Huyu trafiki kumkaribia hivi Rais sio hatari?

Huyu trafiki kumkaribia hivi Rais sio hatari?

mngony

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2012
Posts
5,555
Reaction score
6,972
Kuuliza si ujinga, wengine utaalamu wetu ni kwenye kuhesabu pesa counter, Je kitendo cha huyo Traffic kumkaribia Rais namna hiyo sio Security Breach?

Ukiangalia kwa umakini alikaribia mno tena kupita nyuma ya hao Walinzi wenye silaha nje nje, kwa akili zangu za kawaida naona hatari maana kama mtu mbaya na mwenye mafunzo anapita karibu hivyo anaweza kuwapokonya hao akafanya fujo

Lakini pia baada ya kuambiwa huku usipite pita huko akamgusa huyu afisa mmoja kiunoni kwa nyuma kiasi anaweza kugusa silaha iliyofichwa mfukoni.

Na kuonesha kuwa halikuwa jambo la kawaida, amevuta attention ya karibu wana usalama wanne mpaka watano mpaka waliokuwa karibu kabisa na Rais, kiasi wamegeuka na kumtizama kwa sekunde kadhaa wakati anaondoka, hata huyo Kamanda aliyepigiwa saluti hajamuelewa kabisa huyo askari kamuangalia kwa mashaka.

Hiyo haiwezi kuitwa Security Breach au ni kawaida tu






 
Huyo trafiki ni kama amefanya kusudi kumsukuma mwanausalama baada ya kuelekezwa kwa kupita. Kimsingi, hapo kulikuwa na makosa na huyo trafiki hakufanya vyema kumsukuma mwanausalama na kumtwangia saluti mkuu wake tu.

Lipo jambo la kuchunguzwa na kurekebishwa hapo. Binafsi, sikupenda namna huyo trafiki alivyomsukuma kwa makusudi( tazama mkono wake wa kushoto) mwanausalama.
 
Mfumo wa ulinzi wa mama unatia shaka pakubwa sana kuna picha moja nimeona mlinzi mwanamama kavaa high heels? Hivi wapo serious kweli na uhai wa huyu mama?

Ni kawaida kwa walinzi wa kike kuvaa travolta ila huyu kanishtua kwa kweli leo, mlinzi anavaa kama anaenda ofisini.
 
Mhmhmhmh!

Tuanze mdogo mdogo kwanza!

Kwanza tuelewe mizunguko (guarding circles) inayomlinda Mh Rais. Tukiachana na mzunguko huo ambao umo ndani ambao hatuuoni, kuna mizunguko mitatu iliyo dhahiri katika video.

Mzunguko wa tatu upo huo wa polisi pamoja na wanausalama waliovalia kaunda suti. Unaona kabisa Trafki anaupita na kujitokeza kuukabili mzunguko unaofuata. Hao walijisahau kabisa.

Mzunguko wa pili ni huo wa Wanajeshi walioshikilia mitutu mikubwa mikubwa.
Ukiangalia kwa umakini, kuna mwanajeshi mmoja anamnong'oneza afisa (katika mzunguko wa tatu) kitu. Kumnong'oneza huko kukamfanya kupoteza focus ya kuangalia kwa umakini

Isingelikuwa huyo mwenzake kumuwahi huyo Trafiki na kumuamuru asipite huko bila shaka angelipita karibu kabisa na circle ya kwanza.

Mzunguko wa tatu, unahusisha wanausalama wengine pamoja na huyo mnayemwita Mpambe. Baada ya kuamuriwa kwa kusukumwa trafiki analazimika kupita katikati ya mzunguko wa pili na wa tatu.

Trafiki alifikaje?
Kwanza ametumia advantage ya yeye kuwa sehemu ya usalama. Amevalia kitrafiki.
Akapata upenyo kusogea ndani zaidi.

Lakini tukubali kuwa kuna uzembe ulifanyika wa kumpuuzia.

Hata baada ya kusukumwa anaondoka kwenda kumuagamia mwanausalama kiunoni. Sijui ni makusidi ama kukosa balance.

Huenda ni makusudi kwa kuwa hakusukumwa kwa nguvu sana. Ni kidogo tu. Lakini pia, askari anatakiwa awe mkakamavu, force kidogo kama ile si ya kukuyumbisha kutaka kuanguka.
Huenda si makusidi kwa sababu:
Uoga ulichangia kukosa balance. Nafasi baina ya aliyesukuma na aliyetaka kumuangukia haikuwa ya kutosha.

Je, ni threat?
Hapana, kwa sababu hakusababisha usumbufu wa aina yeyote. Alishindwa kuelewa mipaka yake, mahali anapotakiwa kuishia.

Ila uzembe umefanyika kwa kikosi kushindwa kumzuia kutofika huko.
 
Huyo trafiki ni kama amefanya kusudi kumsukuma mwanausalama baada ya kuelekezwa kwa kupita. Kimsingi, hapo kulikuwa na makosa na huyo trafiki hakufanya vyema kumsukuma mwanausalama na kumtwangia saluti mkuu wake tu.

Lipo jambo la kuchunguzwa na kurekebishwa hapo. Binafsi, sikupenda namna huyo trafiki alivyomsukuma kwa makusudi( tazama mkono wake wa kushoto) mwanausalama.
Hata huyo mwanausalama hajamuelewa kageuka kumtizama sana
 
Kuuliza si ujinga, wengine utaalamu wetu ni kwenye kuhesabu pesa counter, Je kitendo cha huyo Traffic kumkaribia Rais namna hiyo sio Security Breach?

Ukiangalia kwa umakini alikaribia mno tena kupita nyuma ya hao Walinzi wenye silaha nje nje, kwa akili zangu za kawaida naona hatari maana kama mtu mbaya na mwenye mafunzo anapita karibu hivyo anaweza kuwapokonya hao akafanya fujo

Lakini pia baada ya kuambiwa huku usipite pita huko akamgusa huyu afisa mmoja kiunoni kwa nyuma kiasi anaweza kugusa silaha iliyofichwa mfukoni

Na kuonesha kuwa halikuwa jambo la kawaida, amevuta attention ya karibu wana usalama wanne mpaka watano mpaka waliokuwa karibu kabisa na Rais, kiasi wamegeuka na kumtizama kwa sekunde kadhaa wakati anaondoka, hata huyo Kamanda aliyepigiwa saluti hajamuelewa kabisa huyo askari kamuangalia kwa mashaka.


Hiyo haiwezi kuitwa Security Breach au ni kawaida tu
View attachment 1846143[/SIZE]
Kweli kuna yeyote duniani anaweza kumdhuru mama yetu? Kuna yeyote ana uthubutu wa kunyanyua mkono na kumdhuru mama? Hamna kabisa
 
Back
Top Bottom