Huu utapeli ni mpya au upo? Wauza Vyombo vya Mnada wawaliza kina mama Kimara, kuweni makini

Huu utapeli ni mpya au upo? Wauza Vyombo vya Mnada wawaliza kina mama Kimara, kuweni makini

NBica

Member
Joined
Sep 13, 2010
Posts
39
Reaction score
36
WhatsApp Image 2024-11-04 at 13.45.31.jpeg
Aina ya risiti zao

Leo asubuhi kina mama wa Mtaa wa Kilungule B Kata ya Kimara, Wilaya ya Ubungo wameamka na vilio baada ya kutapeliwa na watu waliokuja kufanya mnada wa vyombo mbalimbali kama masufuria na vifaa vingi vikiwa vya kieletroniki kama simu, laptop, sabufa, pasi na vitu vingine.

Ilikuwaje?
Watu hao wakiwa wanaume kama watano walikuja na magari mawili katika eneo hilo. Wakashuka baadhi na kuanza kuuliza kwa Watu vitu mbalimbali. Maswali hayo yalikuwa kama
  • Huku wauzaji wa vyombo vya mnaada wamewahi kuja?
  • Je, Watu wakukopesha vyombo vya Uturuki wamewahi kukopesha mtaani?
  • Wengine wakasema tumekuja kufuatilia madeni kwa waliokopa vyombo na hawajalipa
Baada ya maswali hayo ghafla wakaanza kutangaza kwa kipaza sauti kuwa wanafanya mnada wa kuuza Vyombo vya SACCOSS vya Watu walioshindwa kurudisha marejesho katika SACCOSS lakini cha kushangaza baadhi ya vitu hasa sufuria zilikuwa mpya.

Kama ilivyo ada kina mama ndio wahanga wakubwa.

Wakajitokeza kwa wingi hasaaaa wakiwa na vimkoba vyao vyenye pesa na wao walivyoona watu wengi wakashusha vyombo vilivyo kwenye gari chini wakavipanga na mnada ukaanza.

Waliuza simu kwa bei rahisi sana, Samsung, iPhone, Vivo na zingine sikumbuki brand bei zake zilikuwa 25,000, 50,000, 70,000, hakuna aliyenunua simu zaidi ya laki.

Ikaja TV kwa laki mbili flat screen na Laptop kwa laki mbili.

Lakini cha kushangaza baada ya kufika majumbani simu hakuna iliyowaka, tv na laptop hakuna iliyowaka. Na vifaa hivyo kama simu zilikuwa zimegundishwa na gundi ya superglue vimefungwa fungwa tu maana ilikuwa ni jioni giza linaanza nahisi watu walishindwa kukagua.

Walikuwa na Cable za kufanya test lakini baadaye walisingizia kuwa betri haiwaki ili kuchomeka katika umeme.

WhatsApp Image 2024-11-04 at 13.45.31 (1).jpeg

Hii ni aina ya risiti walizokuwa wanatoa

Waliwapa watu risiti na wakatoa na namba zao wakidai watarudi, lakini namba ikipigwa wanasema kila mtu anajibu lake mara mwenye simu hayupo, simu haipatikani au kuzimwa.
WhatsApp Image 2024-11-04 at 13.45.28.jpeg

Hii ni namba nyuma ya risiti yao

Sasa huu ni utapeli mpya au kuna Watu wanalizwa huko?
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-11-04 at 13.45.28.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-04 at 13.45.28.jpeg
    111.4 KB · Views: 8
Ukipenda vya bei chee matokeo yake ndio hayo ...

Wajinga ndio waliwao..

Polee Kwa wahanga pia
 
😂😂😂😂😂😂 Mkuu pole sana najua wewe ni mmoja wa wahanga msipende vitu vya bure jamani hivi ulishawai ona wapi simu Tsh 2000/=? Hahahaha hao jamaa ukiona wamemuuzia mtu kitu kizima au original ujue walikuja nae hivyo walimshusha mbali akaja eneo la tukio na kujifanya mteje!

Daa pole sana…
 
View attachment 3143388
Aina ya risiti zao

Leo asubuhi kina mama wa mtaa wa Kilungule B wameamka na vilio baada ya kutapeliwa na watu waliokuja kufanya mnada wa vyombo mbalimbali kama masufuria na vifaa vingi vikiwa vya kieletroniki kama simu, laptop, sabufa, pasi na vitu vingine.

