IGP Camillus Wambura afanya mabadiliko kwa wakuu wa kikosi cha Usalama barabarani

IGP Camillus Wambura afanya mabadiliko kwa wakuu wa kikosi cha Usalama barabarani

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Jeshi la Polisi Tanzania chini ya IGP Wambura limetangaza mabadiliko madogo kwenye safu za uongozi wa Kikosi cha Usalama Barabarani. Katika mabadiliko hayo:


polisi.tanzania_1734876233067(1).jpeg

  • Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ramadhani Ng’anzi amehamishwa kutoka Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania kwenda Makao Makuu ya Upelelezi Dodoma. Atakuwa Mkuu wa Kitengo cha Makosa ya Maadili ya Jamii.

  • Nafasi yake sasa inachukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) William Mkonda, aliyekuwa Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda Maalum ya Dar es Salaam.

  • Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Boniphace Mbao, aliyekuwa Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma, amehamishiwa Dar es Salaam kuchukua nafasi ya Mkonda kama Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda Maalum ya Dar es Salaam.

  • ACP Michael Deleli, aliyekuwa Mkuu wa Elimu kwa Umma wa Kikosi cha Usalama Barabarani, amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi Dodoma na sasa atakuwa Kaimu Mkuu wa Maadhimisho ya Kitaifa.

  • ACP Nassoro Sisiwa, aliyekuwa Mkuu wa Operesheni za Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, amehamishiwa Mkoa wa Kilimanjaro kama Mkuu wa Usalama Barabarani wa Mkoa huo.
 
Mimi namuomba tu Afande IGP kama ikimpendeza, awapunguze pia askari wake wa usalama barabarani. Maana wametugeuza madereva na wamiliki wa vyombo vya moto hususani magari; kuwa ng'ombe wao wa maziwa!

Kiufupi hao vijana wake waliotapakaa barabarani kote nchini, wanatuvizia na kututafutia makosa mpaka inakuwa ni kero sasa.
 
Inasaidia nini kwenye kuzuia uonevu barabarani?

Au ni issue za wao kupeleka gawiwo linalotarajiwa na wakubwa?
 
Mkuu wa Operation wa Jeshi akikukataa, umeisha, yeye anaongea moja kwa moja, hivi RPC Mbeya alibaki? -Awadhi
 
Mimi namuomba tu Afande IGP kama ikimpendeza, awapunguze pia askari wake wa usalama barabarani. Maana wametugeuza madereva na wamiliki wa vyombo vya moto hususani magari; kuwa ng'ombe wao wa maziwa!

Kiufupi hao vijana wake waliotapakaa barabarani kote nchini, wanatuvizia na kututafutia makosa mpaka inakuwa ni kero sasa.
Traffic siku hizi wana saccos zao kila week 200,000.

Kufikia hicho kiwango sisi raia wanyonge tunaomiliki Vitz tunateseka sana.
 
kAMANDA GP
Naomba sana kutoa ushauri kwako najua unajua kero hii au hukutani nayo kwa sababu unatumia ridders na road clearance.
"KUNA KERO KUBWA SANA KWA VYOMBO HIVYO
1. kUTOFUATA SHERIA ZA USALAMA BARABARNI NA SASA IMEKUWA MAZOEA
2. Hawavai helmets
3.Kupakia mishikaki abiria zaidi ya mmoja kisheria
4.Mbaya kuliko yote ni kupita kushoto na kuhatarisha usalama barabarani esp Mko wa Dar es Salaam ajali na vofo ni vingi mno MTU UNAKWEPA NTU NA KURUDI KWAKO KUSHOTO UNAKUTA BODA BODA HUKU ANAKUOVATAKE GAFRA UNAMGONGA
5. Bodaboda wana groups za whattsap na hupost mara moja na wanakuja wengi na kufanya fujo hivyo kwa usalama hata ajali ikitokea bora kukumbia ...kwa usalama.
MAONI
1. Kuwepo na elimu kwa umma kuhusu hatari yahayo wayafanyayo.
2.Kuwepo na operation endelevu kuhakikisha hili linakoma.
3. Askari wa usalama barabarani wawe ethical..
4. Tujifunze kwa majirani RWANDA nk wamewezaje eneo hilo
5. Wavae uniform maalum jackets amabazo zina reflectors muundo tofauti na wa POLICE.
6. HILI LINAWEZEKANA HALIITAJI FEDH ZA KIGENI NA DEVELOPING PARTNERS
7. MWISHO VINGOLA KWA MAGARI MAKUBWA IMEKUWA FASHION NA HATAWASIOHUSIKA
8. Magari ya UMMA ST...SU...POLICE ...MAGEREZA NK YANAONGOZA KUKIUKA SHERIA NA HAKUNA HATUA ZA MAKUSUDI.
9.Mh IGP TUNAOMBA SANA SANA UKIWEZA HILI PAMOJA NA MENGI MENGINE UTAACHA LEGACY.
 
Back
Top Bottom