Huyu bidada ni mpuuzi, anastahili adhabu gani?

Huyu bidada ni mpuuzi, anastahili adhabu gani?

Melki Wamatukio

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2022
Posts
6,156
Reaction score
10,974
Twende moja kwa moja kwenye kisa. Rafiki yangu kaniomba ushauri kuhusu huyu bidada.

Huyu rafiki alikodi fremu maeneo yaliyochangamka karibu na soko kwa ajili ya kupika na kuuza supu. Wateja wa huyu rafiki wakaanza kulalamika kuwa wanauziwaje supu bila chapati mbili? Akaona ni bora amsake bidada walau awe anapikia pale chapati na kuwauzia wateja lakini faida ni yake mwenyewe, hatozwi hata mia na huyu rafiki yangu.

Mauzo ya supu yalikuwa yakienda kama kawaida nyakati zote, asubuhi, mchana, jioni hata usiku. Siku chache baadae, bidada alianza kupika na chai au maziwa nyakati za asubuhi, baada ya kama siku tatu akaanza kupika ugali na mbogamboga nyingine na kuuzia ndani ya hiyo fremu.

Shida ikaanzia pale wateja walipoanza kuisusa supu! Mi nilikuwa mmoja wao, nikaona sasa ninywe supu ya 1,500 na ndimu kama kifungua kinywa halafu niache chai yangu ya maziwa ya 300 na chapati 4 za 300 300 nikashiba, inaingia akilini kweli?

Hali ilikuwa siyo kwangu tu hata na wateja wengine nyakati za mchana! Ikafikia hatua supu inalazwa, au kumwagwa! Process zote hizi hazikuwa shirikishi kwa rafiki yangu, yaani hakushirikishwa!

Sasa ni siku ya tatu tokea binti aongeze ubunifu mwingine wa kupika supu ya kuku na pweza wakati rafiki yangu ni mpishi wa utumbo wa mbuzi na ng'ombe [emoji23] Biashara imebuma [emoji24]

Ndo ananiomba ushauri amfanyeje huyu bidada? Hata hiyo kauli ya kwenye title sio ya kwangu, ni ya huyuhuyu rafiki yangu!

Istoshe binti kazungumza na mwenye fremu kuwa baada ya miezi mitatu ya jamaa kuisha, ataongeza pesa kwenye kodi ya maelewano ili fremu apewe yeye!

Nawasilisha, ushauri tafadhari!
 
Hapo kuna namna jamaa kaleta mapenzi kazini anashindwa kumcontrol huyo bidada mtu hawezi fanya anavyojisikia kiasi hichi
 
Duuh hiyo ni noma, kuna vitu uspokua mkali unajimaliza.

Bidada kachangamkia fursa chap.
Kwani huyo rafiki yako mpaka mtu anaanza kupika vyote hivyo yeye haoni tuu??

Na hiyo ni lazima tu ingetokea, alichotakiwa kufanya toka mwanzo ni hiyo biashara ya chapat kutompa mtu angeifanya yeye mwenyewe kwa kuajiri mtu.
 
Sasa hapo nn kinamfanya asimwambie, hapo kuna mapenza atakuchosha bure huyo.
 
Kumuachisha kazi hapo kinashindikana Nini wakati bidada amekiuka mkataba
 
Huyo rafiki yako alipewa kdg mbona sioni POWER ya kufanya maamuzi kwenye eneo la biashara kinyume na hapo hiyo biashara anaifanya na kuisimamia mwenyewe au anasubiri RIPOTI akiwa nyumbani. Basi ATAVUNA MAZAO YAKE, mpe pole kama ni yeye na kama ni wewe fanya maamuzi sasa
 
Kama ni wewe au rafiki Yako mna Cha kujifunza sana hapo. Mlifanya biashara kimazoea Sasa dada kaja kuwaonesha biashara inavyotakiwa kuwa, nyie tafuteni sehemu nyingine mkaendelee kupika utumbo Tena bila hata chapati au andazi alafu mzidi kulaumu watu

Mmefundishwa jinsi biashara huwa Ina grow. Acheni lawama, chukueni ni SoMo
 
Twende moja kwa moja kwenye kisa. Rafiki yangu kaniomba ushauri kuhusu huyu bidada.

Huyu rafiki alikodi fremu maeneo yaliyochangamka karibu na soko kwa ajili ya kupika na kuuza supu. Wateja wa huyu rafiki wakaanza kulalamika kuwa wanauziwaje supu bila chapati mbili? Akaona ni bora amsake bidada walau awe anapikia pale chapati na kuwauzia wateja lakini faida ni yake mwenyewe, hatozwi hata mia na huyu rafiki yangu.

Mauzo ya supu yalikuwa yakienda kama kawaida nyakati zote, asubuhi, mchana, jioni hata usiku. Siku chache baadae, bidada alianza kupika na chai au maziwa nyakati za asubuhi, baada ya kama siku tatu akaanza kupika ugali na mbogamboga nyingine na kuuzia ndani ya hiyo fremu.

Shida ikaanzia pale wateja walipoanza kuisusa supu! Mi nilikuwa mmoja wao, nikaona sasa ninywe supu ya 1,500 na ndimu kama kifungua kinywa halafu niache chai yangu ya maziwa ya 300 na chapati 4 za 300 300 nikashiba, inaingia akilini kweli?

Hali ilikuwa siyo kwangu tu hata na wateja wengine nyakati za mchana! Ikafikia hatua supu inalazwa, au kumwagwa! Process zote hizi hazikuwa shirikishi kwa rafiki yangu, yaani hakushirikishwa!

Sasa ni siku ya tatu tokea binti aongeze ubunifu mwingine wa kupika supu ya kuku na pweza wakati rafiki yangu ni mpishi wa utumbo wa mbuzi na ng'ombe [emoji23] Biashara imebuma [emoji24]

Ndo ananiomba ushauri amfanyeje huyu bidada? Hata hiyo kauli ya kwenye title sio ya kwangu, ni ya huyuhuyu rafiki yangu!

Istoshe binti kazungumza na mwenye fremu kuwa baada ya miezi mitatu ya jamaa kuisha, ataongeza pesa kwenye kodi ya maelewano ili fremu apewe yeye!

Nawasilisha, ushauri tafadhari!
Dah nimecheka sana hii dunia hii
 
Aisee, anunue hiyo biashara au amuondoe. She must be given an offer that she can't refuse
 
Wewe umemshauri nini rafiki yako?

Seems huyo mdada yupo smart kichwani kuliko nyie wote
 
[emoji23][emoji23][emoji23]jaman, wanaume Mungu awasaidie
Ngoja nimuite rafiki yangu Edo kissy nimuulize kama mimi ningemfanyia hivyo, angechukua hatua gan
 
Back
Top Bottom