I will kill him 4 my kids

Kwa kweli ningesafiri hadi nigeria kama si kutafuta na mie nguvu hizo basi kwa mtume joshua, angenisaidia tu, huyu mwanaume katokea sayari gani wajameni, sijawahi ona, mke amwache mwenyewe, wivu wa nini?
Katokea sayari ya Tanga waja leo warudi leo
 
malipo ya ubaya ni hapahapa duniani...... 3 answers; 1. dada akate contact na huyo jamaa(simu)-change number 2. hama mtaa, mkoa 3. timiza lengo-kill him
mengne yote alishafanya ila ufanisi ukawa kidogo labda la kumkill tu sasa
 
mwaka jana walitalikiana, ndoa ya kanisani haifi
Hii situation ni ngumu kidogo, umesema wametalikiana hapo2 ndoa ya kanisani haifi, maybe ungeetueleza vizuri uliposema wametaliakiana wamepeana divorce au wameseparate, mana kama ni separation kweli bado ni mkewe kama ni divorce hapo hakuna ndoa.
watoto wanaugua ugua (kipepo, wakipelekwa kwa walokole wakiombewa wanapona
Hapa pia sijaelewa kwamba watoto wanalogwa! kwani rafiki yako ameelezwa huko kwenye maombi! All in all yuko kwenye hali ngumu inatakiwa wewe kama rafiki umpe support sana asijefanya maamuzi magumu kama anachotaka kufanya. Kwanza anaweza kuanza na wazee wa familia ya mumewe awaeleze kila kitu na kama anaevidence haswa kwa kupigwa jamaa anaowapata na kuguua watoto aseme kila kitu. Kuhama mkoa au nchi well ni wazo zuri but ina effect zake kwenye kuanza maisha sehemu ambayo hujazoea. Umesema ni strong woman inabidi apambane na tatizo na sio kukimbia maana hata akihama huyo kichaa anaweza kumfuata huko aliko. Aanze na ndugu za mtalaka wake, pia asali sana ili kuwa protect watoto wake na yeye pia. Aeleze pia na ndugu zake ili wajue situation aliyokuwa nayo. Pia kama anaevidence za kutosha amshitaki jamaa kwamba anamharass! asijaribu kumrudia huyo jamaa he is a monster! poleni sana
 
Pole zake nyingi huyo mama,
aondokane kabisa na hilo wazo la kumwua ex mume,
hiyo dhambi ya kuua itamtesa zaidi ya hayo mateso ayapatayo sasa.
Bali azidishe maombi na awe na imani na anachoomba kwamba kinafanikiwa,amwamini
mungu kwa moyo wake wote,akili zake zote pasipo kuwa na shaka,huku akiamini,
kuwa mungu hachelewi wala hawaishi maombi yake, pia aamini kuwa hakuna,
linaloshindikana kwa mungu.
Suluhisho la tatizo lake siyo polisi wala ndugu wa mumewe bali ni mungu pekee,
kwa mtaji mdogo tu wa imani yake kwa mungu kuwa anaweza yote. Pia azidishe bidii,
katika masomo yake ili baadaye apate kazi nzuri tayari kwa kuwatunza watoto wake,
pia apunguze hiyo imani ya uchawi katika akili yake, watoto wakiugua ahakikishe anawapatia,
matibabu bora.

Kumwua huyo ex mume siyo suluhisho la matatizo yake bali litakuwa ni kujiongezea,
matatizo zaidi. Mimi naamini kila tatizo kama lina mwanzo basi,
hata mwisho wake haukosekani.
 
Kumua siyo jawabu. Watoto wanaweza kuwa yatima kimchezo mchezo. Baba kafa na mama jailed for life. Mwambie atumie njia zote mbili , ya dini na ya kisheria (injunction order etc).
Mwambie awepeleke watoto for full medical check up/treatment kujua nini kina wasumbua. Baada ya kama anaweza kuzuia visitation za Baba kwa misingi ya kutesa au ketelekeza watoto na pia ahame mji km kutoka kaskazini kwenda kusini.
 

Nguvu za giza ziko kazini. Huyo Dada amtegemee Mungu zaidi kupata ufumbuzi.
Maneno mengi hayatoi jibu.
Kwa ushauri tu mwambie atafute nafasi aende mwenyewe kwenye huduma za Maombezi Riverside awaulizie watendakazi na kuwaona kwa faragha. Ishu hiyo ni nzito kwa sababu inahusisha roho nyingi.Siri ya kupata mafanikio ukiwaona ni kusema ukweli wote ili Mungu aweze kutoa majibu haraka.
 
Nitamwambia.
 
Nitamwambia.

Pole sana dada Sabry001.

Ktk msg yako jana (kama sikosei) ulisema uko-divorced! Could this be your own experience? Either way, Mungu akusaidie/amsaidie rafiki yako asiingie ktk kiwango kingine cha ubaya na mateso kwa kujaribu kulipa ubaya kwa namna hiyo iliyokusudia. Hakika kumuua huyo bwana kutaleta mateso makubwa zaidi maishani mwako/mwake - pale uta/atakapo kuwa akiwaona wanawe yatima kwa mauaji uliyo/aliyotimiza mwenyewe. Ni kosa ambalo halitaweza kuwa reversed, na hivyo majuto yake na mateso yake yatakuwa ni ya maisha!

Tabia ya huyo bwana hakika ni ya muda, na itaisha either kwa yeye kubadilika somehow (kwa kukua/ kushauriwa/ maombi, kuzuiwa kisheria etc). Tafuta uponyaji na ulinzi wa Mungu kwa watoto na kwako/ke, na tafuta wazee/watu anaowaheshibu huyo baba wamshauri. Ikishindikana ni bora hata kumfunga gerezani, lakini si kumuua.

Mungu awasaidie.
 
Kisasi ni cha Mungu kwa kweli. Yule mkaka amepata ajali mbaya ya gari na niandikapo ujumbe huu tumetoka kumfukia. Nadhani rafiki yangu atapata amani sasa. Maombi yana nguvu nimeamini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…