Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,421
Imebainika kiutafiti kwamba wanawake wanne kati ya kumi huwa wanatoka nje kwenye ndoa zao. Idadi hiyo hata hivyo inaongezeka haraka sana, na inawezekana idadi hiyo ikafikia wanawake watano kati ya kila kumi. Kwa upande wa wanaume inaelezwa kwamba, kati ya kila wanaume kumi, sita au saba wanatoka nje ya ndoa zao…………duh! Nashukuru mie simo.
Kwa ujumla takwimu hizi zikikokotolewa, zinaonesha kwamba, kwenye kila ndoa kumi, ndoa nane zina mwanandoa mmoja kati yao ambaye anatoka nje au aliwahi kutoka nje. Kwa hiyo, hivi sasa ulipo hapo kwenye ndoa yenu, jaribu zoezi hili. Hesabu ndoa kumi za watu unaowajua ambao wameoa au kuolewa. Kati a ndoa hizo ni ndoa mbili tu ambazo zina wanandoa ambao hawatoki nje ya ndoa zao. Je ni wewe au mpenzi wako ambaye ni miongoni mwa hao watu wanne waadilifu? (haki ya Mungu Mtambuzi leo nitasutwa).
Hii ina maana kwamba, watu hutoka nje sana kwenye ndoa zao kuliko inavyodhaniwa. Mnaweza kudhani idadi hiyo ni kubwa sana, lakini tafiti karibu zote zilizofanywa kuhusu suala hili zinaonesha ukweli huo. Kama kwa wanawake kwa mfano, wale walioajiriwa kiwango chao cha kutoka nje ni karibu sawa na kile cha wanaume.
Hii ina maana kwamba, mpenzi wako, mkeo au mumeo yuko kwenye hatari ya kuzini muda wowote kulingana na mazingira yaliyomzunguka.Jambo ambalo wapenzi, wachumba au wanandoa wanapaswa kulifahamu ni kwamba kuna sababu tofauti na nyingi zinazosababisha wenzetu kutoka nje.
1. Kuna kutoka nje kwa sababu watu hawako karibu tena, hakuna ule moto wa awali. Tunasema upendo umeisha au moto umezimika.
2. Kuna wale wanaotoka nje kwa sababu wanataka kuonesha kwamba, wanamudu. Kwa baadhi ya watu kutongoza na kukubaliwa au kutongozwa na kukubali, kunaonesha kwamba, mtu ana thamani, anamudu na anapendwa na wengi.
3. Kuna watu ambao kutongoza na kumpata mwanamke fulani ni suala la kushindana.4. Kuna wanaotoka nje ya ndoa zao kwa sababu wanataka kujihisi kupendwa, wanataka kujiona wakiwa kwenye hali ile ambayo tunaihisi tunapopendwa na wengine kwa mara ya kwanza.
5. Kuna kutoka nje ambako ni kama kulipiza kisasi. Inaweza kuwa mpenzi amemfanyia au ameshindwa kumfanyia mwenzake jambo fulani. Ili kumkomoa mwenzake huyo, hutoka nje.
6. Wanawake hasa wanakabiliwa na kutoka nje kwa lengo la kutaka kujithibitishia kwamba, wako safi bado, yaani, 'wanadai' hata wanaume nao kuna wale wanaotoka nje na kutembea na wasichana wadogo sana. Kuna wakati hufanya hivyo kuthibitisha kwamba hawajachoka na kuzeeka. Wanatamani ujana wao.
Ukweli ni kwamba kuna sababu nyingi na tofauti za kutoka nje, lakini kwa leo naona niishie hapa.
http://wordscapes.net/extramarital-affairs.htm
Kwa ujumla takwimu hizi zikikokotolewa, zinaonesha kwamba, kwenye kila ndoa kumi, ndoa nane zina mwanandoa mmoja kati yao ambaye anatoka nje au aliwahi kutoka nje. Kwa hiyo, hivi sasa ulipo hapo kwenye ndoa yenu, jaribu zoezi hili. Hesabu ndoa kumi za watu unaowajua ambao wameoa au kuolewa. Kati a ndoa hizo ni ndoa mbili tu ambazo zina wanandoa ambao hawatoki nje ya ndoa zao. Je ni wewe au mpenzi wako ambaye ni miongoni mwa hao watu wanne waadilifu? (haki ya Mungu Mtambuzi leo nitasutwa).
Hii ina maana kwamba, watu hutoka nje sana kwenye ndoa zao kuliko inavyodhaniwa. Mnaweza kudhani idadi hiyo ni kubwa sana, lakini tafiti karibu zote zilizofanywa kuhusu suala hili zinaonesha ukweli huo. Kama kwa wanawake kwa mfano, wale walioajiriwa kiwango chao cha kutoka nje ni karibu sawa na kile cha wanaume.
Hii ina maana kwamba, mpenzi wako, mkeo au mumeo yuko kwenye hatari ya kuzini muda wowote kulingana na mazingira yaliyomzunguka.Jambo ambalo wapenzi, wachumba au wanandoa wanapaswa kulifahamu ni kwamba kuna sababu tofauti na nyingi zinazosababisha wenzetu kutoka nje.
1. Kuna kutoka nje kwa sababu watu hawako karibu tena, hakuna ule moto wa awali. Tunasema upendo umeisha au moto umezimika.
2. Kuna wale wanaotoka nje kwa sababu wanataka kuonesha kwamba, wanamudu. Kwa baadhi ya watu kutongoza na kukubaliwa au kutongozwa na kukubali, kunaonesha kwamba, mtu ana thamani, anamudu na anapendwa na wengi.
3. Kuna watu ambao kutongoza na kumpata mwanamke fulani ni suala la kushindana.4. Kuna wanaotoka nje ya ndoa zao kwa sababu wanataka kujihisi kupendwa, wanataka kujiona wakiwa kwenye hali ile ambayo tunaihisi tunapopendwa na wengine kwa mara ya kwanza.
5. Kuna kutoka nje ambako ni kama kulipiza kisasi. Inaweza kuwa mpenzi amemfanyia au ameshindwa kumfanyia mwenzake jambo fulani. Ili kumkomoa mwenzake huyo, hutoka nje.
6. Wanawake hasa wanakabiliwa na kutoka nje kwa lengo la kutaka kujithibitishia kwamba, wako safi bado, yaani, 'wanadai' hata wanaume nao kuna wale wanaotoka nje na kutembea na wasichana wadogo sana. Kuna wakati hufanya hivyo kuthibitisha kwamba hawajachoka na kuzeeka. Wanatamani ujana wao.
Ukweli ni kwamba kuna sababu nyingi na tofauti za kutoka nje, lakini kwa leo naona niishie hapa.
http://wordscapes.net/extramarital-affairs.htm