huyu dada vipi,siriaz nisaidieni jamani

Kama unampenda mwambie hutamuumiza. peengine anaogopa huo u handsome wako utapendwa na wengi

Shantel amwambie wapi wakati uwezo huo hana na hata kama uwezo anao dem kashamuona hana mpango na majigambo hayo kuwa ni handsome ameenda south amekuwa sponsored na state house na ashakuwa minister pale UDOM duh na mengine mengi
 
ahhh akimbie tu...akajifagilie mbele ukoooo ..amtafute dul sykes wafungue saccos yao...MAFAGIO SACCOS

Rose1980 wakiwa na Dul na yule rais wa masharobaro wanafaa kabisa kufungua hiyo Saccos
Ila kw adem hapo ajue amekikwaa kisiki
 
Haya handsome boy mwambie tu kama ni wako atakuwa wako
 
wakuu mimi ni mgeni humu jamvini,nilikua navisit tu kambla ya kuregister.haka kajamaa lugha ya malkia inampiga chenga kidogo.me nahic angetumia lugha ya kiswahili mpaka mwisho.sasa yeye anabrag na kujiboast sana.uhandsome wake sio kigezo hata kidogo.he thinks he is more previlaged to win any girl.
 
Kwa kweli ulivojieleza...nina wasiwasi hata kama huyo demu alikujibu hivyo kwa kuhofia kuchanganywa na wengine.
Huyo kakupaisha tu akijua ndicho unachotaka kusikia!
Pole...
Btw, ushapata kazi HB? nenda kafanye modeling.
 
Huyu jamaa mshamba kweli,yan kwenda south africa akakaa cku mbili ndo anaona katembea...hawa ndo wanaofanya udom idharaulike yan.
 
Huyu jamaa mshamba kweli,yan kwenda south africa ndo akakaa cku mbili anaona katembea...hawa ndo wanaofanya udom idharaulike yan.

yaan acha tu
udom kwa sasa inaonyesha jins gan ilivyo....


et ndo alikuwa minister wao....anaonekana mweupeeeeeeeeeeeee kichwan...sjui katokea kashoz...(mhh samahanin jaman...jst jokes)
 
kama ckosei utakua umegraduate wt ba-arabic.
 
Nimekokotoa IQ ya Mh. Handsome inacheza kwa kiwango cha 30-40, sijui amemudu vipi masomo ya chuo kikuu, nakushauri upeleke shauri lako facebook wanaokufahamu wanaweza kukusaidia vema.
 
Hebu andika lugha ya taifa la tanzania tukuelewe mie sijaelewa kabisa hicho kidhungu chako na kufupisha fupisha maneno ndo kabisa........kha!!!
 
ma roomates wa ajabu.hivi unamwambiaje mwanaume mwenzako kwamba uko attractive ! na wasiwasi na hawa jamaa
 

Dogo una safari ndefu sana mbeleni baada ya kumaliza UDOM. Kama huwezi hata kuweka punctuation marks wakati unaadika, ina maana hata barua zako za kuomba kazi zinaweza kutupwa kapuni mapema sana. Angalau, suala la grammatical errors linaweza kufumbiwa macho kwa kuwa linaweza kurekebishwa, na pia inategemea umesomea kitu gani (yawezekana umesoma hesabu); lakini si hili la punctuation marks kwa kuwa linafundishwa tangu shule ya msingi.
 

crap! Crap! CRAP!!!!
 

Mie ndo kamenichanganya kabisa sijaelewa hata kamezungumzia nini,
Halafu kameita News Alert wajameni haya
 

Masaki taratibu mkuu maana jamaa bado mgeni na ndo kaingia inawezekana ikawa post yake ya kwanza.
 

upo chuo kweli? Manake naona hata kujieleza ni tatizo,
au ni mmojawapo wa wanasayansi wachache wasioweza kujieleza vizuri.

Nikisoma maelezo na kuyatafakari nahisi kama unatangaza soko kiaina,
manake umesisitiza sana u handsome wako,
nahisi kama unauona kama ni dili sana kwako,
au ndo njia ya kupata mahusiano mapya??,

jaribu kujipanga upya kwenye maelezo yako,
jaribu kujieleza vizuri mdogo au mtoto wangu,
ukiendekeza kuji handsome sana haitakusaidia sana,
lililo muhimu wewe jitambua tu kuwa ni mwanaume.
 

Nina hakika kwa maswali haya na mashambulizi haya hatarudi tena humu au atakuja na ID mpya kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…