Ijue nyota yako: Fahamu mengi kuhusu nyota yako

hivi gemini kwa gemini ikoje ,yaani na kademu kuachana hamna vita haziishi
 
Zinabadirika kutokana na jina kamili la muhusika na thamani yake.
Kwenye habari ya pesa uliza kwa watu wa punda watakujibu mkuu uthibitisho wangu ni member wenye nyota za punda watakwambia anaweza akakuonyesha ubora na wema wake sasa hivi lakini ukikaa na mtu ndio utamjua.
Ukitaka kujua uhondo wa ngoma ingia ucheze
 
hivi gemini kwa gemini ikoje ,yaani na kademu kuachana hamna vita haziishi
MAPACHA NA MAPACHA

Kwa mtizamo mnaonekana nyote wawili ni wenye asili ya upepo wa pumzi hivyo katika vitu vyenu vingi nyie ni kama pacha wa kiroho lakini hiyo haimaanishi kuwa mmekamilika kwa sababu mnaendana kwa asilimia 83% ingawa mna thamani kubwa ya muendano mtizamo wenu unakuwa
Hakuna mfano wa mahusiano kama yanapokuwa yamejengwa na watu wawili wenye mtizamo huu wa upepo ulio wa kuendana vizuri kwenye haiba, wenye msisimko na furaha kama wa wewe na mwenzio mnaonekana ni watu ambao hamtawahi kuchoshana au kuchokana kirahisi kwa maana nyie ni kama mapacha na ni wenye nia moja kwa kila jambo ;- kasi yenu katika mahusiano inashika namba za juu mkiwa pamoja na mnakuwa ni sawa na mfano wa kuigwa kwa mahusiano ya wengine ndio hawa mkikutana utasikia ndoa zingine zinawapigia mfano kuwa unawaona fulani na fulani.

Nyote ndoto zenu kila mmoja kwa mwenzie ni kubwa na hakuna kati yenu anaweza kumkatia tamaa mwingine. Pia ni wenye mazungumzo ya kuvutia hata chat zenu mtu mwingine akitizama anaweza kutamani jinsi mnavyojibizana na jinsi mnavyoweza kuelewana katika maongezi

pia mahusiano yenu yanaonekana kuwa na marafiki wengi na pamoja mnaweza kuwa mnafanya makaribisho ya chakula au sherehe mkiwakaribisha watu wanakuwa wanawatamani sana. Sex ni mchezo mzuri na uliojaa matani mengi kwenu lakini ndio mahusiano yenu kuna kipindi yanaweza kuwa kama ya juu juu, yasio imara, na msiokuwa na utulivu hasa mkiondoka mazingira ya nyumbani /chumbani na mkikaa muda mrefu bila kukutana na kucheza cheza kimwili basi kila kitu kinakuwa machafuko mkikosa tendo kwa muda ikiwa mnajua au hamjui basi huzuka chokochoko za ugomvi wa maneno.

Rakims
 
Asee 100% utafikiri unatujua,hii dunia kuwa mpole watu wanajua mambo asee
 
Hizi nyota zinanichanganya tu nyota ya kuzaliwa ng'ombe , ya herufi la jina langu ni nyotaa ya kaa lakini nina sifa zote za nyota ya mapacha
 
Mkuu Rakims , naomba kuuliza eti kuna watu wanao uwezo wa kuchukua nyota na akili za wengine na kuzitumia kwa manufaa yao ,natanguliza shukrani.
 
