Huwezi ukamfananisha Eddo Kumwembe na Shaffih Dauda

Kwahiyo Eddo ndo shemeji yetu au umeamua kunfagilia mwanaume mwenzio kwa mahaba namna hii?

BTW hao Edo na Shafi ni bongo movie au bongo fleva?
 
Bongo mchambuzi ni Dr. Leaky tu... Hawa wengine wanaziba njaa zao tu...
 
Kwanza mkubaliane sifa ya mchambuzi. Baadaye mwangalie nani mwenyewe sifa hizo.

Ni dhahiri mchambuzi si mtangazaji wa mpira.

Kwangu mimi atakuwa mtu mwenye uelewa mpana wa mpira. Sheria zake zile 17. Anaelewa mifumo ya mpira - 4 4 2, 4 3 3 nk. Anawaelewa makocha na falsafa/mifumo yao.
Anawaelewa wachezaji iwe wa kigeni au kwetu - ubora na udhaifu wao. Nafasi zao uwanjani na ipi mifumo bora kwao.

Mtu mwenye kuyajua haya kwa undani, akajaliwa namna ya kuongea ili watu waelewe, huyo atakuwa mchambuzi mzuri.

Kwa minajili hiyo, naamini Edo ni mchambuzi mahiri zaidi ya Shafii ambaye nadhani ana uelewa mpana kwenye football business.

Dr. Leakey si mchambuzi kwa maana hiyo. Amebobea Kwenye historia na matukio ya mpira. Natamani awepo studio na Edo kila mmoja akifanya sehemu yake.

Kijana George Ambangile anakuja kwa kasi. Mchambuzi mzuri.
 
Wewe una akili. Una waelewa hawa watu na una uelewa mpira huyo ambangile nmemwona pia. Anakuja vizuri sana.


 
Duh....kazi ipo....
 
Kila mchambuzi ni mzuri kutokana na upeo na mahaba ya msikilizaji mwenyewe!

Ungeweka CV ya huyo asiyekuwa na elimu ya kuunga tuone kama yaliyomo yamo kweli though sioni uhusiano wa uchambuzi na Elimu.

Na utuambie Dr Leakey ambaye ni zaidi ya Edo (According to you) ana Elimu gani.

Kwangu mimi Edo namuona ni mjuaji tu kama ilivyokuwa kwa the late Kibonde kwamba yeye anachambua kila kitu (mapishi,siasa,uchumi,soka,muziki,dini) na anaamini pote yupo competent.

To me,kuna kijana yupo Azam na zamani TV1 every Saturday akichambua mechi ya EPL he's the best.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…