Pre GE2025 Huu ndio wito wa mwanasiasa au mwana harakati yeyote

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

DaudiAiko

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2012
Posts
372
Reaction score
310
Wanabodi,

Tukubaliane kwamba CHADEMA kuingia madarakani ni kama ngamia kupita kwenye tundu la sindano. Ni Jambo ambalo litahitaji maandalizi ya muda mrefu na tofauti na wengi wanavyo fikiria kutokuwa na tume huru au katiba mpya sio sababu inayowakinga.

Tofauti na kipindi cha awali, serikali ya awamu ya tano na sita imefanya mageuzi makubwa kwenye kufanya kampeni kali ambayo imesababisha Rais Samia na Magufuli kipindi alipokuwa hai kuwa maarufu sana. Mafanikio ndiyo yapo, ila yamekuzwa na vyombo vya habari na mitandao ya jamii kuwapa wananchi hamasa kubwa. Imefika hatua ambayo serikali imelipia matangazo ya Instagram na ya barabarani ili kutangaza mafanikio ya Rais Samia. Lakini mafanikio yapo kweli, pia ni kweli kwamba wananchi wanaikubali sana serikali ya Rais Samia Kwa kiasi kikubwa kuliko sera na harakati za wana CHADEMA…

Nini sasa kiwe kipaumbele Kwa walio CHADEMA?. Inabidi tuangalie motisha ya yeyote kuingia kwenye siasa au kuwa mwanaharakati. Wana CHADEMA wanaendelea kupitia ugumu katika harakati zao za kupigania haki nchini. Hawatakiwi kukatishwa tamaa kwa kutokushinda uchaguzi kwasababu harakati za kweli zinatoka moyoni. Wanatakiwa kuamini kwamba siku moja kazi yao itazaa matunda katika mchakato wa kuwa na Tanzania mpya. Wanatakiwa wachukulie yanayo wakuta positively wakilenga kuhakikisha kwamba haya mtokei mwingine hata katika vizazi vijavyo. Huu ndio wito, hiyo ndiyo kazi nzito…

Mabadiliko huchukua muda, kukaa meza moja inahitaji juhudi kali, ila kwa kuzingatia niliyo yaeleza, utagundua kwamba hiyo ndiyo attitude inayofaa. Huo ndio uzalendo wa kweli…..

 
Uchaguzi utakuwa huru?

Wagombewa wa CHADEMA hawataenguliwa?

Mawakala wa CHADEMA hawatasumbuliwa kupata viapo na kuingia katika vyumba vya kura?

Kura zote zitatangaziwa kituoni zilipopigiwa kabla box hazijakusanywa jimboni?
 
Uchaguzi utakuwa huru?

Wagombewa wa CHADEMA hawataenguliwa?

Mawakala wa CHADEMA hawatasumbuliwa kupata viapo na kuingia katika vyumba vya kura?

Kura zote zitatangaziwa kituoni zilipopigiwa kabla box hazijakusanywa jimboni?
Jibu la hilo Swahili linategemea kama mabadiliko yaliyofanywa kwenye tume huru kikatiba yatahakikisha kwamba tume inaweza kuendesha shughuli zake bila kushurutishwa. Ingependeza kama kikosi kazi kinacho jumuisha wawakilishi kutoka Chama tawala na vyama vya wapinzani kingeundwa ili kuandaa kanuni za kuendesha uchaguzi. Kubadilisha muundo wa tume ni ngumu ila kubadilisha standard operating procedure ni kitu ambacho kinawezekana. Mabadiliko haya yanaweza kuwa yanafanywa kila awamu ili kuendana na uhalisia. Ila hata hayo yakifanyika bado itakuwa ngumu Kwa Chama chochote cha upinzani kushinda Kwa sababu za uenezi. Cha muhimu wasikate tamaa katika harakati zao za kupigania haki
 
Wewe juha wa CCM kama walivyo CCM wote, mnajitahidi kujificha kwenye lundo ka oksijeni mkitoa hoja dhaifu na kuficha sababu ya dhahiri kuwa ni CCM haina dhamira ya dhati ya uchaguzi huru na haki.

Mnaleta ngonjera hakikisheni uchaguzi huru na haki kisha mje na hivyo vituko vyenu. Otherwise mnataka teuzi ndio maana mnaleta uchawa halafu mnaandika majina yenu mtafutwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…