Mkuu naomba kujua mambo haya endapo nyota ya cancer na aquarius wakiwa mahusianoni

  • Kazi
  • Biashara
  • Maisha kwa ujumla wake
  • Mahusiano yao
 
Boss mwanaume nyota samaki MWANAMKE punda. Kuna future hapa kweli
 
Hizi nyota zinanichanganya tu nyota ya kuzaliwa ng'ombe , ya herufi la jina langu ni nyotaa ya kaa lakini nina sifa zote za nyota ya mapacha
Ascendant yako inaweza kuwa mapacha
 
Mkuu Rakims , naomba kuuliza eti kuna watu wanao uwezo wa kuchukua nyota na akili za wengine na kuzitumia kwa manufaa yao ,natanguliza shukrani.
Hapana mkuu sio nyota ni kumtoa mtu kafara nyota haichukuliwi bali ni namna ya mvuto wa nguvu yako ndio huchukuliwa wanarahisisha tu kusema nyota
 
Boss mwanaume nyota samaki MWANAMKE punda. Kuna future hapa kweli
Mwenye nyota ya samaki atakufa kibudu.
Hapo ni kujitafutia presha nyota zikigeuka angani shughuli inaanza
 
Ipo karibu
nakumbuka niliwahi kutizama milango miwili ulinitoza elfu mbili kitambo kidogo kimepita vp kwa sasa naweza kulipa tena 2000 na alafu nataka nijijue upande wa betting mchezo upi unanifaa hii football naona nakosa timu moja kila siku hadi nahisi sio kawaida sasa mlango upi wa kutizama kuhusu betting na mingine ikibidi na kwa gharama kiasi gani au bado ni ile ile niliyolipa kipindi kile cha nyuma
 
Ni mwaka na miezi sasa hicho kiwango kilibadirika mkuu.
Lakini kwa kuwa ni mtu uliwahi kutizama nitakutizamia kwa elfu 4 kwa mlango halafu kuhusu mlango wa kutizama betting ni bora ungetizama mlango wa tano na sayari zako 7 kisha kama unataka kutizama kwa ajili ya jackpot basi unaweza kutizama na mlango wa 9

Rakims
 
Mkuu Rakims , naomba kuuliza eti kuna watu wanao uwezo wa kuchukua nyota na akili za wengine na kuzitumia kwa manufaa yao ,natanguliza shukrani.
Kaka nyota huchukuliwa au kuibwa, hii kitu inawezekana ipo na inafanyika epuka matapeli mjini [emoji16]

Elimu changa [emoji3]
 
Labda kama hamfahamu kitu, Binadamu aliumbwa katika sehemu kuu tatu nazo ni mwili, Nafsi na Roho . Ambapo mwili ndio mavumbi au udongo, Nafsi ambayo ndio mtu husika ndio nyota na Roho ndio pumzi ya uhai inayofanya Nafsi na mwili viweze kuwa hai na kufanya kazi zake, katika falaki tafsiri ya nyota ni hii, Nyota ni nini?

Nyota ni Nafsi ya amani ya mtu inayotambulisha mustakabari mzima wa mafanikio ya maisha yake, ule nini? ni nyota yako, uvaeje? ni nyota yako, uwe na elimu gani? ni nyota yako, ulizaliwa wapi? ulizaliwaje? ,yaani kiufupi nyota ndio kila kitu kwa mtu ina details zako zote tangu uliopozaliwa mpaka ulipofikia na mipango yako ya baadae [emoji6], usishangae leo nabii anakuangalia tu anajua jina lako, uliopozaliwa ,maisha yako yote mpaka umefikaje kwake na ukitoka hapo kwake utaelekea wapi na huko utafanya nini na ukilala utaota nini maana anaekusoma nyota atajua hata ndoto zako unapolala maana ndoto ni moja kati ya funguo tano za ulimwengu wa roho ( sio somo la leo),(ingawa sio Manabii wote lakini mi naelezea wale ninaowajua [emoji16] usistuke maana wanajulikana mbona [emoji6]), wanachokifanya wanakusoma nyota kwa kutumia darubini za kichawi then nyota inaeleza kila kitu kukuhusu wewe.