Ilikuwaje?

Watu hao wakiwa wanaume kama watano walikuja na magari mawili katika eneo hilo. Wakashuka baadhi na kuanza kuuliza kwa watu vitu mbalimbali. Maswali hayo yalikuwa kama
  • Huku wauzaji wa vyombo vya mnaada wamewahi kuja?
  • Je Watu wakukopesha vyombo vya Uturuki wamewahi kukopesha mtaani?
  • Wengine wakasema tumekuja kufuatilia madeni kwa waliokopa vyombo na hawajalipa
Baada ya maswali hayo ghafla wakaanza kutangaza kwa kipaza sauti kuwa wanafanya mnada wa kuuza vyombo vya SACCOSS vya watu walioshindwa kurudisha marejesho katika SACCOSS. Lakini cha kushangaza baadhi ya vitu hasa sufuria zilikuwa mpya

Kama ilivyo ada kina mama ndio wahanga wakubwa.

Wakajitokeza kwa wingi haswaaaa wakiwa na vimkoba vyao vyenye pesa na wao walivyoona watu wengi wakashusha vyombo vilivyo kwenye gari chini wakavipanga na mnada ukaanza.

Waliuza simu kwa bei rahisi sana, Samsung, Iphone, Vivo na zingine sikumbuki brand bei zake zilikuwa 25,000, 50,000, 70,000, hakuna aliyenunua simu zaidi ya laki.

Ikaja TV kwa laki mbili flat screen na Laptop kwa laki mbili

Lakini cha kushangaza baada ya kufika majumbani simu hakuna iliyowaka, tv na laptop hakuna iliyowaka. Na vifaa hivyo kama simu zilikuwa zimegundishwa na gundi ya superglue vimefungwa fungwa tu maana ilikuwa ni jioni giza linaanza nahisi watu walishindwa kukagua

Walikuwa na Cable za kufanya test lakini baadaye walisingizia kuwa betri haiwaki ili kuchomeka katika umeme.

View attachment 3143387
Hii ni aina ya risiti walizokuwa wanato

Waliwapa watu risiti na wakatoa na namba zao wakidai watarudi, lakini namba ikipigwa wanasema kila mtu anajibu lake mara mwenye simu hayupo, simu haipatikani au kuzimwa

Hii ni namba nyuma ya risiti yao

Sasa huu ni utapeli mpya au kuna watu wanalizwa huko?
Huu utapeli wa kwenye mnada wa vyombo haujaanza leo, sema nini, mbinu za kutapelia watu hubadilishwa kila siku kama nguo.
Huu ujinga ulikuwepo na Kariakoo kipindi cha nyuma.

Unakuta mtu anauza nguo za mitumba kwa bei kitonga kazikunja pamoja vizuri, ukibeba bila kuhakiki ukifika nyumbani aidha ni marapurapu au nguo za blauzi za kike,wakati wewe ulipatanisha kununua mashati.
 
Tatizo sio hao wafanya mnada tatizo lipo Kwa wanunuaji,ulisikia wapi smart phone inauzwa 25k.Duniani ukiwa mtu wa tamaa tamaa kila siku kwako itakuwa ni vilio tu mpaka siku ya kufa kwako.
 
kwamba wamekutwanga na kitu chenye ncha kali kichwani
 
Hawa jamaa ndio hao utawakuta hata pale karume na mahema yao au karibu na kituo cha polisi pale machinga complex,jichanganye uone
 
Mtanzania especially mwanamke akisikia tu bidhaa imenadiwa kwa kibwagizo ”bidhaa zetu tunatoa uturuki” hapo ni sawa na mbwa kwa chatu yaani hautumii nguvu kubwa kujipigia minoti.

Hapo hata kama ni mchina aliyechangamka watajazana na kuelekezana kama kondoo.
 
😂😂😂😂😂😂 Mkuu pole sana najua wewe ni mmoja wa wahanga msipende vitu vya bure jamani hivi ulishawai ona wapi simu Tsh 2000/=? Hahahaha hao jamaa ukiona wamemuuzia mtu kitu kizima au original ujue walikuja nae hivyo walimshusha mbali akaja eneo la tukio na kujifanya mteje!

Daa pole sana…
🤣🤣🤣🤣🤣 sio mimi bwana
 
Back
Top Bottom