mahunduhamza
Member
- Aug 25, 2021
- 19
- 46
CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Taifa la Ethiopia limekaribisha mwaka mpya hivi karibuni, licha ya kuwepo kwa baadhi ya madhila ya vita na njaa hasa upande wa mashariki wa taifa hili. Fahamu zaidi kuhusu kalenda ya mwaka wa kipekee wa Ethiopia kama urithi wa nchi hiyo.
1) Mwaka ambao una miezi 13
Sio jambo hilo tu la miezi, mwaka huu wa Ethiopia upo miaka saba nyuma na miezi nane ukilinganishwa na kalenda inayotumika ulimwenguni, Jumamosi mwezi huu waliukaribisha mwaka 2014.
Hii inatokana na kwamba wanahesabu mwaka aliozaliwa Yesu kristu tofauti, Kanisa katoliki lilipokuwa limefanyia marekebisho mwaka wa kuzaliwa kristo miaka ya 500 AD, Kanisa la Orthodox halikufanya marekebisha upande wao.
CHANZO CHA PICHA,AFP
Mwaka wao mpya huadhimishwa kila ifikapo Septemba 11 na siku nyingine huangukia tarehe 12 mwezi huo huo.
Tofauti na watoto wanaokua mahali pengine duniani, kuna haja pia kwa vijana wa Ethiopia kujifunza kuwa kuna siku ngapi katika mwezi.
Kwa upande wa Ethiopia ni rahisi, katika miezi 12 kuna siku 30 kila mwezi na mwezi wa 13- Mwezi wa mwisho ukiwa na siku tano mpaka saba tu inategemea zaidi na inapoangukia.