Na ndio maana hakuna kitu hatari ambacho naona members wengi humu wanafurahia kama kusomewa nyota, Ndugu unafanya kitu usichokijua madhara yake, huyo anayekusomea nyota sio mama yako kumbuka, na yeye anapenda kufanikiwa kama wewe na ana tamaa zake tu nyingi kama wewe, halafu anaona unakitu kizuri ambacho hana na hujijui kama unacho hata kama ni wewe msomaji wangu we utafanyeje?[emoji16] Mbuzi kajileta kijiwe cha mishkaki [emoji23], Unakuta kuna watu wana nyota zinangaa hatari halafu anaenda kusomewa nyota either kwa mchawi, mganga, mfuga majini au mtu yeyote mwenye elimu ya Falaki ,huyu yeye hajijui alichobeba lakini mtaalam anaiona inavyotamanisha kwa jinsi inavyo shine,(kifuatacho ITV)ndio watu wengi nyota zao zimekamatwa kwa namna hii watu wanaopenda kuzunguka kwa waganga wa kienyeji, kupigiwa ramli, kusomewa nyota zao,kutabiliwa na Manabii na kwa hizo people hatari nilizozitaja hapo juu[emoji16]

Na ndio maana ukihama kwenye kanisa la Nabii au Mtume wa hivi utateseka na kuhangaika sana, utapata msoto hujawahi ona [emoji3] mpaka urudi tena kwake na watu wengi hawajui Kwanini iko hivi, ndio ushatekwa nyota mzee kwa hiyo mafanikio yako yanategemea yeye anasemaje, kaisha kusajili kwa alama za vidole [emoji1787] kwenye madhabahu yake, kwa sababu ya kupenda kutabiliwa na kusomwa nyota na watu usiojua background zao, muwe mnauliza kwanza jamani 🥲,walisemaga mjini form six [emoji23], maana yake mjini shule huna shule unatekwa na wenye shule yao, akili mkichwa [emoji16].

Hiyo nimeelezea kama akihama lakini kiuhalisia ukishatekwa kwenye madhabahu hizi hutoki kirahisi,(Nimekumbuka meme moja ya watu ambao hawashauriki duniani "mwanaume aliyepata hela ghafla, msichana aliyependa kiukweli na Mwanamke anaesali kwa Mw......osa"[emoji1787][emoji1787] ni meme tu jamani haina uhalisia) tena watu wakikuambia unaona kama vile wao ndio mapepo yametumwa kukujaribu imani [emoji23], hatari sana hizi mambo na si ajabu kukuta wakimwabudu nabii wao kama Mungu wao(mf,Zum.....idi the Don [emoji23]) maana hawana uhuru tena Nafsi zimeshatekwa kitambo na huwaambii lolote labda kama unataka kipigo na huwa wapo tayari hata kujitoa maisha yao ili kulinda hiyo madhabahu, huwa nawafananisha na ndugu zangu wa Dini ya haki [emoji16]. It's just a comparison not really thing (sijasema ni dini gani msinihukumu bure jamani sijataja mtu au imani ya mtu mimi [emoji23]).

Tatizo linakuja pale ambapo wengi wetu tumeaminishwa nyota ni kipaji, lakini sio kweli kipaji ni sehemu ndogo tu kwenye nyota yako(kitaalamu tunawezaiita pembe ya nyota kati ya zile pembe tano) na ndicho kinaweza onesha ni jinsi gani nyota yako inang'aa lakini chenyewe sio Nyota, na Nyota imeundwa na pembe tano na magimba matatu makubwa (ila hili sio somo la leo). Huo ni mwonekano wake katika mtizamo wa falaki.

Na Nyota inaweza kufanyiwa hivi vitu kama haitalindwa vyema, 1.inaweza kumilikiwa, 2.inaweza kukamatwa, 3.inaweza kufifizwa mngao, 4.inaweza kuzimwa kabisa, 5.inaweza kufungwa kwa mafundo na pia 6.inaweza kuibiwa nasisitiza INAWEZA KUIBIWA na kwa kuwa ndio Nafsi ya mtu ikiibiwa ndio unaona mtu kaweuka. avae nguo au asivae sawa tu, alale popote sawa tu, ale chochote hata pumba sawa tu, maana sio yeye tena ila ni mwili na roho na kivuli ndio zimebaki, Nyota yake ishaenda kuuza duka,au kuendesha malori (ila hii ni mifano tu jamani [emoji3]). Na ikitokea ikarudishwa kwenye mwili wake ndipo Kumbukumbu zote zinamrejea anajua mi nani niko wapi, kumbe nipo uchi na mambo mengine ya utambuzi na mtu aliyeibiwa hawezi jijua kama kaibiwa.

