Hussein Bashe na ndoto za kufikirika, za kumbadili kuku wa kisasa kuwa wa kienyeji

Hussein Bashe na ndoto za kufikirika, za kumbadili kuku wa kisasa kuwa wa kienyeji

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Ninae huyu mtu anaeitwa Hussein Bashe, Kwa mlio karibu nae jaribuni kumuonya kwamba hicho kilimo anachojaribu kukianzisha, kimeshashindwa hata kabla hakijaanza .labda kwa sababu yeye ni mtu anaedhani kilimo kinaendeshwa kwa makaratasi, hivyo anajaribu kutoa mishipa ya shingo kwa kuongea sanaaa. Akijua ndio kilimo chenyewe.

Kwanza waliopewa nafasi hizo sio wakulima Kwa asili, ni vijana tu ambao wamesikia hekari zinagawiwa wamezikimbilia, ila vijana wenyewe wanaoishi kwa kilimo na wanailisha nchi tangia tupate uhuru hawajaguswa hata Mmoja. Kilimo hakiitaji makaratasi Bali asili ya mtu, kilimo ni asili usipokuwa nayo hata ukipewa zana zote hautaweza.

Na Rais amehadaika na hayo makaratasi ya Bashe anamwaga mamilioni ya pesa ambayo hata hivyo hayatakuwa na tija yoyote, nasema hayatakuwa na tija kwa sababu waliopelekwa sio wakulima ,wakulima hawajafikiwa na kilichofanyika ni kumlazimisha kuku wa kisasa akajitafutie chakura, nasema Tena mpango huu ungepelekwa kwa wakulima wanaozalisha mahindi Huko rukwa na ruvuma, kwa miaka yote wao wapo shambani hawategemei makaratasi, wao kilimo ndio maisha Yao.

Bashe anajaribu kutuingiza mjini kwa mradi huu ambao kufika 2025 hautakuwepo na hayo mashamba yatabaki mapori ya wanyama na hayawani. Kama mnataka Mali mtaipata shambani. Nendeni kwa wenye asili na kilimo mkawape sapoti ya kutosha mtaona matokeo lakini hii propaganda mnayojaribu kuileta hamtaweza mtakwama, narudia katika hili Nina uhakika mabilioni ya pesa yanaenda kupotea.
 
Ninae huyu mtu anaeitwa Hussein Bashe, Kwa mlio karibu nae jaribuni kumuonya kwamba hicho kilimo anachojaribu kukianzisha, kimeshashindwa hata kabla hakijaanza .labda kwa sababu yeye ni mtu anaedhani kilimo kinaendeshwa kwa makaratasi, hivyo anajaribu kutoa mishipa ya shingo kwa kuongea sanaaa ! Akijua ndio kilimo chenyewe!
Siku zote muda ni mwalimu mzuri let's wait & see.
 
Bila hizi project tutapataje hela.

Kuandaa hekta moja ni zaid ya mil 16, hapo hujapanda, hujapalilia, huja prune, hujapiga dawa na wala hujavuna na bado hujapeleka sokoni.... sasa piga mara 800😂
Hayo mazao sijui yatauzwa wapi ili ya break even.
 
We've to be optimistic but isn't severely
 
Ninae huyu mtu anaeitwa Hussein Bashe, Kwa mlio karibu nae jaribuni kumuonya kwamba hicho kilimo anachojaribu kukianzisha, kimeshashindwa hata kabla hakijaanza .labda kwa sababu yeye ni mtu anaedhani kilimo kinaendeshwa kwa makaratasi, hivyo anajaribu kutoa mishipa ya shingo kwa kuongea sanaaa. Akijua ndio kilimo chenyewe.

Kwanza waliopewa nafasi hizo sio wakulima Kwa asili, ni vijana tu ambao wamesikia hekari zinagawiwa wamezikimbilia, ila vijana wenyewe wanaoishi kwa kilimo na wanailisha nchi tangia tupate uhuru hawajaguswa hata Mmoja. Kilimo hakiitaji makaratasi Bali asili ya mtu, kilimo ni asili usipokuwa nayo hata ukipewa zana zote hautaweza.

Na Rais amehadaika na hayo makaratasi ya Bashe anamwaga mamilioni ya pesa ambayo hata hivyo hayatakuwa na tija yoyote, nasema hayatakuwa na tija kwa sababu waliopelekwa sio wakulima ,wakulima hawajafikiwa na kilichofanyika ni kumlazimisha kuku wa kisasa akajitafutie chakura, nasema Tena mpango huu ungepelekwa kwa wakulima wanaozalisha mahindi Huko rukwa na ruvuma, kwa miaka yote wao wapo shambani hawategemei makaratasi, wao kilimo ndio maisha Yao.

