Kwanza kabisaaa naweza kutoa ushauri mdogo na wa akili ambao mnaomjuwa Richard Mavoko naomba mumfikishie ujumbe na haya ni mawazo yangu kama shabiki yake ambae nilikuwa nafatilia sana nyimbo zake...kwanza kabisaa naweza kusema Rich Mavoko umefanya kosa kubwa sana kujoin WCB kitu ambacho hutokuja kusahau kwenye maisha yako
Kwa nini nasema hivyo nimesema hivyo kwa kwa sababu wewe ulikuvyokuwa unakuja ungeweza kuwa mpinzani wa Diamond kwa kiasi kikubwa sanaa,ok why nasema hivyo kwa sababu nyimbo zako kwa kiasi kikubwa sana zilikuwa zina hit na watu wengi wanazipenda na kukuita Diamond wa pili je swali nini kimekushawishi kuingia WCB??naweza kutoa jibu na kusema kwamba huko WCB nona uwakika wamekutafuta na kukuomba ujoin kwenye rebo yao ili wakumalize kimziki na usizodo kutamba
Nikuambie msemo mmoja unasema kwamba ukiwa unafanya kazi kwa mtu kamwe huwezi kuwa na hela kuliko yeye mwenyewe unaemfanyia kazi hapa namaanisha kwamba kujoin WCB under Diamond ni kwamba kamwe huwezi kuja kufanya mziki ukawa mzuri na kukibalika kumzidi yeye mwenyewe Diamond ambaye ameku sign....kitu kingine ni kwamba Management yako au manager wako atakuwa amekula hongo kubwa kukushauri wewe uingie kule kana kwamba anajuwa anafanya makosaa....
Mziki wako ulikuwa sio wa kujoin kundi lolote au kusainiwa na mtu yoyote wewe ulikuwa ni mwanamuziki wa kipekee ambaye naamini ulikuwa unaji control vizuri sanaa hata kwenye nyimbo zako mwenyewe bila kumshirikisha mtu yoyote yule ulikuwa unafanya vizuri sanaa je nikuulize swali nini ambacho ulikuwa umekosa mpaka kujoin WCB??
Nikutolee mfano angalia huo wimbo ambao umeachia jana je umewahi kuimba nyimbo za design hiyo hata siku moja??je kama upo naomba uwekwe hapa jukwaani....huo wimbo umetoa jana under WCB hata club ukipigwa hamna atakaye amka na kucheza je huo wimbo vile vile unaweza kwenda kwenye show na kuupiga mbele ya mashabiki??
Mimi kama kaka yako nakushauri kwa roho nzuri na kama shida ni hela nipo tayari kukusaidia na kuku support nashauri au nakushauri sikujui na hunijui wala hatuwahi kuonana nakushauri cancel contract endelea kuwa kivyako endelea kutoa vitu vya maana....angala huo wimbo ulitoa jana aalafu uniambie baada ya miezi 2 kama utahit hata kidogo...
Nipo tayari kuku control na kuwa Manager ikiwezekana kwa kipaji chako ulichonacho nipo tayari kuku control kimuziki