Huu mtindo wa CCM wa kuwapa madaraka ya juu wazee wastaafu waliochoka ndio utamaduni wao!

Huu mtindo wa CCM wa kuwapa madaraka ya juu wazee wastaafu waliochoka ndio utamaduni wao!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Kuna vitu vinashangaza mnoo katika siasa za CCM ambapo kile kinachoimbwa majukwaani (kuwawezesha vijana na wanawake) ni tofauti kabisa na kile kinachofanyika. Hili la wazee wastaafu waliochoka na kuchokwa kurejeshwa kinguvu kwenye ulingo wa kisiasa ni miongoni mwa maajabu ya siasa za CCM.

Hizi harakati hazikuanza leo wala jana, tangu John Malecela akiwa mzee mstaafu (amekalichwa benchi) na kuanza kulala usingizi, ghafla miaka ya mwanzoni 2000 Mkapa akamkurupusha toka usingizini na akampa umakamu mwenyekiti wa CCM, alichokifanya Melecella ni kutengeneza mtandao wake wa kisiasa na 2005 akakamata fomu yake ya kutaka kugombea urais bahati mbaya 'wahuni' wakamkata juu kwa juu kwa fitna!

Magufuli naye akamteua mzee mstaafu aliyechoka, mzee Mangula akiwa amestaafu, yuko zake shambani akilima Nyanya zake, maisha yamemchapa kweli kweli akaokota dodo, akateuliwa kuwa makamu mwenyekiti, katikati ya harakati akalichwa sumu akiwa Lumumba, mzee wa watu chupu chupu akaponea Muhimbili.

Samia akarudia hayo hayo kwa kumteua mzee mstaafu aliyechoka, mzee Kinana kuwa makamu mwenyeki, Kinana naye 'akachonga ule mtego' aliposhtukiwa akakatwa juu kwa juu na ili kuficha yaliyo nyuma ya pazia akaigiza kutema bungo , na leo Samia amerejea tena kumteua Wassira, baada ya muda yatakuwa yale yale tu. Mzee Wasira tunajua, na hajawahi kubadilika.
 
Hii picha ilipigwa takribani miaka mingi iliyo pita more than 5 years
 

Attachments

  • img_1_1737214785337.jpg
    img_1_1737214785337.jpg
    32.7 KB · Views: 2
Mfano hawa vijana wa CDM kazi ni kuvuana nguo kwa kuitisha press conference hawaijui hata maslahi ya chama zaidi ya ambitions zao.
Hawa ndiyo wapewe nafasi...
 
Kuna vitu vinashangaza mnoo katika siasa za CCM ambapo kile kinachoimbwa majukwaani (kuwawezesha vijana na wanawake) ni tofauti kabisa na kile kinachofanyika. Hili la wazee wastaafu waliochoka na kuchokwa kurejeshwa kinguvu kwenye ulingo wa kisiasa ni miongoni mwa maajabu ya siasa za CCM.

Hizi harakati hazikuanza leo wala jana, tangu John Malecela akiwa mzee mstaafu (amekalichwa benchi) na kuanza kulala usingizi, ghafla miaka ya mwanzoni 2000 Mkapa akamkurupusha toka usingizini na akampa umakamu mwenyekiti wa CCM, alichokifanya Melecella ni kutengeneza mtandao wake wa kisiasa na 2005 akakamata fomu yake ya kutaka kugombea urais bahati mbaya 'wahuni' wakamkata juu kwa juu kwa fitna!

Magufuli naye akamteua mzee mstaafu aliyechoka, mzee Mangula akiwa amestaafu, yuko zake shambani akilima Nyanya zake, maisha yamemchapa kweli kweli akaokota dodo, akateuliwa kuwa makamu mwenyekiti, katikati ya harakati akalichwa sumu akiwa Lumumba, mzee wa watu chupu chupu akaponea Muhimbili.

Samia akarudia hayo hayo kwa kumteua mzee mstaafu aliyechoka, mzee Kinana kuwa makamu mwenyeki, Kinana naye 'akachonga ule mtego' aliposhtukiwa akakatwa juu kwa juu na ili kuficha yaliyo nyuma ya pazia akaigiza kutema bungo , na leo Samia amerejea tena kumteua Wassira, baada ya muda yatakuwa yale yale tu. Mzee Wasira tunajua, na hajawahi kubadilika.
ANYWAY, IN ACADEMIC EXCELLENCY UPSTAIRS, THE SAME TREND IS OBSERVED!
Look here
The average age of Nobel Prize winners varies by category and year, but is generally around 60–65 years old
 
ANYWAY, IN ACADEMIC EXCELLENCY UPSTAIRS, THE SAME TREND IS OBSERVED!
Look here
The average age of Nobel Prize winners varies by category and year, but is generally around 60–65 years old
Nobel price winners wanapatikana kwa njia ya tofauti, wanapitia stages 7 mapaka kupatikana mshindi. Political apointees hawana hata hadhi ya kufuta vumbi viatu vya hawa mabwana

Nobel price hupewi as fadhila, as asante, unapewa because you deserve
 
Back
Top Bottom