Msela Wa Kitaa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2021
- 1,396
- 2,704
Kisiwa cha Idjwi nchini Kongo ni eneo lililosahaulika ambalo limeishi kwa miongo kadhaa ya vita bila kuathirika.
Kisiwa cha pili kwa ukubwa kilichoko ziwani barani Afrika, Idjwi, kipo katika sehemu ya kusini ya Ziwa Kivu, kikizungukwa na nchi mbili ambazo zimekuwa katika vita kwa karibu miongo mitatu: DRC na Rwanda.
"Hatuna wanajeshi hapa, kutoka upande wowote. Hatujawahi kusikia milio ya bunduki au mabomu, lakini tunahisi athari za vita," anasema Yves Minani, mjasiriamali na mkurugenzi wa kituo cha redio cha ndani.
Maisha kwenye Idjwi yanaelezwa kuwa ya amani, na mazuri. Ni tofauti kabisa na sehemu za bara ambako waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wameteka miji miwili mikuu ya mkoa, Goma na Bukavu.
"Tangu mwanzo hapa, hakujawahi kuwa na vita," anasema Mustafa Mamboleo, msimamizi wa eneo la Idjwi na afisa wa Kivu Kusini.
"Lakini hofu inaenea miongoni mwa wakazi kwani kufungwa kwa benki na mizozo sehemu za bara kunamaanisha bidhaa muhimu pia hazitufikii."
Kisiwa hicho ni makazi ya watu wapatao 300,000: Wengi wao, wahavu, wameishi hapa kwa miongo kadhaa.
Hakuna umeme au maji ya bomba na huduma za afya ni ngumu kupatikana. Hata hivyo, watu wanaokimbia vita katika Mashariki ya DRC wanaona ni mahali salama.
Chanzo cha picha, AFP
Maelezo ya picha, kuna huduma chache kwa wakazi 300,000 wa Idjwi
Kufuatia mapigano makali katika mji mkuu wa Kivu Kaskazini, Goma, na maendeleo yasiyo ya kawaida ya waasi wa M23 katika mkoa wa Kivu Kusini, makumi ya maelfu ya Wakongo waliokimbia makazi yao wamekimbilia Idjwi.
Sasa wanalala katika kambi za wakimbizi zisizo rasmi kaskazini mwa kisiwa hicho, wakitegemea tu ukarimu wa wenyeji kwa msaada.
Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, kuna angalau watu 42,000 wanaoishi katika kambi za muda, lakini hakuna rekodi rasmi kwa wale waliokolewa na familia za wenyeji. Wenyeji wanakadiria kuwa kunaweza kuwa na wakimbizi wengi kama 60,000 wanaoishi Idjwi.
"Hukuna kaya hapa ambayo haijammpokea mwanafamilia, rafiki, au jamaa wa mbali aliyekimbia vita," anasema Yves Minani.
Vituo vya wakimbizi vimeanzishwa katika makanisa, shule na majengo yaliyotelekezwa. Mbali na jenereta chache, hakuna umeme au maji ya bomba.
Kuna hospitali kuu moja tu, na kuna magari machache tu, mara nyingi haiwezekani kwa wale walio katika maeneo ya mbali kupata matibabu.
"Wakati mwingine tunalazimika kutembea kilomita 10 na mgonjwa kwenye machela," anasema Yves. "Wakati mwingine wanakufa njiani kwa sababu hatuwezi kufika kwa haraka vya kutosha."
Licha ya kuwa na rasilimali chache, hii sio mara ya kwanza kwa wakaazi wa kisiwa hicho kufungua milango yao kwa wale watu wenye shida. Katika miaka ya 1990, wimbi la wakimbizi wa Rwanda lilifika Idjwi kukimbia maafa ya mauaji ya kimbari nyumbani kwao.
"Hiyo ndiyo Idjwi, hatuna makubwa watu, lakini tunakaribisha," anasema Yves.
Wakati wa Vita vya Kwanza na vya Pili vya Kongo vilivyoharibu eneo hilo katika miaka ya 1990, pia vinajulikana kama Vita vya Dunia vya Afrika, Idjwi ilikuwa sehemu salama.
Wenyeji wanasema mfululizo wa mazungumzo na vikundi vya waasi na vikosi vya jeshi viliwazuia kuingia kwenye mzozo.
"Tulisikia tu kuhusu vita kwenye redio au mara kwa mara wakati sauti ilivuka ziwa," anasema Yves.
Biashara kati ya kisiwa hiki na Rwanda ni ya muda mrefu sana," anasema Padri Adrien Cishugi, ambaye ana nyumba kisiwani na anatumia muda mwingi huko kusaidia jamii ya Wapigmi.
Anasema kwamba katika baadhi ya sehemu za kisiwa, hasa kusini, watu hutumia zaidi faranga ya Rwanda kuliko faranga ya Kongo kwa sababu biashara yote inafanywa na Rwanda.
Kuna safari za mara kwa mara zinazounganisha miji ya Goma na Bukavu na Idjwi, na safari inachukua saa mbili hadi tatu.
Mwishoni mwa Januari, mapigano kati ya M23 na jeshi la Kongo yalisimamisha safari hizi, na kukinyonga kisiwa.
"Bila boti, maisha hayapo hapa," anasema PadreiAdrien Cishugi.
Bandari ya Goma ilipofungwa Januari baada ya wanajeshi wa M23 kuuteka mji, safari zote za boti zilisimamishwa. Lakini "walifanya msamaha maalumu kwa kisiwa kwa sababu kilikuwa matatizoni," anasema Padri Adrien.
