Huu ni ujumbe kwa Wasanii wote wa mziki, Diamond hafai kuweni naye makini

Hayo ndo maono Mungu aliyonirudhuku kuyafikilia kulingana na uwezo wangu nawe una ruksa ya kutupanua mawazo tujue tusivyo jaaliwa kuvifikiri.
Mungu huwa hawajalii watu wake kuongea chuki,ila anawajaria busara na hekima. Wewe unadhani leo hii ukiwauliza timu yake nzima ya WCB,ndugu jamaa na marafiki zake wa karibu na watu wote ambao DIAMOND kawasaidia watakuona wewe ni mtu wa namna gani,kwa kumzungumzia mtu aliyewasaidia vile ....???
 
UMELIPWA SHILINGI NGAPI??

NYINYI NDIO WACHAWI

ACHA HIZO MWANANGU HII DILI MLIYOPEWA NI HARAMU.
 
Hapo ndo shida yetu watanzania. Mtu ukimuajiri umemsaidia au mnasaidiana maana hawalipi bure wanafanya kazi na wanalipwa stahik zao. Mfano kina rayvan kawasaidia au wanasaidiana?
 
Tip top, AY, YAMOTO, Diamond &WCB wapo chini ya the same managers. Hivi hujawahi jiuliza kwann diamond na wasafi yake yuko mbali compared na hao wengine ilihali wote wapo chini ya the same managers???
 
Kuna kitu kinaitwa Muziki by darassa ft Ben Pol, yaaani kwa jins ngoma ilivyo kali na haihit kiviiileee ndo huwa naamini huenda figisu + ushirikina ndo vinaitawala industry nowadays
Mkuu unakosea sana kusema ngoma ya darasa haihit wakati ndo inaongoz kwa ngoma zilizotok wiki hii ikifuatiwa na kokoro so tuzipe muda then tutajua kwel kunakuwag na figisu au la
 
Hapo ndo shida yetu watanzania. Mtu ukimuajiri umemsaidia au mnasaidiana maana hawalipi bure wanafanya kazi na wanalipwa stahik zao. Mfano kina rayvan kawasaidia au wanasaidiana?
Hivi wewe ni mfuatiliaji wa haya mambo kweli ...........Rayvanny na Harmonize WAMESAIDIWA,KWASABABU HAWAKUWA WAMETOKA KIMUZIKI KUSEMA KWAMBA WANAWEZA KUINGIZA PESA. KWAHIYO KAWASAIDIA KUTOKA,KISHA SASAHIVI NDIO WANAFANYA KAZI NA KURUDISHA PESA ILIYOWEKEZWA KWAO.Mtu ambaye hakumsaidia ila amemsaini kufanyakazi ni RICH MAVOKO.
 
Aisee
akiri=akili

wamsitili=wamsitiri

Mpaka hapo inadhihirisha ni mtu wa namna gani
 
Diamond sio msanii wa kawaida. Anapaswa kupongezwa kuliko kubezwa!

Amejituma sana, mpaka akavuka viwango vile ambavyo wasanii wenzake wa miaka nenda rudi, hawakuwahi kuifikiria! Tusimuombee mabaya!

Ameipeleka sanaa ya Tanzania haswa muziki wa Bongo fleva kwenye level nyingine.

Yeye ndi ICON ya Bongo fleva kwa sasa! Tuwe wakweli tu, Kijana ana udhaifu wake kama binadamu, lakini amefanya mengi mazuri kuliko madhaifu madogo madogo aliyoyaonyesha!

Mimi sio mpenzi wa muziki wa kizazi kipya, lakini najivunia mengi anayoyafanya DIAMOND.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni!
 
Nadhan mihemko ndo shida maana mapenz ni sawa na upofu. Rayvan kamchukuwa ili amsitili maana kwa sasa hana jipya ndo maana unaona anavyo panic katiaka media. Any way time is a good judge.
 
Wakae nae mbali kivipi
Wakati wanategemea kick kwake
Wanaishi kwa nguvu ya kick kisa kumsema diamond
Jua hawawezi
 
Mkuu unakosea sana kusema ngoma ya darasa haihit wakati ndo inaongoz kwa ngoma zilizotok wiki hii ikifuatiwa na kokoro so tuzipe muda then tutajua kwel kunakuwag na figisu au la
Lete kigezo ulichokitumia ............(Kumbuka hatutaki kuongea hisia,ila kitu ambacho unaushahidi wa unachokisema.)
 
Hapo ndo shida yetu watanzania. Mtu ukimuajiri umemsaidia au mnasaidiana maana hawalipi bure wanafanya kazi na wanalipwa stahik zao. Mfano kina rayvan kawasaidia au wanasaidiana?
wanasaidiana lkn ebu nambie, unahs wangetoka kwa juhudi zao binafs wangekuwa ktk level ya juu kama walivyo saiv... Mfano Harmonize juz kat kapat tuzo mbili za kimataifa. Bila kutokea kwa mgong wa Diamond unahs angekuw hapo alipo kweli
 
Nadhan mihemko ndo shida maana mapenz ni sawa na upofu. Rayvan kamchukuwa ili amsitili maana kwa sasa hana jipya ndo maana unaona anavyo panic katiaka media. Any way time is a good judge.
Umeshamaliza hoja,sasa umeipa nafasi chuki uliyojifanya kuificha ikutawale,wacha nikuache sina muda wakujadili chuki na mtu asiyejua hata historia za watu anaowazungumzia.
 
wanasaidiana lkn ebu nambie, unahs wangetoka kwa juhudi zao binafs wangekuwa ktk level ya juu kama walivyo saiv... Mfano Harmonize juz kat kapat tuzo mbili za kimataifa. Bila kutokea kwa mgong wa Diamond unahs angekuw hapo alipo kweli
Tuzo za diamond and his companies wananunua brother kwa sasa hatuna iman nazo tena. Sory for that boss
 
Mpumzisheni mtoto wa watu. Hakauki vinywani mwenu mnampinga lakin mkumbuke yeye ndo maji usipokunywa, utaoga.

Wenye roho mbaya tunawajua mondi hayupo huko
 
Hao uliowataja mavoko,rayvan na hamonize umewasikia wanafanya shoo? Ni moja au mbi na zikizid ni tatu kw mwaka? Unajua maana yake ni nn?
Ww jamaa kweli muongo kwa mwaka huu tu hawo mdogo wamepiga show zaidya ishirini asa cjui unataka show gan izo.....punguzen mihemuko mda ukifika automatically atashuka
 
Nadhan mihemko ndo shida maana mapenz ni sawa na upofu. Rayvan kamchukuwa ili amsitili maana kwa sasa hana jipya ndo maana unaona anavyo panic katiaka media. Any way time is a good judge.
Kupaniki kule hakutokani na kutokuwa na jipya bali ni vitu vya ajab ajab na matusi wanayomtukana kupit kiasi yanawavuruga sana wasanii sema ataivyo wanajitahd sana kuvumilia. Mfano matusi wanayotukana Diamond na kiba kwakwel mtu yeyote lazm upanick, si unaonag Baraka da prince anavyoreact ovyo ovyo akitukanwa
 
Uandishi wako tu hasa ulivyoanza hapo mwanzo utafikiri hujasoma kiswahili, Hamna cha koma wala nukta, kiukweli mimi sijakuelewa hasa ulivyoanza, kama vipi rudi shule mkuu
Mbona wewe umeeka alama za mkato tu hata nukta hamna.chizi siku zote hujiona mzima ila anaowaangalia anawaona machizi kumbe yeye ndiye chizi halisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…