IGP Sirro anapopingana na Dhana ya Ulinzi Shirikishi

IGP Sirro anapopingana na Dhana ya Ulinzi Shirikishi

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kamanda Sirro amekuwa akijinasibu kuhamasisha watu na ulinzi shirikishi. Sirro amekuwa akihimiza kuwa:

"ushirikishwaji watu katika maeneo yao ndiyo njia pekee ya kuumaliza kabisa uhalifu katika maeneo husika."

Kamanda Sirro amekuwa akieleza zaidi kuwa, wahalifu wote wanajulikana katika jamii zao na hata wanafanya nini kwenye uhalifu wao. Kwamba mashirikiano ya karibu baina ya polisi na jamii yatamaliza kabisa uhalifu.

Kisa cha mauaji ya wafanya biashara wa madini wakazi wa Ifakara kwenye kesi maarufu ya Zombe kinayathibitisha maneno mazito haya ya kamanda huyu.

Kwenye kesi hiyo, Rais Kikwete alilazimika kuunda tume ya uchunguzi baada ya wananchi kuikataa ripoti ya polisi kuwa marehemu walikuwa ni majambazi.

Kwa upande wao, jamii ya wananchi waliokuwa wakiishi na marehemu hao (Ifakara na Dar es Salaam) waliikataa katakata taarifa hiyo ya polisi. Tume ya uchunguzi iliuthibitisha ukweli huo wa wananchi dhidi ya uongo, ubambikiziaji kesi, ufedhuli, uuwaji, ujambazi nk wa polisi.

Kamanda Sirro, wananchi tuliokuwa tukiishi na mheshimiwa Mbowe mitaani tunamfahamu. Mbowe anafahamika vyema na majirani zake.

Tambua kuwa katika maneno yako dhidi ya Mbowe na maneno ya Mbowe dhidi yako, Mbowe anaaminika zaidi kuliko wewe.

Kumbuka kamanda wewe na jeshi lako mnafahamika kuwa mu wabambikizia watu kesi mlio sugu. Mheshimiwa Rais Samia ametamka hivyo si mara moja. Kesi kadhaa mlizobambikizia watu zimekuwa zikifutwa hadharani.

Ni yesu au Mungu yupi unayemhusisha na Mbowe leo ambaye hamkuwahi kumhusisha wakati mkiwabambikizia watu kesi?

Kweli wewe utakuwa hujishangai kuwa ndugu, marafiki na majirani zake wanakushangaa wewe na madai yako haya ya ugaidi kumhusu bwana Mbowe?

Kama vile haitoshi umefikia hatua kututisha tusifike mahakamani kinyume cha katiba.

Kamanda Sirro haki zetu kama zilivyo za mheshimiwa Mbowe pia zina thamani.

Tukutane mahakamani.

Tusitishane.
 
Mbowe sio gaidi.
Sirro acha ubambikaji.

Kwa dhana hii mpya ya kamanda Sirro kuhusiana na mheshimiwa Mbowe hakuna haja ya kushiriki ulinzi Shirikishi au hata kushirikiana na polisi.

Kwani Sirro au polisi waliwahi kuokoka lini hata wakaacha kubambikizia watu kesi kufikia kuanza kutuhubiria sisi habari za Yesu au kumhusu Mungu?
 
Lini polisi ya bongo ikashirikiana ma wananchi??

I wish watu mngetembelea nchi zilizoendelea muone jinsi dhana ya polisi jamii inafanya kazi uzuri kabisa.

Ila kwa polisi hii inayofungamana na CCM hamuwezi kunishawishi hata kidogo.
 
Lini polisi ya bongo ikashirikiana ma wananchi??

I wish watu mngetembelea nchi zilizoendelea muone jinsi dhana ya polisi jamii inafanya kazi uzuri kabisa.

Ila kwa polisi hii inayofungamana na CCM hamuwezi kunishawishi hata kidogo.

Kesi ya Zombe ilivyoanza hadi kupelekea tume jaji Kipenka kuundwa ni ushahidi wa wazi wa kiwango cha udhwalimu mkubwa uliokithiri ndani ya jeshi la polisi.

Waliwachukua wafanya biashara wale wakawapora pesa zao zote na wakaenda kuwauwa kikatili kwa kuwapiga risasi moja moja visogoni mmoja baada ya mwingine wakiwa wamewalaza kifudi fudi porini mabwepande.

Kama vile haitoshi bado wadai wameuwa majambazi hatari waliokuwa wakiwatafuta wakiwa katika harakati zao za kutoroka huku wakiwarushia wao risasi.

Hiiiiii bagosha!

Tuwaamini kwa lipi hawa? Kwani basi hata walitubu na kuokoka lini tukategemee matokeo tofauti?
 
Kesi ya Zombe ilivyoanza hadi kupelekea tume jaji Kipenka kuundwa ni ushahidi wa wazi wa kiwango cha udhwalimu mkubwa uliokithiri ndani ya jeshi la polisi.

Waliwachukua wafanya biashara wale wakawapora pesa zao zote na wakaenda kuwauwa kikatili kwa kuwapiga risasi moja moja visogoni mmoja baada ya mwingine wakiwa wamewalaza kifudi fudi porini mabwepande.

Kama vile haitoshi bado wadai wameuwa majambazi hatari waliokuwa wakiwatafuta wakiwa katika harakati zao za kutoroka huku wakiwarushia wao risasi.

Hiiiiii bagosha!

Tuwaamini kwa lipi hawa? Kwani basi hata walitubu na kuokoka lini tukategemee matokeo tofauti?
CCM inachofanya kina baraka ya polisi..

Na polisi inachofanya kina baraka ya CCM

Yani hawa kuwatenganisha ni kazi sana
 
Sirro anachofanya kina baraka za Samia.

Yote hayo yanajulikana. Halipo jipya hapo:


IMG_20210704_051559_619.jpg


 
Yote hayo yanajulikana. Halipo jipya hapo:


View attachment 1877770

Kwa huyu maushungi, tumepigwa.
 
Kwa huyu maushungi, tumepigwa.

Iko hivi, uchaguzi wa kupigwa au kutopigwa ni wetu:

 
Back
Top Bottom