Bashe anajaribu kutuingiza mjini kwa mradi huu ambao kufika 2025 hautakuwepo na hayo mashamba yatabaki mapori ya wanyama na hayawani. Kama mnataka Mali mtaipata shambani. Nendeni kwa wenye asili na kilimo mkawape sapoti ya kutosha mtaona matokeo lakini hii propaganda mnayojaribu kuileta hamtaweza mtakwama, narudia katika hili Nina uhakika mabilioni ya pesa yanaenda kupotea.
Kwenye hili nakubaliana nawe kwa 100%. Huu mradi ni upotevu mkubwa wa pesa za wananchi.

Tafiti zote Duniani zinaonesha kuwa ukitaka mradi fulani ufanikiwe ni lazima uanzie kwa wahusika na siyo uwapelekee. Mradi wa kuwapelekea watu unakuwa hauna ownership ya wahusika.

Hii pesa ambayo sasa hivi inapelekwa kwenye hicho kilimo cha kufikirika ingepelekwa kwa watu ambao tayari wana ownership kwenye kilimo, ingefanya mambo makubwa na ingeleta positive impact kubwa sana. Mafanikio ya hao ambao tayari wapo kwenye kilimo yangewavuta wengi kuingia kwenye kilimo. Wakishaingia tayari kwenye kilimo ndipo wanakutana na mkono wa msaada wa Serikali. Serikali kazi yake ingekuwa kuwahamasisha vijana kuingia kwenye kilimo kwa kuwaonesha mafanikio ya wale wenzao ambao wapo kwenye kilimo.

Kinachofanyika sasa ni upotevu mkubwa wa pesa ya wananchi. Kama alivyosema mleta mada, huu mradi wa kilimo nadharia, kamwe hautafanikiwa.

Kwenye hili Bashe na Rais Samia wamefeli kabisa. Hawakijui kilimo. Kilimo ni sayansi ambayo huwezi kuijua kwa kumpeleka mtu darasani kwa wiki moja. Ni sayansi ambayo elimu kubwa unaipata kwa kutenda, tena kwa miaka siyo miezi, siyo kwa kukaa darasani, ndiyo maana hakuna msomi wa kilimo nadharia aliyewahi kuwa na mafanikio kwenye kilimo cha vitendo.
 
Alichofanya Bashe sio kwamba hajui Kuna Wanakulima tayari ila strategy ni kuwatoa wasomi kwenye kufikiria A/C za maofisini waende kulima. So anatarajia mafanikio ya hao wachache walioanza iwe motisha kwa wale wengine Ili mwisho wa siku vijana wasomi waone kilimo ni ujanja.

Ila uki support "wazee" wenye uzoefu wa kilimo wa huko "Rukwa" vijana watadai wanapenda kilimo ila hakuna mazingira wezeshi. So Wacha awape support Ili washindwe wenyewe lawama ziishe.

Sasa asipowasaidia wasomi wajiajiri KELELE akiwasaidia KELELE. WaTanzania mnataka Nini? Kama hamtaki "wenye makaratasi" wapewe support basi msiilaumu serikali mnapoona wasomi hawana ajira ila mpiganie ajira za wasio na makaratasi peke Yao!!
 
Tafiti zote Duniani zinaonesha kuwa ukitaka mradi fulani ufanikiwe ni lazima uanzie kwa wahusika na siyo uwapelekee. Mradi wa kuwapelekea watu unakuwa hauna ownership ya wahusika.
Umeongea ukweli, ila je Ile training waliyopewa haitoshi? It's fine, Sasa basi unamshauri vipi Kijana aliyemaliza chuo anatamani kufanya kilimo alafu hajui pa kuanzia hasa mtaji?
 
Bila hizi project tutapataje hela.

Kuandaa hekta moja ni zaid ya mil 16, hapo hujapanda, hujapalilia, huja prune, hujapiga dawa na wala hujavuna na bado hujapeleka sokoni.... sasa piga mara 800😂
Hayo mazao sijui yatauzwa wapi ili ya break even.
Duh 🙄 !!
 
Maajabu ya TANZANIA eti mkulima anaenda kupewa mafunzo ya kilimo.

Ngastukaa machale kundesah!
 
Maajabu ya TANZANIA eti mkulima anaenda kupewa mafunzo ya kilimo.

