Ijue nyota yako: Fahamu mengi kuhusu nyota yako

Vipi kuhusu uchumba mwanamke mizani mkubwa amezid umri kidogo mwanaume ng'ombe inaweza kufanikiwa kufikia ndoa?na kama ikiwepo wataishi kwa raha?
 
Mpendwa, umenipa maneno mengi kuhusu mashuka na dhahabu ya kuchongwa. Sina neno, naweza kuvaa chupi na shuka na suti. Sitaki kuingilia katika imani yako kuhusu umuhimu wa tarehe za kuzaliwa kwa tabia au wakati ujao... Hii shauri yako, si imani yangu.
Ila tu kama tunakubaliana:
unajimu ni kitu tofauti na sayansi kama fizikia au kemia (hii ulidai, ni sababu yangu ya kujibu)
Ukitumia neno "nyota" si magimba yale katika anga la ulimwengu ambayo kila moja ni kama Jua letu. Nyota zako ni kitu kisichopimika kwa njia ya sayansi.
Hapa naweza kutulia nyota unazotaja ni siri yako.
Mimi nimejibu kwa sababu sipendi kama vijana wanachanganyikiwa na lugha ya aina hii.
Ninapenda sana kuangalia nyota jinsi zilivyo na kujua zaidi kuhusu tabia zao.
Ambayo ni kitu tofauti na imani yako.
 
Mkuu huelewi kuwa kiswahili ni lugha isiyokuwa na maneno yake rasmi? mengi yamekopiwa sana?
kaa na upuuzi wako wa kushangaa meli haizami shilingi inazama.

Rakims
 
Vipi kuhusu uchumba mwanamke mizani mkubwa amezid umri kidogo mwanaume ng'ombe inaweza kufanikiwa kufikia ndoa?na kama ikiwepo wataishi kwa raha?
Habari mkuu,
Elewa ya kwamba mizani na Ng'ombe kinyota huwa wapo katika hali moja ya sayari yaani wote huwa ni ZUHURA(VENUS)
Mara nyingi ng'ombe akiwa na umri wowote ule basi hujihisi kuwa kwenye mvuto wa kimapenzi na Mizani popote vyovyote vile amuonavyo lakini kinachomfanya asiweze kudumbukia kwenye lindi la mapenzi na nyota hii huwa ni ugumu na maamuzi yake ya kuhisi kupotea katika mahaba na mizani, maana ng'ombe humuona mizani ni mtu mwenye mvuto kimapenzi,mwenye huba na shauku na mwenye kutawala sana mapenzi na mwenye kuweza kumteka yoyote kimapenzi, kwa maana mizani yeye huzaliwa chini ya mahaba mazito sana ya watu wawili waliopendana kwa dhati wakati wanamtafuta kama mtoto nae hutengenezwa au hupatikana mara nyingi pale wazazi wake wanapokuwa kwenye highest state za mapenzi wote wawili. kutokueleweka kirahisi kwa mizani huzidisha zaidi mapenzi ya ng'ombe kwa maana asili ya kutokuzoeleka kwa mizani humfanya ng'ombe kila siku amuone ni mtu mwenye mapenzi mapya.
tatizo linalokuja kwenye mahusiano ya wawili hawa ni pale ambapo wote hutawaliwa sana na mapenzi ya mwenziwe ambapo hapo huleta shida zaidi katika maswala ya kushare kipato kila mmoja hupenda kufanya kitu cha kuweza kumfurahisha kwa kumzidi mwenziwe wanakuwa na ushindani wa kimapenzi hii hupelekea kuanza matumizi ya hovyo na kutia hasara ndani ya nyumba na tunashauri zaidi wenye kuoana chini ya nyota hizi mbili wawe ni wenye nafasi kimaisha wasiwe wenye kipato kidogo. ndio hapo huja kauli ya mapenzi na dhiki, pia kwa baadae kumbuka kuwa ng'ombe hupenda sana utawala hivyo mizani hupenda haki sawa sasa mwishoni mwa majibu ni kuwa hii couple haiwezi kuchukua muda mrefu wao huachana

Rakims
 
Hizi mambo nishafatilia sana hazina ukweli wowote kimaisha labda uya rasimishe na ushirikina tofauti na hivyo hakuna uhusiano na maisha ya kawaida ni uongo tu
 
Salama ok mkuu asante sanaa
 
Hizi mambo nishafatilia sana hazina ukweli wowote kimaisha labda uya rasimishe na ushirikina tofauti na hivyo hakuna uhusiano na maisha ya kawaida ni uongo tu
mkuu sio kila anaeambiwa kuuza dhahabu na madini mengine ni utajili huwa anakubali hasa kwa watu kama wewe wasiojua chochote kinachoongelewa walioishia kudanganywa tu.
 
