change formula
JF-Expert Member
- Sep 8, 2020
- 729
- 1,559
Kwanza niipongeze TFF hii ya Wallace Karia, imefanya kazi kubwa sana licha ya mapungufu yaliyojitokeza katika uongozi wake ambayo ni machache na yanatokea kutokana na uelewa finyu wa watanzania walio wengi kuhusu mpira wa miguu na wengi kuendekeza ushabiki wa u-Simba na u-Yanga.
Kutokana na ligi kuu ya Tanzania kuzidi kukua na kuvuta mashabiki kutoka pande zote za jamhuri ya muungano wa Tanzania, mimi kama mdau wa michezo na mtaalamu wa masuala ya pesa na uwekezaji, napendekeza mambo yafuatayo.
Moja Tff ibadilishe kanuni za usajili ili timu zenye uwezo ziruhusiwe kusajili idadi zaidi ya kumi ya wachezaji wa kigeni ili kuongeza ushindani katika ligi yetu.
Itazisaidia timu zinazocheza mashindano ya kimataifa ziweze kufika mbali zaidi na kuitangaza nchi yetu, pia zitapata pesa nyingi ambazo zitasaidia kuboresha timu na hata wawekezaji kupata faida.
Pili kama hilo haliwezekani basi wachezaji wanaotoka E.A community wasiesabiwe kama wageni, hii itasaidia wachezaji wa nchi za Africa Mashariki kuja kwa wingi kwenye ligi yetu na ligi yetu itatangazika na kutazamwa zaidi kwenye nchi za afrika Mashariki.
Najua wapo watu wanasema wachezaji wa kigeni wakiwa wengi tutakosa wachezaji wa timu ya Taifa na Taifa stars itakuwa dhaifu!!! Hoja hii haina mashiko, wachezaji wa kigeni wakiwa wengi hii itasaidia wachezaji wazawa kujitambua na kujituma zaidi ili wafanye vizuri na kupata number na hii itakuwa ndio njia nzuri ya kuwajengea confidence ya kupambana na watu kutoka mataifa mbalimbali, wakizoea watafanya vizuri na timu ya taifa itafanya vizuri pia.
Kutokana na ligi kuu ya Tanzania kuzidi kukua na kuvuta mashabiki kutoka pande zote za jamhuri ya muungano wa Tanzania, mimi kama mdau wa michezo na mtaalamu wa masuala ya pesa na uwekezaji, napendekeza mambo yafuatayo.
Moja Tff ibadilishe kanuni za usajili ili timu zenye uwezo ziruhusiwe kusajili idadi zaidi ya kumi ya wachezaji wa kigeni ili kuongeza ushindani katika ligi yetu.
Itazisaidia timu zinazocheza mashindano ya kimataifa ziweze kufika mbali zaidi na kuitangaza nchi yetu, pia zitapata pesa nyingi ambazo zitasaidia kuboresha timu na hata wawekezaji kupata faida.
Pili kama hilo haliwezekani basi wachezaji wanaotoka E.A community wasiesabiwe kama wageni, hii itasaidia wachezaji wa nchi za Africa Mashariki kuja kwa wingi kwenye ligi yetu na ligi yetu itatangazika na kutazamwa zaidi kwenye nchi za afrika Mashariki.
Najua wapo watu wanasema wachezaji wa kigeni wakiwa wengi tutakosa wachezaji wa timu ya Taifa na Taifa stars itakuwa dhaifu!!! Hoja hii haina mashiko, wachezaji wa kigeni wakiwa wengi hii itasaidia wachezaji wazawa kujitambua na kujituma zaidi ili wafanye vizuri na kupata number na hii itakuwa ndio njia nzuri ya kuwajengea confidence ya kupambana na watu kutoka mataifa mbalimbali, wakizoea watafanya vizuri na timu ya taifa itafanya vizuri pia.