Ibaki Story: Ngoma Mbovu kuliko zote WCB

Bila bias yoyote, mi huwa napenda mziki mzuri iwe hip-hop, rnb au mahadhi yoyote. Kuna kitu kimoja hua nina imani nacho sana katika kupelekea nyimbo iwe nzuri nacho ni ala/mapigo ama Beats/Instrumental. Ukizingatia nyimbo nyingi za siku hizi hazibebi ujumbe bali ni mahususi kwa ajili ya kuleta mizuka/flavor tu ya kusikiliza ama kucheza,Kwa uzoefu wangu beat ikiwa nzuri sana inaweza kuinua hisia za msikilizaji regardless mashairi yawe mazuri au yasioeleweka na mara chache yanaweza kuubeba wimbo usio na mapigo mazuri ila hilo hutokeaga aidha kukiwa na flow nzuri ama yakibeba ujumbe mzito sana.
Ukilifuatilia hilo kwa umakini waweza kuipata point yangu.

Back to topic ya mtoa mada, kwa hio ngoma ya mavoko haina flavor kabisa yani, beat hamna kitu na flow ya mashairi ni hewa tu kulinganisha na nyimbo za nyuma hasa ile "pacha wangu", it was one of his perfect piece of arts. Ushauri ainvest kwa producers wazuri hasa Bob Manecky wa AM records na yule wa Sei records wanaziweza sana beat za likes zake!
Hata Diamond mwenyewe bila mkono wa manecky mungu ndio anajua!
 
Team zitakapokwisha ndio tutapata kuuelewa mziki mzuriii...

Huu wimbo ni mzuri na unaweza kuufananisha na "silali" ...una levo kubwa zaidi ya "natafuta kiki"

Ila nimefurahia jambo moja tu ...bongo flava ya miaka ya nyuma inaanza kurudi maana from aje,mama kija,ndi ndi ndi etc....
 
Sikulaumu unaonekana wewe mgeni humu ndani kaa tulia na pitia thread hapa jukwaa la celebrity utapata majibu yako uliyouliza
Sasa wewe mwenyeji humu ndani huo muda uliotumia kukomenti si ungeutumia kwa kuiweka hiyo linki hapa ??? ( nasema bado mutatuwekea kila kitu kinachomuhusu yeye, TUKIWAULIZA JE, MWANZO MULIKUWA HAMUMUONI/HAMUMJUI MAJIBU MTAHISHIA KUJIUMA TU.)
 
Umeongea ukweli tupu mkuu
 
yeah, mi pia naipenda ile nyimbo iko mukide it sounds great zaidi ukiwa uko booze mdogo mdogo, iko kama blues flani hivi!
Yeah, mashabiki mandazi wasojua mziki mzuri ndo wanaweza kuifananisha hii ngoma na za kina harmonz, Ali K Ana melody ya kipekee sana
 
Kama Mavoko asingejiunga na WCB, leo hii angekuwa hajadiliwi kwa wingi wa comment hizi, kwa namna moja ama nyingine amefaulu kuingia midomoni mwa watu kupitia WCB zaidi ukilinganisha na nyuma.

Nadhani hilo kibiashara ni zuri, jamaa pamoja na kuwahi kutoa ngoma kali kama Mary Me, Pacha Wangu, Roho Yangu nk humu haikuwa kuwekwa thread ikafika page zaidi ya 3.

Mwanzo mzuri kibiashara, ni nina uhakika hii nyimbo itapigwa sana mpaka watu waizoee.
 

Kaka nikuulize kitu kimoja, kabla ya Rich kuingia Wasafi alishawahi kujadiliwa kwenye Media kama hivi?,
we huoni kwa muda mfupi tu tayari amekuwa kwenye vinywa vya wapenda mziki wote?
Hilo ndio lengo hasa, na pia ukae ukijua huwezi hata kama ukiwa mzuri kiasi gani kuna kipindi tu ambacho utatoa nyimbo mbovu hiyo ni kawaida,
Rich Mavocko atakuja kuwa zaidi ya alivyokuwa na kweli atapata pesa akiwa na hao wakina Babu Tale na Mkubwa Fella jamaa wanalijua hasa soko la Tanzania na East Africa kwa upana wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…