Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina Wa TANU Na Al Jamiatul Islamiyys

Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina Wa TANU Na Al Jamiatul Islamiyys

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Kuna mtu kaniuliza ni nani Iddi Faiz Mafungo?

Maswali kwangu yanakuwa mengi mno kuhusu historia ya TANU na Mwalimu Julius Nyerere kiasi naelemewa.

Muulizaji angeweza kuingia Google angemsoma lakini naona si adabu kumwelekeza huko.

Nimeamua kuweka picha ya Iddi Faiz Mafungo hapa na maelezo yake kidogo kwa faida yetu sote.

Huyo aliyesimama mkono wa kulia wa Nyerere ndiye Iddi Faiz Mafungo.

Hapo wapo uwanja wa ndege wanamsindikiza Nyerere safari ya kwanza UNO mwaka wa 1955.

Iddi Faiz alikuwa Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) na pia Mweka Hazina wa TANU.

Kwa ajili ya nafasi hizi mbili alizoshika ndiyo akachaguliwa kuwa mkusanyaji wa fedha za safari ya Nyerere UNO.
Screenshot_20201121-100902.jpg
 
Mzee heshima yako

Nauliza hakuna Wakiristo waliotenda makubwa Wakati wa harakati za kudai Uhuru wetu?

Huoni upo umuhimu wa kujaribu kubalance 'Udini' ulio nao Angalau kidogo ukaongea Habari zao?
 
Mzee heshima yako

Nauliza hakuna Wakiristo waliotenda makubwa Wakati wa harakati za kudai Uhuru wetu?

Huoni upo umuhimu wa kujaribu kubalance 'Udini' ulio nao Angalau kidogo ukaongea Habari zao?
Uzalendo,
Ikiwa ni suala la udini kuandika historia ya uhuru wa Tanganyika na kueleza mchango wa Waislam ambao ulifutwa basi udini watakuwanao hao waliowafuta Waislam katika historia hiyo.
 
Back
Top Bottom