Huu mkataba wa TFF na GSM kwanini usihojiwe kama sio Rushwa?

vvvv

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
406
Reaction score
717
Kwanini mkataba kama huu usihojiwe? Mdhamini mkuu wa ligi (NBC Bank) mkataba wake unahojiwa,huu wa GSM na TFF kwanini usihojiwe?

Ndiyo maana marefa mpira ukigonga mwamba ukarudi uwanjani filimbi inapulizwa mpira upelekwe kati.

 
Mikia huu mwaka mtasema yote.

Uzuri mpira unachezwa uwanjani kila mtu anaona.
 
Pigo kama hizi tulikua tunazileta sisi Yanga kipindi kile tuko vibaya. Muulizie Karia akuambie tulivyokuwa tunampelekea moto.

Anyway, Kuimba Kupokezana.
 
TFF ni shirikisho la mpira wa miguu linaloendeshwa kihuni sana, wale jamaa pale Karume wanajiona miungu watu.

Huo mkataba wa TFF na GSM lazima una contents za hovyo ndio maana unafichwa, ni ujinga wa hali ya juu sana kutishia watu kuwashtaki endapo wataujadili, hili sio taifa la mazezeta kama wanavyodhani wale wahuni.

Katiba yetu inatoa uhuru wa kutoa maoni bila kutuwekea mipaka, wao TFF na GSM wanakuja na kamkataba chao cha kihuni kutuzuia tusiujadili, ni wapuuzi sana wale jamaa, corrupt leaders, na ndio wanajidai wamefunga... nonsense.

Nitashangaa sana kama timu za mpira wa miguu ligi kuu vitanyamaza kimya kama walivyotishwa na hao wahuni, wao ni shareholders wana haki ya kujua chochote kinachohusu mpira wao, sheria zote za nchi hii ziko upande wao, wasiwe wajinga wakanyamaza kimya.
 
Ila Makolo ,ina maana hata kusoma hamjui nyie watu
Huu mkataba ulisainiwa mwaka 2021 halafu mnakuja kuhoji Leo ?
Na pia ,mbona huu mkataba ulisitishwa baada ya kelele ndio maana huoni Bango la GSM kwenye mechi za ligi kuu isipokua Kwa zile team zenye kudhaminiwa na GSM
Mnaacha kutengeneza team mnaleta viroja, kipindi kile mnasajili kina Ngoma mlijiona mmewin ,sasa HV mnalilia mikataba
 
Huu mkataba ni wa mwaka 2021 na ulikufa kibudu, simba waliugomea.
 
Jamaa ana stress aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…