Huwezi amini haya yametokea

samilakadunda

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2011
Posts
1,780
Reaction score
355
Naomba kushirikishana juu ya kuzingatia afya zetu najuu ya kumuamini dactari mmoja, hapa Morogoro mjini, ninandugu yangu alipimwa na dactari na kuambiwa anauvimbe mkubwa tumboni, amefanya checkup mara tatu na dactari huyohuyo nakuambiwa majibu yaleyale, akapewa apointment ya kufanyiwa upasuaji, kilaalipopangiwa Dr alipata dharura zaidi ya miezi 5 hukuuvimbe ukikua kwa kasi, ndipo alipoamua kwenda Dar kwa upasuaji, walipo mpima wakamwambia hana uvimbe ni ujauzito wa miezi 8, nakwakuwa umri wake ulikuwa umeongezeka, hakushtuka pamoja hakuona siku zake. Je huyu docta alitaka kuua kiumbe kisicho na hatia? Au ni taaluma ndogo? USHAURI WANGU UNAPOFANYA UCHUNGUZI JUU AFYA YAKO HUDHURIA HOSP TOFAUTI ILI KUJUA UKWELI WA TATIZO LAKO NA TIBA SAHIHI. Tunamshukuru mungu mtoto anaumri wa miezi 11.
 
Labda dk alijua siri ya "uvimbe" ndi maana alikuwa anakwepa! Operation labda alimaanisha cesarean!!??
 
Nduguyo alienda kwa daktari au mganga wa kienyeji?
 

Uja uzito wa miezi nane halafu mwenye ujauzito hajahisi chochote? ..yaani hata huyo kiumbe tumboni alikuwa hajigeuzi geuzi? Yaani mwenye mimba hajahisi chochote?..daah!.. amakweli nchi hii ina watu wa kila aina!..miezi nane?
 
mh.huyo mwenye ujauzito hakuhis chochote jamani? hata mtoto kucheza? ni checkup ya aina gani alifanya? au alibinywabinywa tumbo nini? maan ultrasound unaona kilichopo tumboni wakat unapimwa hata copy inatoka. khaa! nina waswas alienda kwa mganga wa jadi wala sio doctor
 
sihitaji kumtaja jina, ni dr bigwa wa magonjwa ya wanawake, na ni maarufu hapa moro

sasa ukishasema hivi mbona tunamjua, gynacologist yupo mmoja tu, labda kama amehamia hivi soon, na kwakuwa umesema ni maarufu basi huyo si mwingine ni Dr Lyamuya. Anajifanya anajua sana, hataki wenzake wapractice instead anawambia wakasome, wakati nipo intern niligombana sana coz alikuwa hana shule. I know her. Anapenda sana ccd
 
Makanjanja wengi, utakuta alikutana na kanjanja.
 
dactari na mgonjwa walikutana pipa na mfuniko..... Mgonjwa aso jua dalili za mimba had miez nane?
 

where you are!!Dr
 
unajua hawa ndugu i mean drs huwa wananichanganya sana, miezi 4 iliyopita, niliweka bandiko juu ya mke wangu, akiwamjamzito alitokwa na damu nikaomba ushauri hapa nikampeleka hosp, akapigwa utrasound tukiwa wote kwa dr alicoment mimba imeharibika anatakiwa kusafishwa, mimi sikukubaliana na zoezi la kusafishwa, tukakaa kama mwezi mwingne aftercheckup akaonekana ana mimba ya miezi 4 na mtoto anaafya njema, hadinavoandika nategemea kupata mtoto mwezi wa 6, kwahiyo alitaka kuua mwanangu? sometimes i dont trust Drs.
 
Hao ndio ma dk wetu wa dot com. inatakiwa kufanyiwa uchunguzi na mtu zaid ya 1 ili kujiridhisha.
 
Aisee ! Poleni , mbaya sana hii. Hawa madakitari wa siku hizi ni tatizo sana.
 
Aisee ! Poleni , mbaya sana hii. Hawa madakitari wa siku hizi ni tatizo sana.

asante mkuu, nilichojifunza kabla huja chukua maelekezo ya dr, unahitaji kutafakari sana, kuna mimba ngapi zina tolewa kwa uzembe wa watu kama hawa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…