Huu ni ugonjwa gani? msaada tafadhali

upo mwanza sehemu gani nikupe maelekezo nilikukuwa na mtoto mwenye hiyo shida kapona tiba iringa
Mwanza nipo maeneo ya kirumba jirani na monarch hotel mkuu, nisaidie!!!
 
Mkuu hebu tuambie dalili za mwanzo za mgonjwa zilikuaje?
 
Hayo mapepo mpeleken kweny maombi
Mkuu Neema tulisha peleka kila aina ya maombi lakini mafanikio hamna!!

wewe kumbuka tokea 2007 akiwa kidato cha pili mpaka leo hii hakuna dalili yoyote ya kupona!
 
Mkuu Neema tulisha peleka kila aina ya maombi lakini mafanikio hamna!!

wewe kumbuka tokea 2007 akiwa kidato cha pili mpaka leo hii hakuna dalili yoyote ya kupona!
Duh ipo kaz hapo maana kama angekuwa na ugonjwa ungeonekana hospital ebu jarbun kumpeleka kwa mwakasege maana mapepo au mtu aliyelogwa huwa akipelekwa hospital vpmo huwa havionesh chochote
 
Anapokuwa anajitambua aombe sana kutafuta mahusiano mema binafsi na Mungu atubu na kuacha aina zote za dhambi na Yesu atampatia uponyaji kusoma biblia na kufunga iwe tabia yake Mungu
Hivi unafkiri kuna binadamu anaweza {(kuacha)} madhambi ya aina zote? c atakua mtakatifu ss huyo, sawa na Malaika tu au Mungu mwenyewe...!!! Ungemshauri ajitahidi kumwomba Mungu ajikatalie kadri atakavyoweza, lkn naamini kuacha dhambi hicho kitu hakipo,,, Msi2danganye nyie walokole kwamba kuna kuacha dhambi,, tunajikatalia tyu kwa kias tuwezavyo bhn,, but in 100% ni ndoto..!!!
 
Huyo si mgonjwa wa ugonjwa wowote ule ila mtoa mada hajatoa details za kutosha za huyo Dada anayeanguka.

Ila kwa uzoefu kuna watu au mtu anampitia huyo na kuondoka naye kwenda naye ktk kazi za kuzimu na huyo Dada anatumika tu.

Wakimaliza kumtumia wanamrudisha na ndipo fahamu zake zinarudi ila wanakuwa hajapoteza fahamu kabisa na mtoa mada anajua kuwa huyo Dada huwa kope zake za macho zinacheza cheza muda wote anapokuwa ameanguka.

Sasa kwa wataalam wa DINI na Imani watafunga huo mlango unaotumika kumuingia na Kuchukua.
 

Basi kwa maana hiyo hakuna binadamu yeyote atakae enda mbinguni maana biblia inasema hakuna chenye udhaifu wowote kitakachoingia mbinguni

Ipo hivi 1Petro 1;15 inatuasa kuishi maisha matakatifu kama Mungu alivyo mtakatifu na kwa mantiki hiyo binadamu tunaweza kuwa watakatifu kama tutajisalimisha kikamilifu kwa Mungu na watakatifu ni watu walio hai wala sio marehemu (When we are alive we can be saints but not HOLY)


Ukweli ni huu hakuna binadamu anaeweza kuacha dhambi na na hii inakuwa ni sababu ya wengi kukata tamaa ya kuishi bila dhambi kwa mfano mtu unapo dhamiria kuwa mwema na kuamua kuacha dhambi utakuta zile/ile dhambi unayodhamiria kuiacha na kujitaabisha kujitenga nayo utajikuta ndo unaitenda kuliko hata ya awali kama ni uzinzi utajikuta unazini na kushindwa kujizuia na hapo utakuta mtu uliamua kufunga na kuomba kuishinda hiyo dhambi lakn umeirudia. Unajua kwann???

Binadamu wote hatuna nguvu za kupambana na shetani ama uwezo wa kuyashinda matakwa yetu ya mwili hivyo tunachokosea ni kujaribu kutaka kujiokoa wenyewe toka kwenye hatari hizo na kwa asili hatuna nguvu za kumshinda shetani ila tunazipata kwa Mungu

Hivyo ili mtu uweze kuishinda dhambi inapaswa uache kupambana na dhambi ila upambane kumuomba Mungu awe sehemu ya maisha yako inapaswa kwa kufunga na kuomba utafute kuwa na mahusiano binafsi na Mungu kisha Mungu ndie atakuongoza kuzishinda dhambi, kama tukiwa na mahusiano mema ya karibu na Mungu hakuna litakalokuwa gumu kwako kwani Mungu akiishi ndani yako utayaweza yote maana ndie atakae kuwa nguvu yako hat huko makanisani Wakristo tunakosea kuomba magari, uponyaji na miujiza mingine badala ya kumuomba Mungu mwenyewe aje kwetu tunakosea hapa watu tunaomba matunda ya Roho (amani, upendo n.k) badala ya kumuomba Roho na ndio maana shetani ametumia fursa hiyo kutoa hayo matunda ili watu tupotee maana watu tunaenda kuomba tukiyatazama matatizo yetu badala ya kumtazama Munga ( We have to pray for the presence of God in our lives and not to pray for the answers)
 
Mkuu Neema tulisha peleka kila aina ya maombi lakini mafanikio hamna!!

wewe kumbuka tokea 2007 akiwa kidato cha pili mpaka leo hii hakuna dalili yoyote ya kupona!
Vip mkuu alishapona? Tupe mrejesho Tafadhali
 
Vip mkuu alishapona? Tupe mrejesho Tafadhali
Natamani ingekuwa hivo mkuu!

Ningeanzisha uzi mrefu sana wa kushukuru na wengine labda wangepata kupona!

Lakini mpaka leo ni ile ile!
 


Picha ya ugonjwa tafadhali.
 
Nendeni kwa padre wao wanaomba kwa utaratibu hawamforce watambembeleza taratibu ataongea, ila awe padre mwenye nguvu, kuna dada aliniambia mdogo wake yalimtokea walihangaika sana ila kwa padre alipona musoma huko, yalikuwa ni mapepo aliwekewa na mama ake mkubwa, yalipokuwa yanatoka yalisema kwako padre tunatoka umeongea na sisi kwa ustaarabu bila makelele kwa wengine walikuwa wanatupigia kelele sana tunatoka tunakaa hapo nje akitoka tu nje tunaingia tena hayo yakaondoka, ndo akajitambua muda wote walikuwa wanaishi naye kumbe alikuwa siyo yeye
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…