Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 33,679
- 49,841
Siku za karibuni nilitembelewa na mpenzi (mchepuko) wangu, na ilipofika jana jioni nikaona nimtoe 'out' kidogo, tuende 'club' moja kusikiliza mziki pamoja na kuburudika.
Mpenzi wangu akaomba, huku akinilazimisha; avae kikaptula kifupi, pamoja na tshirt ya nyuzi nyuzi, kwa sababu kuvaa kwake hivyo ndio atajisikia vizuri; kwa sababu yeye ni mtu wa kwenda na wakati.
Nikatafakari, nikaona hakuna tatizo; ila baadaye nilikuja kugundua kuwa huwa anataka 'attention' za watu. Akipita mahali, kila mmoja amkodolee macho kwa uzuri alionao.
Ikabidi tuingie 'club', tukapiga vinywaji vyetu, pamoja na kucheza mziki. Ilipofika saa tisa, tukarudi nyumbani.
Leo majira ya saa tisa mchana nikapigiwa simu na mchepuko wangu wa zamani ambaye yupo mkoa mwingine, alipiga mara ya kwanza sikupokea, akapiga mara ya pili sikupokea pia. Ikabidi nimtumie ujumbe, nipo kwenye kikao nitafute baadaye.
Saa 12 jioni akanipigia; ikabidi nipokee simu yake, ili niweze kumsikiliza. Akasema alikuwa anataka anijulie hali tu, nami nikamwambia niko powa. Pia akasisitiza, ijumaa tuonane kwa ajili ya kukumbushia penzi. Nikamjibu, tutaanglia kama muda utaruhusu.
Baada ya mazungumzo hayo; akaniambia ameota ndoto mbaya juu yangu; mi nikamuuliza, inahusu nini? Akasema, nimeota juzi ulienda 'club' na mwanamke, alikuwa amevaa pensi ya rangi nyeusi, na pale 'club' mlifanya 1,2,3.
Ingawa aliyosema ni sahihi, ila kwenye siku alichanganya; mi nikamjibu hakuna kitu cha namna hiyo, nilikuwa nyumbani nafanya mambo yangu na wala sijatoka na mtu.
Basi, akasema; itakuwa ndoto yake si ya kweli. Hofu niliyonayo, huyu binti ni mtu anayependa sana mambo ya kwenda kwa babu, hasa kuhusu mambo ya biashara zake. Inawezekana, kwenda huko alijaribu kunipiga chabo; ndio akapewa hayo maelezo.
Hapa nilipo nimetafakari sana; nikaona Ijumaa hakuna ulazima wa kukutana naye, ingawa amesisitiza sana; hofu, ni kutotaka kuingia kwenye mtego nisioujua.
Wakuu, ushauri wenu muhimu.
Mpenzi wangu akaomba, huku akinilazimisha; avae kikaptula kifupi, pamoja na tshirt ya nyuzi nyuzi, kwa sababu kuvaa kwake hivyo ndio atajisikia vizuri; kwa sababu yeye ni mtu wa kwenda na wakati.
Nikatafakari, nikaona hakuna tatizo; ila baadaye nilikuja kugundua kuwa huwa anataka 'attention' za watu. Akipita mahali, kila mmoja amkodolee macho kwa uzuri alionao.
Ikabidi tuingie 'club', tukapiga vinywaji vyetu, pamoja na kucheza mziki. Ilipofika saa tisa, tukarudi nyumbani.
Leo majira ya saa tisa mchana nikapigiwa simu na mchepuko wangu wa zamani ambaye yupo mkoa mwingine, alipiga mara ya kwanza sikupokea, akapiga mara ya pili sikupokea pia. Ikabidi nimtumie ujumbe, nipo kwenye kikao nitafute baadaye.
Saa 12 jioni akanipigia; ikabidi nipokee simu yake, ili niweze kumsikiliza. Akasema alikuwa anataka anijulie hali tu, nami nikamwambia niko powa. Pia akasisitiza, ijumaa tuonane kwa ajili ya kukumbushia penzi. Nikamjibu, tutaanglia kama muda utaruhusu.
Baada ya mazungumzo hayo; akaniambia ameota ndoto mbaya juu yangu; mi nikamuuliza, inahusu nini? Akasema, nimeota juzi ulienda 'club' na mwanamke, alikuwa amevaa pensi ya rangi nyeusi, na pale 'club' mlifanya 1,2,3.
Ingawa aliyosema ni sahihi, ila kwenye siku alichanganya; mi nikamjibu hakuna kitu cha namna hiyo, nilikuwa nyumbani nafanya mambo yangu na wala sijatoka na mtu.
Basi, akasema; itakuwa ndoto yake si ya kweli. Hofu niliyonayo, huyu binti ni mtu anayependa sana mambo ya kwenda kwa babu, hasa kuhusu mambo ya biashara zake. Inawezekana, kwenda huko alijaribu kunipiga chabo; ndio akapewa hayo maelezo.
Hapa nilipo nimetafakari sana; nikaona Ijumaa hakuna ulazima wa kukutana naye, ingawa amesisitiza sana; hofu, ni kutotaka kuingia kwenye mtego nisioujua.
Wakuu, ushauri wenu muhimu.