Ibrahim Ajibu wa Simba jaman

Mr Mikazo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2016
Posts
1,594
Reaction score
800
PASS YA IBRAHIM AJIBU vs TZ PRISONS

Na prof. Mikazo

Jana kulikuwa na mchezo mkali sana wa wa ligi kuu ya vodacom mabingwa wa muda wote wa CECAFA dhidi ya TZ Prison na Simba kuibuka na ushindi mnonon wa goli 3-0 huku Simba akicheza mpira mwingi sana kama Barcelona

Siongelei Matokeo sababu ushindi kwa Simba n kawaida kama Yanga kufungwa 5 tu lakini ni kitendo cha Ajib kupiga pass ya dunia ambayo Ozil anaota aipige siku moja pass hyo ilienda kwa Mavugo na kufunga goli kaliiiiiiiiiiii

Pass nilikuwa hivi ajibu alipata mpira magharibi mwa uwanja akaambaa ambaa kama Neymar mabeki wakaogopa kumkaba akasogea akainua shingo kama Eagle akawasha indicator akavuta pumzi akaomba dua akamuangalia Mavugo akapiga pass iliyochanganyika vitu vya Modric, Iniesta, Mata, Mikhtaryan, Carrick, Xavi

Inasemekana Pass aliyoipiga ajib cadabra Jana kwenye nchezo wa vpl kwenye physics tunaita Density kwenye hesabu tunaiita Jometri kwenye kiswahili tunaiita Kiarifu kwenye English tunaiita Hawa the bus driver kwenye Stadi za Kazi tunaiita jinsi ya kumpikia baba Mkwe maandazi.

Na kwaatarifa yako mwana ndala chuo kikuu cha Oxford huko kilipo kimeipitisha pass ya ajibu kuwa course mpya it a mayor in dishes chuoni hapo kwa ngazi ya Masters course hyo itaitwa "Ajib pass make oxford great again"

Kule Lamasia pass ajab itatumika kufundishia watoto jinsi ya kutoa assist za videoni sio kupiga madochi tu kama Akizimana

Sasa Mikhtaryan anasema amepata mpinzani anaogopa kufunikwa ajib mutoto ya msimbazi sasa mawakala wanamsumbua huku Mino Raiola akitaka kumeneji ajib cadabra aka roho inapenda

Pass ya ajib Mara ya mwisho ilipigwa kwenye mchezo wa kumkaribisha muitaliano Marco polo wakati aliporejea kutoka Uchina wakati wanamkaribisha Marco Polo nyumbani Italia ukapigwa mchezo wa soka hyo ilikuwa mwaka 1247.

Wakati ile pass inapigwa mgeni rasmi wa mchezo Hugo babu yake Benito Mussolini Mzee Francesco Toldo Mussolini alisimama na kusema " vita congratulazioni molto difficili hanno casa molto buona da mangiare" kwa kiswahili maana yake " Magufuli amefanya maisha yawe magumu sana hapa Italy"

Huyo ndio Ibrahim Ajib Migomba Jana alifanya mbwana samata aandike twitter kuwa pale Genk anakosekana ajib tu watwae champions league msimu ujao.

Valentine day yangu namdedicatia mama watoto wangu pass ya Ajibu [emoji8][emoji8][emoji8][emoji8]
 
pale mchangani kila mchezaji anatamba na sababu zake...

Mavugo alitamba na kuwa maarufu kwa mbio kali akiwa kiwanjani mpaka akawa anaacha mpira nyuma.

Kichura alitamba kwa bao dhidi ya yanga.

Ajibu anatamba kwa pasi tu, tena moja kwanye mechi lukuki alizocheza.


wanaotamba kila week huku yanga..

Tambwe
Ngoma
Chirwa
Kamusoko
Msuva
Kaseke
Niyonzima

yaani hao niliotaja huwa wanatamba kwa ''MABAO TU''

Hakuna mbwembwe za ziada.
 
Mkuu umekuja? Hongera kwa ushindi dhidi ya wavuvi mkuu, kwa hisani ya ajib migomba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…