Idadi ya walioambukizwa Kenya kufikia watu Elfu kumi mwishoni mwa Mwezi April

Idadi ya walioambukizwa Kenya kufikia watu Elfu kumi mwishoni mwa Mwezi April

joto la jiwe

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2017
Posts
26,117
Reaction score
46,617


Wizara ya Afya ya Kenya imesema kwamba idadi ya watu wenye virusi nchini humo inategemea kuongezeka kwa kasi sana na kufikia watu 10,000 ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kutoka sasa, hii itakuwa ni idadi kubwa kuliko nchi yoyote hapa Africa.

Tamko hili toka kwa hawa majirani linaonyesha wazi ni kwa kiasi gani serikali ya Kenya ilivyodhaifu katika kukabiliana na hili tatizo. Wakati ambapo nchi ndogo ya Rwanda imetangaza kuzuia raia wa nchi nzima kutotoka nje " Total lockdown" idadi ilipofika 40, Kenya bado hawaonyeshi dalili yoyote ya kufanya hivyo na hakuna mipango yoyote madhubuti ya kupunguza kasi hiyo zaidi ya kupima na kutangaza walioathirika.

Hii nchi inasababisha mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kuwa magumu sana katika ukanda huu kutokana na uzembe wa viongozi wa Kenya kama kawaida yao miaka yote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ungeyasikia ya Tanzania ungeacha kuwalaum wakenya.... Tanzania rais analala juu ya mawe katika kipindi hiki cha mapambano, rais anakunywa kawahawa kijiweni katika kipindi hiki na Anasema raia wasiogope corona Ni shetan.... Bila shaka ukiyasikia haya ya Tanzania utaacha kuiponda kenya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiona hivyo basis ujue wana idadi.kubwa kuliko inayotajwa sasa!!!! Kama Kenya wakifika 1,000 basi Tanzania kwa hatua tunazochukua tutakua na wagonjwa 10,000
 
Ndio kutishana kwenyewe huku Tanzania inakupiga vita

Kuna haja gani ya kuwatengenezea wananchi taharuki kihivyo?

Huku Tanzania kinachosisitizwa ni kuchukua tahadhari lakini mambo yaendelee kama kawaida, watu wachape kazi kama kawa Hakuna wa kukuletea sahani ya wali mezani.
 
Back
Top Bottom