Idris Gueye agoma kuomba radhi kwa kutokuunga mkono LGBTQ+

Idris Gueye agoma kuomba radhi kwa kutokuunga mkono LGBTQ+

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1653283632955.png

๐—œ๐—ฑ๐—ฟ๐—ถ๐˜€๐˜€๐—ฎ ๐—š๐˜‚๐—ฒ๐˜†๐—ฒ ni mchezaji wa klabu ya mpira wa miguu ya Paris Saint Germain (PSG) aliyekataa kuvaa jezi ya timu yake ambayo kwa upande wa namba ilikuwa imeandikwa rangi zenye kuashiria mahusiano haramu ya jinsia moja na watu waliobadili jinsia kwa pamoja wanajitambulisha kama LGBT+.

Hivi karibuni ametoa kauli kufuatia sakata lake hilo la kuonekana kwamba anadharau alama hiyo na kuikataa kabisa akisema: "Nipo tayari kuondoka Ufaransa (na kuachana na klabu ya PSG) ila sitaomba radhi (wala kutaka msamaha). Nafahamu misingi ya Imani yangu, sihofii kupoteza Mkataba au Umaarufu wangu hapa Ulaya, nipo tayari kurudi nyumbani (Afrika)".

Hayo yamekuja baada ya shirikisho la mpira wa miguu nchini Ufaransa kumtaka aombe radhi kwa kitendo hiko cha kiimani alichokifanya.

PIA SOMA
- Akacha mechi kwasababu hataki kuunga mkono vitendo vya kishoga
 
Embu acha ujinga kijan kula mshara zepa zako Africa Ni tabu tupu hkn tulijualo

Piga mshahara wako ukimliza mkataba tafuta klbu nyingine misisimmo ya kiafrica Ni ubatili na umasikini tu kuzanya hell kjn ujaanza wew Kuchukizwa na tabia za ushoga lkn hkn namna utaikwepa kwa sas HV Ni Bora utulie kimy unadhani mesi yey anapenda hvyo vitu au Ni mfumo tu umempelekea yey kukubli tu
 
Sidhani kauli ya kuunga mkono ni sahihi. Nadhani lingetumika neno kutambua/kuwatambua wapo. Maana ni kweli wapo. Mimi sioni shida kama tukitambua kuwa wapo.
Kukataa kuvaa hakuondoi wala hakubadilishi kuwa hawapo. Wapo.
 
Anasimamia msimamo wa dini ya kuletewa..halafu walio mletea dini ndio ma ceo wa hiyo timu...na wao wanaunga mkono.

Aje tule michembe afrika.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom