Ifahamu sumu kuvu (mycotoxins)

Ifahamu sumu kuvu (mycotoxins)

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Kwa mujibu wa Shirika la Afya pamoja na Shirika la chakula na Kilimo Duniani (2018) wanaitafsiri sumu kuvu kuwa ni aina ya ukungu unaojitokeza kwenye nafaka kutokana na kuvu (fungi) jamii ya Aspergillus, Fusarium na Penicillium.

Sumu kuvu "mycotoxins" huweza kuzaliwa kwenye nafaka, matunda yaliyokaushwa na vingo(spices). Sumu hii huweza kupenda hata katika sehemu za ndani kabisa za nafaka iliyoathiriwa na kuvu.

Madhara ya sumu kuvu "mycotoxins" ni pamoja na :kuua(sumu), kudhohofisha kinga ya mwili, na saratani. Sumu hii ina madhara pia kwa wanyama.

Zipo namna nyingi za kuepukana na sumu kuvu miongoni mwa njia ni pamoja na uchambuaji mzuri wa nafaka kwa kuhakikisha nafaka zilizoathiriwa na kuvu hazichanganyiki na nafaka nzima na jambo la muhimu zaidi ni uhifadhi mzuri wa nafaka.

Tanbihi: Hii kwa wakulima wenzangu huwa tunaiona sana unaweza ukawa shahidi wa hili.

download.jpeg
download (1).jpeg
download (6).jpeg
download (8).jpeg
Screenshot_20210307-215952_Chrome.jpg
 
Safi mleta mada swali langu hv hatuwezi kupata mashine inayoweza kubagua ama kutenga nafaka zilizoathirika na hiyo sumu!!??
 
Inawezekana ila tukiwa "proactive" tukichukua tahadhari mapema lakini tukichekewa tatizo huwa kubwa zaidi kwa sababu sumu hii hupenya hadi sehemu za ndani za nafaka na huenda kwa kasi.
Safi mleta mada swali langu hv hatuwezi kupata mashine inayoweza kubagua ama kutenga nafaka zilizoathirika na hiyo sumu!!??
 
Kuna mahali nimeona watu wanajadili kuwa mahindi yamehifadhiwa kwa kutumia sumu. Uzi huu natamani uwe sehemu ya kuhamasisha uelewa zaidi juu ya suala la sumu kuvu.
 
Mkuu basi hata ungeweka kapicha kanako onyesha tofauti kati ya mbegu yenye kuvu- sumu (mycotoxin) na mbegu ambayo haina hiyo kuvu-sumu.
 
Ah..ah...ina madhara makubwa sana hiyo Mkuu.

Ya haraka ni sumu inaua ila ya taratibu ni kuharibu kinga ya mwili na saratani.

Wale wapeenzi wa udaga tuwasiliane.
Wala dona ndio wahanga wakubwa wa hili janga.
Dokita Ndodi Mungu anakuona kwa upotoshaji wako.
 
Mkoa wa Mara wanaongoza kwa kutumia ugali wa dona.

Afya zao ziko hatarini.
 
Hii ndiyo motives ya uzi
 

Attachments

  • Screenshot_20210306-223546_Chrome.jpg
    Screenshot_20210306-223546_Chrome.jpg
    120.3 KB · Views: 4
Asilimia kubwa ya wabongo wanaweza wasiwe exposed kwenye kiwango kikubwa cha aflatoxin na aina nyingine za sumu kuvu kutokana na kula ugali wa sembe, kukoboa mahindi kunapunguza sumu kuvu kwa kiwango kikubwa sana. Kwa wale wanaopenda dona, ni bora ukaandaa mahindi yako mwenyewe, ukaaondoa yale mahindi mabovu, ukaosha na kuanika kabla ya kwenda kusaga.

Kwa sababu karanga zinaweza kuwa na kiwango kikubwa cha aflatoxin, inafaa kuzichambua na kuondoa zile mbovu na zilizosinyaa. Kwa wale wanaoandaa unga kwa ajili ya watoto wawe makini zaidi kuchambua mahindi na karanga kwa ajili ya kusaga unga kwa ajili ya uji wa mtoto, nafikiri tumeelewana ndugu zanguni....
 
Kuna swali najiuliza hapa naomba kusaidiwa.
Je hii sumu kuvu ipo tangu lini? kama ipo tangu zamani je madhara yake hayakugunduliwa tangu zamani au ndo watu walikua wanakufa bila taarifa? au madhara yake yamekuzwa kipindi hiki cha dot com? maana imeanza kutiliwa mkazo sana miaka ya karibuni hapa...au mabeberu wanatumia sumu kuvu kututishatisha kama ilivyo koona? maana mababu na mabibi zetu walipiga sana dona kabla ya mashine za kukoboa kuwasili nchini kwetu....nadhani naweza kupata majibu kwa wenye uelewa juu ya suala hili la sumu kuvu...shukran
 
Kuna swali najiuliza hapa naomba kusaidiwa.
Je hii sumu kuvu ipo tangu lini? kama ipo tangu zamani je madhara yake hayakugunduliwa tangu zamani au ndo watu walikua wanakufa bila taarifa? au madhara yake yamekuzwa kipindi hiki cha dot com? maana imeanza kutiliwa mkazo sana miaka ya karibuni hapa...au mabeberu wanatumia sumu kuvu kututishatisha kama ilivyo koona? maana mababu na mabibi zetu walipiga sana dona kabla ya mashine za kukoboa kuwasili nchini kwetu....nadhani naweza kupata majibu kwa wenye uelewa juu ya suala hili la sumu kuvu...shukran
Utafiti kuhusu sumu kuvu hasa aina ya aflatoxin ulianza kushika kasi miaka ya 1960 baada ya kutokea mlipuko wa vifo vya bata mzinga (turkeys) huko nchi za ulaya baada ya kupewa vyakula vyenye aflatoxin ambavyo baadaye iligundulika vilitengenezwa na karanga kutoka Brazil, na huo ugonjwa kujulikana kama Turkey X Disease...mabadiliko ya tabia nchi huweza kusababisha kuongezeka na kusambaa kwa fungus na wadudu wanaoshambulia mazao na pia ukame ambao huweza kuathiri mazao kuhimili kupambana na wadudu waharibifu na fungasi wanaozalisha aflatoxin kwenye mazao..
 
Utafiti kuhusu sumu kuvu hasa aina ya aflatoxin ulianza kushika kasi miaka ya 1960 baada ya kutokea mlipuko wa vifo vya bata mzinga (turkeys) huko nchi za ulaya baada ya kupewa vyakula vyenye aflatoxin ambavyo baadaye iligundulika vilitengenezwa na karanga kutoka Brazil, na huo ugonjwa kujulikana kama Turkey X Disease...mabadiliko ya tabia nchi huweza kusababisha kuongezeka na kusambaa kwa fungus na wadudu wanaoshambulia mazao na pia ukame ambao huweza kuathiri mazao kuhimili kupambana na wadudu waharibifu na fungasi wanaozalisha aflatoxin kwenye mazao..
Shukran mkuu
 
Back
Top Bottom