Na mimi nawapenda wanawake sana sana, ashukuriwe aliyeumba maua haya yaipambayo dunia...sifa zivume kwa mfalme wa wafalme awezaye kufanya mambo makubwa ambayo akili zetu wakati mwingine haziwezi kuyaelewa. Ombi langu awasaidie wanaume wote kuyapata yale maua wanayoyatamani ili wamtukuze milele kwa jambo hili jema alilowaumbia.
Wewe nakupenda zaidi.......:smile-big::smile-big:Asante kwa kutupenda,,ubarikiwe sana
Kama wewe ni mwanamke, tafadhali pokea pongezi na furaha yangu kwa dunia hii kuwa na viumbe adhimu na wa pekee wa aina yenu. Ahimidiwe Mungu aliegundua dunia bila ninyi haikaliki (kama unaamini uumbaji)
- Nawapenda kwa tofauti mnayofanya kwenye dunia yetu. Each new day, women make some difference in this world. Yes indeed.....Its unfortunately not seen by many, but you are so fantastic
- Najaribu kufikiri namna mlivyobeba mimba za watu kama mimi kasha zikaitwa zisizopangiliwa na mwaliowapa mimba wakawakimbia .hata hivyo, you never give it up, you carried us through alone mpaka tukazaliwa kwa nini nisiwapende jamani?
- Navuta kumbukumbu mnavyotumia siku yenu kufikiria na kuwazia watoto wenu zaidi ya sisi wanaume tunavyofanya. Kwa mbali namuona mwanaume anamka asubuhi na kupiga starter ya gari kuona kama iko vizuri kwendea ofisini kisha anarudi ndani na kupanga makabrasha yake wakati mwanamke ndani anaandaa mavazi ya mwanaume kwenda kazini na mtoto kwenda shule (huku akitakiwa kujiandaa mwenyewe kwa kuwahi kazini)
- Navuta hisia baba yuko busy na laptop pembeni wakati attention ya mama iko kwenye kumfundisha mwanae kuvaa vema suruali au kaptura yake
- Navuta hisia za wakti ule nilipokuwa nikiishi bila mwanamke ndani ya nyumba yangu nilifanya mengi nikafanikiwa na mengine sikuona umuhimu wa kuyafanya. Alipoingia tu ndani ya nyumba yangu mwanamke, she made a difference. Nikaanza kufanikiwa zaidi ya awali na zaidi nikaanza kuona yale niliyokuwa naona hayana maana kwa sasa kuwa ya maana. I mean, your presence and advises in our lives, take us into highest reaches, viwango vikubwa zaidi ya kama hamko kwenye maisha yetu
- Jamani nyie ni fluid ya dunia hii. Ni sawa na zile za kwenye magari kuzuia msuguano unaoweza haribu vyuma kwenye gari. Ninyi mnaifanya dunia ikalike. You are the fluid na mnajua kuweka balance nzuri. We angalia hata hapa JF, tukishatifuana kule kwenye Jukwaa la kupandisha viharusi na kufanya systolic/diastolic readings zetu ziwe juu, tunakimbilia huku....ukifika huku unakuta kuna Preta....unapata neno moja na kiharusi chote chali...unamkuta Rose1980, mara hujakaa vizuru mara AfroDenzi na wengineo wengi...pressure inashuka na unarudi tena Jukwaa la makeke ya kina DSM na Zomba.
Ni mengi kwa kweli na siwezi kuyamaliza hapa. Wenyewe mnayajua na wanaume ni mashahidi wa haya, mimi nikiwa mstari wa mbele
Nawachukia sana wanaowafanyia haya
- Wanaume wanowaona si mali kitu wakati mliwabeba miezi na miezi matumboni mwenu. Hebu waambieni wanaowadharau wajaribu kufunga matambara kwenye matumbo yao na watembee nayo kwa siku nzima kama wataweza thubutu, hii ya kupigwa mateke tumboni ni hatari, nakumbuka wife alivyokuwa akilalamika bwa mdogo anamkandamiza mateke na magumi tumboni....naamini ni kweli...
- Wanaume wanaowapiga hawa nawachukia zaidi. Sijui jibu la ni kwa nini mwanaume anafikia hatua ya kumpiga mwanamke. Nimejiandikia kati ya ujinga nitakaofanya duniani ni kuinua mkono wangu kumgusa mwanamke nikikasirika sana na mkono ukiwahsa nitapiga ukuta, ila kwa mwanamke sitampiga, nitamnunulia zawadi nzuri itakayomfanya avute masikio yake nimueleze kuwa alinikosea na nikajisikia vibaya
- Wale wanaowafanya kama substances/instruments fulani za purpose ya ku-serve shida zao za muda. Hawa wanajiita playboys, mabingwa wa hit and run ..Hawajui utamu wa kukaa na nyie ndani. Wangejua wangeamua kukubaliana na mmoja na kukaa nae ndani na hatimaye kupata ile raha ya kukaa na nyie kwa utulivu
Hebu nisiwachoshe JAMANI WAPENZI WANGU LADIES, NI MENGI NINGESEMA ILA FAHAMUNI TU KUWA NAWAPENDA KWA SABABU YOU MAKE THIS WORLD HABITABLE AND DIFFERENT AND YOU TAKE MEN HIGHER JAPO HUWA TUNAJIDAI HATUONI (Sio kuwa hatuoni, ila huwa tunajiai hatuoni).
Wewe nakupenda zaidi.......:smile-big::smile-big:
you are damn right!!.........just a question.........nani kauvunja? i will replace it.......i have got two unused hearts.am sure u won't break my heart,but rather u will make it :smile-big:
basi watakavyo kuja mibichwa imevimba hapa mh! l.o.l
am sure u won't break my heart,but rather u will make it :smile-big:
you are damn right!!.........just a question.........nani kauvunja? i will replace it.......i have got two unused hearts.
i will replace and install electric fence around it. How about that?!
Mtoa mada mke wako ni mwanamke mwenye bahati sana kupata mume kama wewe
you are damn right!!.........just a question.........nani kauvunja? i will replace it.......i have got two unused hearts.
i will replace and install electric fence around it. How about that?!
Mtoa mada mke wako ni mwanamke mwenye bahati sana kupata mume kama wewe
Ni-PM nitakupa story kamili. Mimi sio fundi Moyo, ni replacer wa mioyo iliyokata tamaa
We Big....where did you get them....mmmhhh!!!!!
maty umeona ee?
Mtoa mada I salute you!
At least ndo nachoweza kusema ili kuitendea haki thread hii tamu.
Salute to all women....My mama, wife, kids, wajukuuz and all women in the world. Bila nyie, dunia isingekuwa sehemu tamu ya kuishi.
Amen!
I am just a call away.......you know that.come zis way basi,,haujavunjwa lkn nimeweka alert naogopa kuvunjwa mie