Ngastukaa machale kundesah!
Mbona wakulima tupo wengi tu na mashamba tunayo ila nguvu ya kufanya kilimo cha kisasa ndio hatuna ! Kwa nini wasingeanza na sisi kutupa misaada tunayoihitaji sana. !!
 
mzeewaSHY Nashangaa wenye spirit ya kilimo hatuitwi Ila watu ambao hawajui na hawataki ndio wanalazumishwa wawe wakulima.

Nilikuwa na mradi wangu wa kilimo na ufugaji niliuandika mwenyewe nikaupeleka wizarani nipate sapot hata connection tuu aisee sikuamini nilichokutana nacho yaan pale vetenary mie ndio nilionekana labda ndio profesa wa kilimo na ufugaji kwajinsi mawe niliyokuwa nayo niliishia kupewa hongera tuu huku wao wakiwa hawajui kitu
 
Ninae huyu mtu anaeitwa Hussein Bashe, Kwa mlio karibu nae jaribuni kumuonya kwamba hicho kilimo anachojaribu kukianzisha, kimeshashindwa hata kabla hakijaanza .labda kwa sababu yeye ni mtu anaedhani kilimo kinaendeshwa kwa makaratasi, hivyo anajaribu kutoa mishipa ya shingo kwa kuongea sanaaa. Akijua ndio kilimo chenyewe.

Kwanza waliopewa nafasi hizo sio wakulima Kwa asili, ni vijana tu ambao wamesikia hekari zinagawiwa wamezikimbilia, ila vijana wenyewe wanaoishi kwa kilimo na wanailisha nchi tangia tupate uhuru hawajaguswa hata Mmoja. Kilimo hakiitaji makaratasi Bali asili ya mtu, kilimo ni asili usipokuwa nayo hata ukipewa zana zote hautaweza.

Na Rais amehadaika na hayo makaratasi ya Bashe anamwaga mamilioni ya pesa ambayo hata hivyo hayatakuwa na tija yoyote, nasema hayatakuwa na tija kwa sababu waliopelekwa sio wakulima ,wakulima hawajafikiwa na kilichofanyika ni kumlazimisha kuku wa kisasa akajitafutie chakura, nasema Tena mpango huu ungepelekwa kwa wakulima wanaozalisha mahindi Huko rukwa na ruvuma, kwa miaka yote wao wapo shambani hawategemei makaratasi, wao kilimo ndio maisha Yao.

Bashe anajaribu kutuingiza mjini kwa mradi huu ambao kufika 2025 hautakuwepo na hayo mashamba yatabaki mapori ya wanyama na hayawani. Kama mnataka Mali mtaipata shambani. Nendeni kwa wenye asili na kilimo mkawape sapoti ya kutosha mtaona matokeo lakini hii propaganda mnayojaribu kuileta hamtaweza mtakwama, narudia katika hili Nina uhakika mabilioni ya pesa yanaenda kupotea.
Siku zote uwoga wa kuthubutu ndiyo adui mkubwa wa mafanikio. Bashe ukiona unapondwa na watu wenye akili ndogo tambua kuwa unachofanya ni sahihi.

Pandisha tinted wala usiwasikie
 
mzeewaSHY Nashangaa wenye spirit ya kilimo hatuitwi Ila watu ambao hawajui na hawataki ndio wanalazumishwa wawe wakulima.

Nilikuwa na mradi wangu wa kilimo na ufugaji niliuandika mwenyewe nikaupeleka wizarani nipate sapot hata connection tuu aisee sikuamini nilichokutana nacho yaan pale vetenary mie ndio nilionekana labda ndio profesa wa kilimo na ufugaji kwajinsi mawe niliyokuwa nayo niliishia kupewa hongera tuu huku wao wakiwa hawajui kitu
Ahahaha! Tanganyika taifa la ajabu sana!

Wanaoitwa wataalamu wengi ni vilaza wasio na msaada wa kutatua changamoto katika jamii.
 
Shida yetu Tanzania ni rushwa na kupendeleana pasipo kutanguliza maslahi ya taifa mbele.

Hao vijana waliopewa hiyo fursa wengi walifanyiwa connection na watu wao. Ni mambo ya ajabu sana.

Mfano kuna hii inayoitwa "mikopo ya vijana" hivi kuna mnufaika yeyote humu jamiiforums ambaye alipata access ya hii mikopo?

Lakini wakiwa bungeni utasikia yanatajwa mabilioni ya pesa kuwanufaisha vijana kupitia mikopo nafuu.

Mleta mada nakuunga mkono kwa hoja zako.
 
Back
Top Bottom