Ibada kuu ya Eid el Fitr Morogoro Municipal

Clark boots

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2017
Posts
6,770
Reaction score
6,202
Habari za majukumu JF members wote.

Mungu ni mwema na hatimaye yamebaki Masaa tu kama sio dakika tuimalize Ramadhan ambayo imechukuwa Siku takribani 30.

Ni furaha ilioje kwa Waislam wote na wasio Waislam kesho kusheherekea sikukuu ya Eid baada ya kumaliza Mfungo salama salimini.

For now nipo Morogoro mjini, si mwenyeji kihiivyo but nahitaji nifahamu wapi(Kiwanja) itafanyika ibada/Swala ya IEDD kimkoa (hapa mjini) maana nahitaji kesho panapo majaaliwa nijumuike na Waislam wenzangu kufanya Ibada hii Adhim kwetu.

Asante
 
Bakwata na viwanjani wapi na wapi?.hapo ni ndani ya msikitini
 
Waliosherehekea Leo ndio wamefanyia viwanjani.,
 
Siku zote ibada ya eid Morogoro inaswaliwa kwa misikiti na sio kiwanjani... So jiandae kwenda "boma road" ama msikiti wa mafiga "kwa mahita"
Akiamka asubuhi achukue boda apelekwe Msikiti mkubwa uliopo Boma road.
 
Mkuu mwezi kweli ni mkubwa lakini sio suala la kubeza kwa sababu jana kulikuwa na mawingu hivyo walikuwa sahihi kwa upande wao kutokuuona jana.

Mimi leo nimesali nikamsikia mtu analalamika yeye anasali kesho anasema daah lakini mwezi mkubwa ule,nikamuambia kwa hapa tulipo ule ni wa leo


Hizi ni khiLaaf zisitugombanishe kabisa.

Hata hapo zamani wanazuoni walitofautiana juu ya suala la mwezi lakini hawakutukanana juu ya utofauti wa misimamo yao kila mmoja alimheshimu mwdnzie.

Mimi nimekula leo lakini siwezi kusema kuwa ule mwezi wa jana kamwe,nitasema wa leo kwa sababu umeonekana leo na watu wengi.

Mimi nimekula leo kwa kuamini kuwa mwezi wa popote unanihusu na mimi maadamu nimepata taarifa.

Wengine wanaamini mpaka uandame nchini kwao kwa sababu ndio asli ufate pale ulipo kwanza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…