Huu ndo ukweli toka moyoni mwangu!!!!

Nachotaka kusema likija swala la utoaji mimba watu wanawaona wanawake ndiyo chanzo cha tatizo; but am telling you it is because of men. Hawa wadada wanaotoa mimba hicho kitendo kinawaumiza sana and they live with that pain maisha yao yote.

Kwa vile mimba haitungwi na mtu mmoja, I place the blame squarely on both or all who take part in destroying it. Kama mdada akiamua mwenyewe kwenda kutoa kwa sababu zake mwenyewe basi na lawama abebe yeye. Kama anashawishiwa na huyo mwenzake na yeye anakubali halafu huyo mwenzake analipia, mbele yangu wote wanabeba lawama. Kama familia inatoa shinikizo na mdada anakubali kwangu wote wanabeba lawama. Katika hili pia siwa excuse waganga wanaozitoa. Matter of fact, ni wauaji tu na wenyewe.


Nakubali kuna wasichana mcharuko kutoa mimba ni kama kunywa maji. Ila kuna wengine nina imani hata wakisoma hii thread wanaangua kilio; they have killed their babies si kuwa wanapenda bali they were forced to.

This is a very, very weak and lousy argument! Mdada anayeenda mwenyewe kutolewa mimba yake huyo ni kaamua kufanya hivyo. Unless uniambie alifungwa kamba na akaburutwa kupelekwa huko wanakozitolea hizo mimba.

Mama mwenye mimba, ukiachilia mbali ajali zinazoweza kusababisha miscarriage, ndiye mwenye uamuzi wa mwisho kabisa wa kukibakiza na kukitunza hicho kiumbe tumboni mwake.

Kuna wasichana mimi nawajua ambao walikataa katu katu mashinikizo ya familia zao ya kutoa mimba na wakazibeba hadi wakazaa. Na walipozaa wazazi wa hao wadada mbona walisutwa na dhamiri zao!! Kila walipokuwa wanawaona wajukuu zao wakicheka na kutabasamu na jinsi walivyokuwa wazuri, najua kabisa dhamiri zao ziliwasumbua. Kwamba walikuwa wanataka hao viumbe waangamizwe kabisa na katu wasije na wao kuonja raha na karaha za dunia hii.

Sasa leo unakuja unakaona kajukuu kako, mashavu hayo yametuna, halafu na kenyewe kanatabasmu kila kamwonapo mtu yeyote yule. Wewe mzazi uliyekuwa unataka kukaangamiza hako katoto, kama una moyo lazima itakusumbua. Lakini kama una jiwe wala haitakusumbua.
 
<br />
<br />
huyo dada aliemtema jamaa kwa kumlazimisha kutoa mimba binafsi naungana nae,

Sikia,

miaka ya nyuma sana kipindi sisi tunamaliza form four nilikuwa na rafiki yangu wa kike ambae alikuwa na boylover wake, nakumbuka she was my best friend kwani nilibahatika kumfahamu kuanzia primary nilikosoma nae na kufanikiwa kuchaguliwa nae the same sec school,

alichoniboa, tulivyomaliza form 4 yeye matokeo yalionyesha kuwa amefanya vibaya lakini pia alishakuwa na ujauzito wa mie 5, nilimshangaa sana baada ya kusikia kuwa kaitoa mimba ambayo ilikuwa inajulikana mtaa mzima kwa ushirikiano na mama yake ambae ni nurse kisa wamempatia chuo cha kufoji cha nursing!!


She was my best friend since darasa la kwanza lakini kuanzia siku ile alinitoka rohoni hata yeye alijua, na nilimwoma mama yake muuaji, I ndan hata kama ningeugua hosptln ningeweka barrier kuwa asiniguse ingawa mwanzoni nilimuheshimu kama mama yangu.

Totaly Anetoa mimba sio rafiki yangu hata tone.
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
iwapo ikibaki itahatarisha uhai wa mama au mtoto au wote.
<br />
<br />
Bado hujajibu swali, ni mimba chache mno zinazotolewa kwa sababu ya msingi inayoeleweka kama hiyo, huenda ikawa 1/100 vinginevyo wengi wanatoa kwa sababu zisizo za msingi.
 
<br />
<br />
iwapo ikibaki itahatarisha uhai wa mama au mtoto au wote.

Jamani hili suala siyo rahisi kama watu wanavyolifikiria. Hakuna mtu (mke au mume) anayekaa akatoka tu na amani moyoni kwenda kutoa mimba. Nimeshasema kuwa kuna mwingiliano wa sababu ambazo zinawafikisha watu katika point hiyo. Siungi mkono utoaji mimba ila pia sitaki kuona watu wanamwaga lawama za jumla jumla.

Na kama ni kuua, kwani wanaotoa mimba ndiyo wauaji peke yao katika hii dunia?? Au tunawalaani kwa sababu hawawezi kutoka publicly kujitetea?
 
<br />
<br />
Bado hujajibu swali, ni mimba chache mno zinazotolewa kwa sababu ya msingi inayoeleweka kama hiyo, huenda ikawa 1/100 vinginevyo wengi wanatoa kwa sababu zisizo za msingi.

Mkuu,

Ila unaamini kwamba watu wengi wanatoa mimba (tena katika mazingira yasiyo salama)???? Na kama wanatoa unadhani wewe ni kwa nini wanafanya hivyo? Au tuseme tu kuwa ni vichaa na malimbukeni??
 
