idadi ya watoto vs maisha bora

Kuzaa inategemea uwezo wa kuzaa na uwezo wa kutunza. Unaweza kusema unataka 2, kumbe hata ukishapata huyo 1 ndiyo huwezi tena, kiafya (nimeshaona mfano). Na pia unaweza kutaka wengi na ukawapata wakakushinda kutunza. Lakini wapo pia waliopata watoto wengi (8, 10 au zaidi) na wamewatunza wote vizuri, inategemea na walivyojizatiti kiuchumi na kijamii, na uimara wa uhusiano wao kama familia.

Kama ni suala la utafiti, ni vigumu kupata idadi ya wastani ya watoto ambao unaweza kupendekeza wanandoa wazae, maana hayo masuala ya social and economic stability yanatofautiana sana baina ya watu.

Mimi nitazaa wangapi? Nitaangalia hali itakavyokuwa wakati huo ninapozaa, na kama yapo matumaini ya improvement. Nilishaona mtu fulani alizaa watoto 2 tu kwa sababu eti hali yake ya uchumi ilikuwa mbaya. Lakini wale 2 walipomaliza sekondari, biashara zake zikamkubali akapata pesa nyingi sana. Akaanza kubwabwaja kuwa angejua angezaa wengi zaidi. Sasa ya nini kujilaumu baadae?

Tunaishi kwa matumaini kuwa hali itakuwa bora huko baadae kutokana na bidii tunazofanya. Hivi kama mimi sasa hivi naishi chumba cha kupanga, niogope kuzaa ati kisa sina nyumba? Sasa nikifika miaka 50 nikapata nyumba yangu mwenyewe, nikizaa muda huo nitatunzaje hao watoto.

Namalizia hivi: Kama unaweza mahitaji ya kawaida ya mtoto kwa wakati huu, zaa. Kama una wawili na hushindwi kumlisha wa 3, na huna shida za kiafya, zaa. Endelea hivyo, hata wakifika 5, 6, 7 nk, idadi ya mwisho ya watoto itajileta yenyewe kulingana na hali ya wakati huo unapofikiria kuzaa mwingine.
 
mie nataka weeeeeeeeeeengi mpaka kizazi kitakapochoka chenyewe

Heeeee! umekaa sana uhindini ndo umeiga mpaka tabia zao .... maana mwanamke anazalishwa mpaka kizazi kinachoka na kuzaa taahira ambaye ndo wa mwisho kazi ipo..........................
 
Watatu me wananitosha, lakini mtarajiwa akihitaji zaidi ya hao poa tu hata kumi.
 
Heeeee! umekaa sana uhindini ndo umeiga mpaka tabia zao .... maana mwanamke anazalishwa mpaka kizazi kinachoka na kuzaa taahira ambaye ndo wa mwisho kazi ipo..........................

mungu alisema enendeni duniani mkaijaze dunia sasa kama mie nitaza kamoja au tuwili dunia itajaa lini??
 
huyo mama mimi namkubali
 
Baba utaweza kweli haya maisha bora? wale 5 ambao tayari ongeza 4 tena? mhh? unanitia wasiwasi.unataka tuanzishe timu ya mpira?

Huwezi jua tunaweza kumpata JK wetu. Si tukaze mwendo tu usiogope.
 
Watu bwana!!! tuko selfish sana!! Yaani tunapenda tu kutanua na hatutaki watoto wengi!! yaani sielewi..msomi unakuwa na mtoto 1 au wawili??

Minimum kwa wasomi iwe ni 5 na wamachinga iwe 3!

Wasomi you are not doing Justice to the future welfare of Tz!

Eti unakuta Professor mzima ana watoto wawili ..na mmachinga ana watoto 6! If this fair kwa future ya hili taifa kweli?
 
Dah wakuu mie wawili tuu, haya maisha ya kusomesha watoto st Maries Academy haya kindergatten tu mtoto analipiwa 1M na zaidi noma mtupu
 

Kuhusu suala la idadi ya watoto unaotakiwa kuwa nao,kuna factos kadhaa unazotakiwa kuzizingatia kabla hujafanya maamuzi,ila yote juu ya yote kigezo cha uchumi au hali yako ya kipato usikikiuke mana kufanya hivyo ni majuto makubwa baadae,japo kuna wanao egemea upande wa dini kuwa imewaelekeza waje ulimwenguni kuujaza,I don't know!.....kama utakua ni kiwanda (an industry) cha kufyetulia watoto wakati hujawaandalia maandalizi yoyote ki roho na ki mwili huo utakua ni uzembe ambao hao watoto wako watakuja kua ni wa kwanza kukulaani kwa akili zako hizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…