serikali tatu utakuwa imara kuliko huu wa sasa. Muungano wa serikali tatu unaweza kuvunjwa kwa urahisi mno na mtu mmoja upande mmoja ambaye ameamka asubuhi kutoka Ikulu akili haiko sawasawa siku hiyo na akaamua tu kuwa hakuna muungano na ikawa hivyo!! Ukiniambia muungano imara ni wa serikali moja nitakuelewa Mkubwa, jambo ambalo wengi wanakiri sio rahisi kwa sasa!!
 
Hoja za Mkinga zinapwaya kidogo kwani uchambuzi wake unatumia nguvu ya kufoka na kidogo mantiki. Anaelezea mapungufu ya serikali tatu kwasabau tuu inavunja hati ya muungano na kwamba idadi ya watu waliosema wanataka serikali tatu katka repoti ya ziada ya warioba bni wacache. hakiaka nimeshangaa huyu mwanasayansi ya siasa wmenzangu uelewa wake wa mbinu za utafit ni finyu kiasi hicho.

Mimi nadhani waTanzania tujadili hoja bila kuanza kujikita kwenye kudumisha fikra tuu. Hoja ya kwamba serikali tatu itakuwa na gharama kubwa ilijibiwa na Pole pole kwa utulivu na uelewa mkubwa kushinda ufokaji wa bwana Mkinga. demokrasis ya kweli na inayolenga kujenga ustawi wa watu inagharima. Mifumo mizuri ya uwajibikaji iliyowekwa katika rasimu ya pili ya katiba kama itatekelezwa vizuri itapanua ushiriki wa wananchi katika uchumi, siasa na jamii na hivyo kuongeza pato la taifa litakalo gharamia mifumo hii mipya ya demokrasis ikijumlisha mfumoa wa seikali tatu. Kukataa mifuomo mizuri ya demokrasis kwa kutumia kigezo cha gharama ni sawa na kuogopa mtoto wako asikue eti ataongeza ghrama maana atavaa gauni ama suruali ya bei kubwa. Gharama ya kuendelea na mfumo wa serikali mbili ambayo kila pande inavizia na kutegea mwingine ni kubwa kwa ustawi na maendelea ya pande zote hivyo tukatae wale wanaotupotosha kwa maslahi ya kulinda ukubwa na mamlaka hewa yanayotolewa na serikali mbili.

Polepole amenukuu vifungu vya katiba zote mbili vinavyodhoofisha Muungano. Zanibar ni nchi ndani ya nchi, huwezi kuwa na Muungano ambapo moja nii nchi na nyingine si nchi bali muungano. Polepole alinukuu utafiti wa mapato na jinsi mgawanyo kwa kuendesha serikali mbili unagandamiza nyingine. Mkinga aliacha domo wazi tuu a kurudia kufoka bila sababu. Tunahitaji staha katika kuchangia mada ili wananchi waelewe tofauti ya kelele na hoja.

Nimechoka zaidi Mkinga pale anaposema ama serikali mbili au moja. Serikali moja haiwezzekanai, kwasababu Zanzibar ni nchi huru na iheshimiwe kwa hilo. Serikali mbili tumeishi nayo miaka hii yote na imeturudisha nyuma kimaendelea kwasisa za kutegeana, kutegemeana, kulaumiana na kuviziana. Pili hoja ya Mkinga kwamba hati ya Muungano ifuatwe jamani yeye alikuwa haelewi manung'uniko ya pande zote kuhusu Muungano? Ofcourse Mkinga anahoja kwamba Bunge la Katika halitapisha hoja ya serikali tatu kwasababu ya uwing wao katika bunge la Katiba. Labda sisi wanaharakati tuendelee kuwaelimisha wabunge wa CCM kwamba hatima ya nchi yetu iko mikononi mwa na wapige kura wakiiweka nchi mbele maana vyama vinakufa lakini nchi ikilindwa haifi.

Mwisho, tuenedelee kujielemisha kuhusu swala la Muungano pasi kufuata ushabiki wa watu wenye mawazo ya kizamani kiasi kwamba hoja yao kubwa ni kuwatuhumu kina Jaji warioba kwamba mbona hawakusema naneno hayo wa serikali 3 wakati Malimu akiwa hai. Sasa jamni wakati ndo huu wa kusema kwa hiyo jaji Warioba na sisi waTanzania wengine tufiche mawazo yetu eti tuu hatukusema Mwalimu akiwepo. Nani asiyejua kwamba wakati na mahali ni vgezo muhimu katika kutoa mmamuzi kwa mwanadamu? leo hii tunazungumzi haki za watoto, kina mama na nk lakini mpaka miaka ya 1978 nhci nyingine wanawake na watoto hawakuwa watu na hivyo hawakustahili kupika kura katika nchi zao. sasa kwavile hatukusema haki za akina Mama miaka ya 70 hivyo sasa tusiseme? Jamani tupanuke mafikira yetu

Ndugu yangu, kwanza sikuzungumzia gharama katika hoja yangu. Pili, hata kama Polepole amenukuu vifungu vinavyodhoofisha muungano, narudi kwenye hoja, suluhu rahisi ni serikali tatu? Tatu, kuhusu manung'uniko, narudi palepale, suluhu rahisi ni serikali tatu? Nne, umesema kutetea muungano uliopo ni "mawazo ya kizamani"--swali rahisi tu--unaachana na mawazo mazuri kwa sababu tu wewe (na wenzako) unadhani ni ya zamani? Lakini kama utadhani mawazo hayo ni ya zamani utabadili mawazo mangapi ndugu yangu? Au hujui katika taifa lolote makini kuna Mambo ya MSINGI?
 
Back
Top Bottom