<br />
<br />
mkuu

hapo juu umesema kama ni kuua kwani ni wao peke yao!! Kweli sio peke yao lakini wauaji wengine huenda wanafanya hivyo either kwa mazingira yanayohusiana na

1. Bahati mbaya

2. Uadui

sasa,

mwanamke anapochukua hatua kwenda hosptl au kutumia madawa ya kutoa mimba tumweleweje!

1. Ni bahati mbaya?

2. Ana uadui na hicho kiumbe kilichoko tumboni?
 
mmh ivi madocta mnawaweka wapi katika swala hili?
Mana wao ndo wanaotoa inamana wakigoma kama Masheli ya Tanzania nadhani tatizo litaisha.

Watoaji ni madokta wakikataa kutoa itasaidia.

Note:mimba nyingi zinatolewa na madokta kuliko njia ya vidonge.
 
Kumbuka swala hili limekaa ki-imani zaidi..ndo maana kuna nchi zingine zina ruhusu utoaji mimba..! kumbuka kuna wanaozaa na kwenda kutupa,kuna wanaozaa mlemavu wa aina fulani ambae hatakiwi katika jamii husika pia hutupwa ama kuuawa! Lakini yote tisa pia hata ukifanya mapenzi na kuzitupa mbegu zako pia ni dhambi coz ndani yake kuna viumbe..!
 
kuhusu suala la imani naweza kuungana na wewe kwa asilimia kidogo, nasema hivyo kwa sababu mambo kama hayo yalitokea zamani mno,,,,, siku hizi watu ni mwendo wa kuchukia watoto, wanabeba mimba wanazitupa, wanazaa watoto wanawa tupa chooni, wanafungwa lakini hawasikii!!!!!!!!!!


sasa jiulize, kuna shetani gani amekata akili za watu?
 
mmh ivi madocta mnawaweka wapi katika swala hili?
Mana wao ndo wanaotoa inamana wakigoma kama Masheli ya Tanzania nadhani tatizo litaisha.

Watoaji ni madokta wakikataa kutoa itasaidia.

Note:mimba nyingi zinatolewa na madokta kuliko njia ya vidonge.
hapo nakuunga mkono, kama unaweza kuwabana vizuri nahisi tatizo lingepungua sana,,

lakini kwa nini hawa madktari wasiheshimu miiko ya kazi zao?

kw nini wasiogope uovu? kwa nini mtu uwe na profession ambayo mwisho wa siku inakupeleka jehanum?

mtu alisomea kazi yake ili awe msaada kwa jamii lakini kama ndo professions zina tumiwa hivyo tutafika????????????????
 
mmh ivi madocta mnawaweka wapi katika swala hili?
Mana wao ndo wanaotoa inamana wakigoma kama Masheli ya Tanzania nadhani tatizo litaisha.

Watoaji ni madokta wakikataa kutoa itasaidia.

Note:mimba nyingi zinatolewa na madokta kuliko njia ya vidonge.

They are murderers too.
 
<br />
<br />
Ugumu wa maisha ndo sababu yao kubwa inayowapelekea kufanya mambo kama hayo.

Mimi nadhani kila mtu aki play part yake kwa ukamilifu haya matatizo yataisha.

Walopeana mimba-Walee mimba yao na hatimaye mtoto.

Madocta-watoe huduma ya uganga na kuheshimu miiko yao ya kazi{Ethics}.
 

Kwa sababu yoyote ila. Tunapaswa kuamini kuwa lazima kuna sababu ambayo huyo mtu anaiona niya msingi (hata kama sisi tunaona ni upuuzi) inayomfikisha katika kuchukua hatua hiyo. Kama watu makini, jukumu letu ni kuzitafuta sababu za namna hiyo ili tujue pa kuanzia. Kuendekeza tabia ya kulaumu na kulaani hakutasaidia lolote zaidi ya kulifanya hili tatizo liwe gumu zaidi!
 

Sina hakika kama una data ya hicho unachokiongea. Nitakutafutia paper moja iliyoripoti utafiti uliofanyika Temeke na Kagera na kuonesha kuwa unsafe abortions ni nyingi zaidi kuliko zile zinazofanywa na Madaktari!

Nadhani bado hatujajikita kwenye kiini cha tatizo.

Data ni hizi hapa:
 
They are murderers too.

Sawa mkuu,

Hivi sisi tulio pembeni tunachukua hata dakika moja kujiuliza kwa nini? Haiwezekana hawa watu wakawa wauaji na wakatili bila sababu!

Hata magaidi wanazo sababu kwa nini wanajilipua!
 
kwa nini waota mimba wasiukumiwe kifo jamani
 
Sawa mkuu,

Hivi sisi tulio pembeni tunachukua hata dakika moja kujiuliza kwa nini? Haiwezekana hawa watu wakawa wauaji na wakatili bila sababu!

Hata magaidi wanazo sababu kwa nini wanajilipua!

Ni wazi sababu zipo na chache kati ya nyingi ni ubinafsi, ukatili wa asili, kutokujali, na tamaa. Lakini kwa vile sababu zipo hiyo haina maana ya kwamba ni sawa. Kukiondoa kiumbe ambacho wala hata hakiwezi kujitetea ni ukatili wa kupindukia.

Nitajisemea nafsi yangu mwenyewe. Sijawahi na sitakuja kushiriki, iwe moja kwa moja au la, kwa hiari yangu, kuondoa uhai wa binadamu ambaye hajazaliwa. Huo ndiyo msimamo wangu na ninajivunia kuwa hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…