Ifike muda wahitimu wa vyuo waliokopeshwa na Serikali kusoma, walipe deni bila riba

Ifike muda wahitimu wa vyuo waliokopeshwa na Serikali kusoma, walipe deni bila riba

uchumi2018

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2018
Posts
1,657
Reaction score
2,406
Habari zenu wana jamvi.

Kwa muda mrefu sasa nimeangalia wahitimu wa vyuo mbalimbali waliofanikiwa kupata ajira na ambao bado wanalazimika kulipa mikopo waliyokopeshwa na serikali ili kufikia ndoto zao za elimu. Jambo ambalo mimi binafsi naliona ni jema kwa kuwa wanafanya mfuko huo uweze kuishi ili uwasaidie na wengine.

Kitu kinachoshangaza ni pale ambapo wanatakiwa kutoa na riba kwa kiasi cha fedha ambacho bado hakijalipwa.
Pendekezo langu kwa serikali ni kwamba,kwa kuwa huyu mhitimu analipa kodi kutoka kwenye mshahara wake basi asilazimike kulipa riba alipe kiasi alichokopeshwa tu,ikiwa na maana kwamba serikali kwa kumsomesha imepanua wigo wa walipakodi na hivyo kuongeza mapato.

Jambo hilo litampatia unafuu wa maisha mhusika ukitilia maanani ndo kwanza ameanza maisha.

Kupitia hizo kodi zinazokusanywa,serikali iwe inajazia (inflation rates) kwenye mfuko wa bodi ya elimu badala ya mzigo huo kuelekezwa kwa mwajiriwa huyu mpya.

Kwa maoni yangu jambo hili litaongeza ufanisi kazini,kwa wahusika kufanya kazi bila msongo wa mawazo na pia kuepusha tamaa za rushwa zinazochochewa na kipato kutokidhi mahitaji ya mhusika.

Nawasilisha.
 
Unaambiwa hilo deni halilipiki
Mkuu mbona wengi wanalipa kupitia waajiri wao? unakatwa juu kwa juu
sema kwa sababu ya hiyo riba unakuta deni haliishi,maana linazaliana
 
Serikali inatafuta njia mpya za kuongeza mapato wewe unataka kuipunguzia mapato
 
Sheria zao wenyewe zinawafunga wenyewe ,kulipa deni la mkopo wa elimu ya juu ni ngumu ,elimu yenyewe haituruhusu kujiajiri naona baada ya kumaliza form 6,vijana wakopeshwe iyo fedha kama mtaji tofauti na elimu inayomfanya mhitimu kuwa mtumwa huku hana hata Baki ya mia mbovu mfukoni
 
Serikali inatafuta njia mpya za kuongeza mapato wewe unataka kuipunguzia mapato
Mkuu nimependekeza namna nzuri ya kuongeza pato. Unapomkamua ng'ombe kwenye mazingira rafiki
unapata maziwa mengi zaidi.
 
Acheni ubinafsi, hiyo riba ndio inaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo. Na serikali inakata kiasi cha asilimia 15 tu pale utakapoanza kupokea mshahara.
 
Acheni ubinafsi, hiyo riba ndio inaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo. Na serikali inakata kiasi cha asilimia 15 tu pale utakapoanza kupokea mshahara.
Wanufaika wa mikopo wataongezeka tuu kupitia kodi inayolipwa na wanufaika wa zamani.
Kumbuka sijasema wasilipe deni bali nimesema wasilipe riba.
Itakuwa inavunja moyo kuwa na wasomi mtaani wenye 'take home" za laki tatu baada ya makato yote
wakati muuza genge anaingiza zaidi ya hiyo kwa mwezi.
 
Serikali ipo kwa ajili ya kukusanya kodi na kuyafikia malengo...

Hata ukilipa kodi mara mbili mbili wao haiwahusu... serikali sikivu...




Cc: mahondaw
 
Wanufaika wa mikopo wataongezeka tuu kupitia kodi inayolipwa na wanufaika wa zamani.
Kumbuka sijasema wasilipe deni bali nimesema wasilipe riba.
Itakuwa inavunja moyo kuwa na wasomi mtaani wenye 'take home" za laki tatu baada ya makato yote
wakati muuza genge anaingiza zaidi ya hiyo kwa mwezi.
Kuna kigezo gan ulicho2mia wew kumnyanyua mhitimu juu kimapato na kumshusha chini muuza nyanya mkuu ifike sehemu jamii ibadili mentallity yake juu ya kisomo mi naanza na wew niliyesoma mlengo wako badilika acha mtizamo huo aliyekupeleka shule alikuambia kuwa ukimaliza shule umemaliza maisha na changamoto? Halafu unalalamikia vitu vyepesi kumbuka kuna wa2 hawakupata nafas ya kusoma hata kuufikia huo mkopo na tupo hapa tunafanya maisha yanaenda na kuwasaidia wahitimu jinsi ya kucope na maisha, ndio tumeishia la saba je unatuhukumu kuwa tusiingize kipato kikubwa regarding na elimu zetu? Acha hizo mhitimu apambane alipe na riba kwasababu mzazi alisaidiwa kama ni kodi tunalipa wote hata ambao hatukuchukua mikopo hakuna kufuta riba eti kwa kisingizio cha kulipa kodi
 
Back
Top Bottom