Kisiwa cha pili kwa ukubwa kilichoko ziwani barani Afrika, Idjwi, kipo katika sehemu ya kusini ya Ziwa Kivu, kikizungukwa na nchi mbili ambazo zimekuwa katika vita kwa karibu miongo mitatu: DRC na Rwanda.
"Hatuna wanajeshi hapa, kutoka upande wowote. Hatujawahi kusikia milio ya bunduki au mabomu, lakini tunahisi athari za vita," anasema Yves Minani, mjasiriamali na mkurugenzi wa kituo cha redio cha ndani.
Maisha kwenye Idjwi yanaelezwa kuwa ya amani, na mazuri. Ni tofauti kabisa na sehemu za bara ambako waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wameteka miji miwili mikuu ya mkoa, Goma na Bukavu.
"Tangu mwanzo hapa, hakujawahi kuwa na vita," anasema Mustafa Mamboleo, msimamizi wa eneo la Idjwi na afisa wa Kivu Kusini.
"Lakini hofu inaenea miongoni mwa wakazi kwani kufungwa kwa benki na mizozo sehemu za bara kunamaanisha bidhaa muhimu pia hazitufikii."
Kisiwa hicho ni makazi ya watu wapatao 300,000: Wengi wao, wahavu, wameishi hapa kwa miongo kadhaa.
Hakuna umeme au maji ya bomba na huduma za afya ni ngumu kupatikana. Hata hivyo, watu wanaokimbia vita katika Mashariki ya DRC wanaona ni mahali salama.
Chanzo cha picha, AFP
Maelezo ya picha, kuna huduma chache kwa wakazi 300,000 wa Idjwi
Kufuatia mapigano makali katika mji mkuu wa Kivu Kaskazini, Goma, na maendeleo yasiyo ya kawaida ya waasi wa M23 katika mkoa wa Kivu Kusini, makumi ya maelfu ya Wakongo waliokimbia makazi yao wamekimbilia Idjwi.
Sasa wanalala katika kambi za wakimbizi zisizo rasmi kaskazini mwa kisiwa hicho, wakitegemea tu ukarimu wa wenyeji kwa msaada.
Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, kuna angalau watu 42,000 wanaoishi katika kambi za muda, lakini hakuna rekodi rasmi kwa wale waliokolewa na familia za wenyeji. Wenyeji wanakadiria kuwa kunaweza kuwa na wakimbizi wengi kama 60,000 wanaoishi Idjwi.
"Hukuna kaya hapa ambayo haijammpokea mwanafamilia, rafiki, au jamaa wa mbali aliyekimbia vita," anasema Yves Minani.
Vituo vya wakimbizi vimeanzishwa katika makanisa, shule na majengo yaliyotelekezwa. Mbali na jenereta chache, hakuna umeme au maji ya bomba.
Kuna hospitali kuu moja tu, na kuna magari machache tu, mara nyingi haiwezekani kwa wale walio katika maeneo ya mbali kupata matibabu.
"Wakati mwingine tunalazimika kutembea kilomita 10 na mgonjwa kwenye machela," anasema Yves. "Wakati mwingine wanakufa njiani kwa sababu hatuwezi kufika kwa haraka vya kutosha."
Licha ya kuwa na rasilimali chache, hii sio mara ya kwanza kwa wakaazi wa kisiwa hicho kufungua milango yao kwa wale watu wenye shida. Katika miaka ya 1990, wimbi la wakimbizi wa Rwanda lilifika Idjwi kukimbia maafa ya mauaji ya kimbari nyumbani kwao.
"Hiyo ndiyo Idjwi, hatuna makubwa watu, lakini tunakaribisha," anasema Yves.
Wakati wa Vita vya Kwanza na vya Pili vya Kongo vilivyoharibu eneo hilo katika miaka ya 1990, pia vinajulikana kama Vita vya Dunia vya Afrika, Idjwi ilikuwa sehemu salama.
Wenyeji wanasema mfululizo wa mazungumzo na vikundi vya waasi na vikosi vya jeshi viliwazuia kuingia kwenye mzozo.
"Tulisikia tu kuhusu vita kwenye redio au mara kwa mara wakati sauti ilivuka ziwa," anasema Yves.
Biashara kati ya kisiwa hiki na Rwanda ni ya muda mrefu sana," anasema Padri Adrien Cishugi, ambaye ana nyumba kisiwani na anatumia muda mwingi huko kusaidia jamii ya Wapigmi.
Anasema kwamba katika baadhi ya sehemu za kisiwa, hasa kusini, watu hutumia zaidi faranga ya Rwanda kuliko faranga ya Kongo kwa sababu biashara yote inafanywa na Rwanda.
Kuna safari za mara kwa mara zinazounganisha miji ya Goma na Bukavu na Idjwi, na safari inachukua saa mbili hadi tatu.
Mwishoni mwa Januari, mapigano kati ya M23 na jeshi la Kongo yalisimamisha safari hizi, na kukinyonga kisiwa.
"Bila boti, maisha hayapo hapa," anasema PadreiAdrien Cishugi.
Bandari ya Goma ilipofungwa Januari baada ya wanajeshi wa M23 kuuteka mji, safari zote za boti zilisimamishwa. Lakini "walifanya msamaha maalumu kwa kisiwa kwa sababu kilikuwa matatizoni," anasema Padri Adrien.