Idhaa za Kiswahili zimejaa Watangazaji wa Kenya, ni sawa kabisa!

Idhaa za Kiswahili zimejaa Watangazaji wa Kenya, ni sawa kabisa!

SOVIET UNION

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2017
Posts
509
Reaction score
1,391
Kama watangazaji wetu ni aina ya mtu kama Kitenge, ni kwa nini Idhaa za Kiswahili zisichukue Wakenya?

Naona Maulid Kitenge anafanya project ya kutoka Kituo A kwenda kituo B na kurudi kituo A tena, sidhani kama kuna mtangazaji anawaza kutoka Local na kwenda kutangaza International.

Kwa sasa hizi Idhaa za kiswahili imejaa Wakenyanya kwa sababu inaonekana ndio wana uwezo na sishangai hata kidogo!

===

Naziona Idhaa za Kiswahili zikiwa na Wakenya kwa asilimia hadi 100 kwa sabbau sioni watangazaji wa Kitanzania wa sasa wa kuweza kufit kule.

Kama aina ya Watangazaji ndio wakina Kitenge ambao asiliamia 90 wanafanya comedy studio basi tutarajie Wakenya kujaa kwenye hizo İdhaa.

Na ni sawa kwa sababu Watangazaji wa Kikenya hata kwenye station zao wako serious na very professional, ukilinganisha na Watanzania.
 
Hao wakenya kiswahili hawajui,ni vile walau siku hizi wanajua kidogo basi wanapeana koneksheni tu,kitenge analipwa hela ndefu kuvipa umaarufu vipindi
 
Kama watangzaju wetu ni aina ya mtu kama kitengene, ni kwa nini Idhaa za kiswahili zisichukue Wakenya?

Naona Maulid Kitenge anafanya project ya kutoka Kituo A kwenda kituo B na kurudi kituo A tena, sidhani kama kuna mtangazaji anawaza kutoka Local na kwenda kutangaza International.

Kwa sasa hizi idhaa za kiswahili zimejaa Wakenyanya kwa sababu inaonekana ndio wana uwezi na sishangai hata kidogo,
Upuuzi mtupu sasa heading na content zinapingana


USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
YANI MAULID KWENDA WASAFI IMEKUWA NONGWA🤣🤣😂😂😅😅😜😜😜
 
Naziona Idhaa za Kiswahili zikiwa na Wakenya kwa asilimia hadi 100 kwa sabbau sioni watangazaji wa Kitanzania wa sasa wa kuweza kufit kule.

Kama aina ya Watangazaji ndio wakina Kitenge ambao asiliamia 90 wanafanya comedy studio basi tutarajie Wakenya kujaa kwenye hizo İdhaa.

Na ni sawa kwa sababu Watangazaji wa Kikenya hata kwenye station zao wako serious na very professional, ukilinganisha na Watanzania.
 
Mfumo mbovu unatoa watu wabovu kuanzia viongozi mpaka wanaoongozwa. Kwa mfano kenya watu wanauhuru wa kujoji mambo mengi sana kuliko kwetu sasa media nying zina watu wenye weledi shida mfumo tulionao hautakibweledi ndo maana hata wale wanaochipukia kutaka kuleta weled wanajikuta wanakosa pa kushika (rejea issue ya hando miezi kadhaa iliyopita) sasa IDHHA haziajiri jina zinaajiri mtu mwenye uweledi kqa nafasi husiika jambo ambalo ni ngum kulipata nchini kwetu mkui
 
Huku kwetu bongo, ukiwasikiliza watangazaji wetu kwenye vyombo vya habari, kwanza Wana upeo mdogo wa mambo ya kidunia, Siasa, geopolitics, uchumi,s ports

Pili hawana ujuzi wa lugha, communication skills, wengi Wanapenda story nyepesi za Zuchu, Mond, na mpira

Wenzetu wanatafuta nafasi mashirika ya kimataifa, huku kwetu watu wanajisifia kuhama Etc kwenda Wasafi, au Clouds

Screenshot_20230502-120640_2.jpg
 
Kama wale watangazaji wa kipindi cha MGAHAWA Cha wasafi fm....
wanatangaza udoko mtupu
 
Sisi wasikilizaji ndo tunatka umbea
Simba na Yanga nk ndo maana Taarifa ya habari dk 10 michezo masaa 4
 
Wasafi na efm ndo uchwara

Na wale wa EATV wa kipindi cha sport extra, wanatangaza kuwa kipindi cha michezo yote ila ukisikiliza ni simba na yanga mwanzo mwisho hakuna na ishue za maaanaa


Ni ujinga
 
Huku kwetu bongo, ukiwasikiliza watangazaji wetu kwenye vyombo vya habari, kwanza Wana upeo mdogo wa mambo ya kidunia, Siasa, geopolitics, uchumi,s ports

Pili hawana ujuzi wa lugha, communication skills, wengi Wanapenda story nyepesi za Zuchu, Mond, na mpira

Wenzetu wanatafuta nafasi mashirika ya kimataifa, huku kwetu watu wanajisifia kuhama Etc kwenda Wasafi, au Clouds
Si kukosa ufahamu tu wa msuala uliyoanisha. Hata usomaji wao ni wa hovyo sana. Ukiwasikiliza kwa mfano wasoma taarifa za habari wa ITV, unavumilia tu lakini kwa kweli mimi nilishaacha kuwasikiliza, wao ndiyo wamefanya nimepoteza hamu ya kutazama ITV, sijui ni kujifanya mabingwa wa kiswahili au nini, wanazungumza haraka haraka kama vile wamemezeshwa tape za mchiriku, wakati mwingine hata huelewi wamesema nini, hata taarifa za habari hazina mvuto kabisa. Mtu anasoma haraka haraka habari kama vile ana wasiwasi ametoka kufumaniwa.....Azam tv nako kuna kamuntu...dah ni aibu

Lakini ukiwasikiliza wasoma habari wa Kenya kwa mfano, hata kama anasoma kiswahili au kiingereza unasikiliza kwa uwazi kila neno na unafurahia kusikiliza tofauti na vyombo vyetu vya TZ, ni kama wanaajiri rappers na waimba mchiriku kuwa wasoma habari.

Radio zetu hasa binafsi ndiyo bure kabisa....hawana ajenda ni umbea na udaku tu
 
Kituo pekee nilichobaki naangalia taarifa ya habari ni UTV TENA akitangaza ivona kamuntu au baruan muhuza ndio haswaaa wanakuwa wamenikosha.
Kongole Kwa Azam TV .
TBC Wana program nzuri Ila manjonjo yamekuwa mengi Hadi yanakera yaani kwenye chumba cha habari wanaweza Hadi jiko, ubunifu ukizidi unakuwa ni uchafu.
Hivyo vingine vilivyobaki ndo huwa hata siangalii.
 
Hata vyeo vya udc na u-RC vingekuwa vinafanyiwa usaili na waombe raia wa Kenya,Rwanda na Uganda watanzania wasingepata tumechezea mno elimu!!
 
Back
Top Bottom