Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kitongoji cha Madiga, Kijiji cha Darajani, Kata ya Kipatimu, Jimbo la Kilwa Kaskazini, Mkoa wa Lindi, Katibu Mkuu Kiongozi wa Baraza Kivuli la Mawaziri la ACT Wazalendo, Idrisa Kweweta amewataka Wananchi kuikataa CCM kwa vitendo.
"Jimbo zima la Kilwa Kaskazini wamebakisha wagombea tisa (9) tu kati ya wagombea 34 wa vijiji na wajumbe wasiozidi 40 kati ya 600. Nyinyi mliobaki lazima mtume salam kwamba CCM haitakiwi, wachagueni viongozi wetu wachache waliobaki. Ikataeni CCM." amesema Idrisa.