u
mkuu sio kila anaeambiwa kuuza dhahabu na madini mengine ni utajili huwa anakubali hasa kwa watu kama wewe wasiojua chochote kinachoongelewa walioishia kudanganywa tu.
naamini hauna elimu ya literature ndiyo maana sikulaumu ila inabidi niounguze uzito wa hoja ili tufikie muafaka
 
mkuu sio kila anaeambiwa kuuza dhahabu na madini mengine ni utajili huwa anakubali hasa kwa watu kama wewe wasiojua chochote kinachoongelewa walioishia kudanganywa tu.
Alichoandika LOVE U JF ni maarifa yake. Anastahili heshima na kutoambiwa eti hajui chochote na amedanganywa.
Nilikuambia huko juu madai yako kuhusu "sayansi" ya imani yako hayana msingi, ulishindwa kujibu chochote. Nilikuambia pia yale unayoita "nyota" hayana uhusiano na nyota halisi. Hujakuwa na jibu.

Basi kwa hiyo isingekuwa vibaya ukijibu watu wa unyenyekevu kiasi badala ya kuwasemea, sivyo?
 
unyenyekevu unaujua wewe? hapa unachotaka kuwaambia wengine ndio na wewe unaambiwa hivyo hivyo.
Kuna member kama 500 na zaidi wamesoma thread na kujifunza kisha wakakaa kimya wengine wanadeal na mimi P.M na wengine wanauliza na kujibiwa kistaarabu na kielimu kama maswali yao yalivyo ukiona umejibiwa pumba jua umeongea Pumba na hujui upo kwenye jukwaa lipi, wengine kati ya idadi ya member hao wanasoma na kuyaacha yalivyo. wewe kihele hele cha kuquote usiyoyajua ni nini?

Rakims
 
unafiki au umbea huanza pale unapoona mtu anaongea na mtu mwingine halafu wewe unadakia kudakia.
 
Katika mambo fulani hebu nieleweshe, nataka kuelewa ni hizo rangi za nguo tunazotakiwa kuzivaa zina impact gani je ni kuleta mvuto zaidi ama zina nini hasa kila mwenye nyota afuate yale yanayopasa avae?
 
Naomba unijibu swali langu hapo juu
 
Katika mambo fulani hebu nieleweshe, nataka kuelewa ni hizo rangi za nguo tunazotakiwa kuzivaa zina impact gani je ni kuleta mvuto zaidi ama zina nini hasa kila mwenye nyota afuate yale yanayopasa avae?
Darasa hilo mkuu lakini kifupi nitakujibu hivi hapo kinachotakiwa ni rangi ya nguo ya kuvaa maana hizi huwakilisha nguvu ya sayari inayochomoza kwa mwenye nyota hiyo mara tatu kwa siku ambapo anapovaa huwakilisha sayari hiyo kwa wanajimu, lakini kwa wenye mambo ya kiroho rangi hizi mtu anapovaa basi huwakilisha au kutawala majini na kuwashinda nguvu wanaotawala sayari hiyo, pia kuvaa rangi hizi kwa maana nyingine humletea mtu usafishwaji wa aura ya nyota yake hasa ukirudi hapo nilipoandika kuwa mwenye nyota ya hii nyota inayomsaidia kipesa labda ni simba hivyo akitaka apate msaada wa pesa au kufanikisha jambo la kipesa itabidi atumie mahitaji ya nyota ya simba kwa siku maalum na hali maalum. umeelewa kidogo?
 
Safi sana mkuu nimekuelewa sana umefanya simple ila contents imeshiba maana ya swali langu,ahsante sana
 
unatakiwa ujue kwanza kwamba nyota sio uchawi lakini kama imani yako inakwambia nyota ni uchawi basi achana na kuzifuatilia
Asalaam mkuu,
Mimi ni muumini mkubwa wa mafundisho yako, hasa kutokana na elimu uliyojaliwa ya kupambanua maarifa mbalimbali juu ya meditation, nyota n.k

Niende moja kwa moja kwenye swali. Mimi nna majina mawili, jina la utotoni na jina la shule. Moja linaanziwa na G na lingine linaanziwa na M. Pia tarehe yangu ya kuzaliwa ni SEPTEMBER 7. Je nyota yangu ni ipi hapo mkuu?
 
ni p.m details zako za kuzaliwa ikiwemo jina la kuzaliwa na jina hilo la shule,
tarehe mwezi mwaka na saa pia eneo uliozaliwa, nitakurudia hapa na majibu mkuu, karibu wengi hawafahamu ya kuwa ukijifunza kitu sio lazima kufanya mengine baadae yanakupa maarifa mtu akitaka kufanya unajua huyu kaanza hivi ataishia hapa,

Rakims
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…