Yaani kama wewe hapo unajijua mimi naitwa fulani naishi sehemu fulani mamaangu ni fulani na unasoma uzi huu wewe hujaibiwa nyota ukiibiwa nyota hayo yote hutayajua unakuwa chizi au kichaa narudia tena kwa msisitizo unakuwa chizi, lakini kama unajitambua huenda imefanyiwa vingine ila sio kuibiwa.

Lakini nyota zinaibiwa tena sana hili ninalijua anaebisha abishe lakini huo ndio ukweli na kuna siri kubwa sana imefichika kwa hao vichaa wanaotangatanga barabarani sio wote wagonjwa wa akili zaidi ya asilimia 90 ni watu walioibiwa nyota zao,( zina make money somewhere then yeye anakuwa monitored na radar za kipepo, [emoji2960] usishangae radar tu, sheol kuna mpaka computers powerful duniani hazipo maana wengi wetu wanafikiri kuzimu ni madawa madawa tu matunguri [emoji23], mambo ya kienyeji enyeji, labda tu nikumegee ka Siri ila usimwambie mtu [emoji16] Technology nyingi kubwa zinazoushangaza ulimwengu za dunia ya leo kwenye mawasiliano, usafiri,uhandisi,afya n.k sio kwamba wazungu walikaa wakafikiri tu [emoji16] maana najua ndivyo ulivyokaririshwa na wenzako, behind the scene ni sehemu kidogo sana ya maarifa ya huko.

Ingekuwa ni kufikiri tu hata wewe ungefikiri mkuu,kwani wewe huna kichwa cha kufikiri au mzungu kakuzidi vichwa vingapi au masikio mangapi, au mikono mingapi fikiria mtu wangu?, (Usione vyaelea havijaundwa vimekuwa copied somewhere you never see [emoji23]na wenye dunia yao) ila hii ni ya kwangu jamani[emoji16]. na kwanini technology kubwa zinatoka kwao tu (Whites, especially America) kuna nini America? Why not Malawi? Hata ikitokea huku haiwezi kuwa global why?. Labda nikupe mfano halisi......., mhh lakini basi tu maana navyokujua wewe utaenda kusema tu na wakati tumekubaliana ni siri yetu[emoji23].

Jamani ndugu zangu ki ufupi Dunia inawenyewe na ina mkuu wake na ina mifumo yake, mwisho wa siku umekaribia, tukeshe katika kusali, kuomba na kumtafuta Mungu wa kweli maana yupo na anapatikana, achana na watu wanakuambia hakuna Mungu kwa sababu eti haonekani, au hakuna ulimwengu wa roho, usiwalaumu wala kuwahukumu maana unakuta wengine hawajui hata wanaongelea [emoji16] nini wanaposema ulimwengu wa roho au huenda ndio wazee wa shughuli wanaona wanaumbuka wanajaribu kutapatapa maana uchawi ni kujificha (mazingara ombwe) ukiufichua huwa unakawaida ya kukosa nguvu kwako (hako ni ka siri kapya tena nimekupa ila usiseme kwa sauti [emoji16] kama huna nguvu ya kutosha wasije wenye siri zao, wakakukunywa supu asubuhi na mapema[emoji1787], sema ukiwa umejipanga vizuri like someone who write something to you now in JF).

Mwisho wa yote ndugu tuwe tayari ili atakapokuja atukute tuko tayari twende naye kwetu(Mbinguni)panako tuhusu sio hapa tulipo saa hizi, hii ndio ponapona yetu, tofauti na hapo mi sijui.

Naomba niishie hapa jamani njaa inauma[emoji3525].

Source: Elimu changa [emoji3]

#Zakuambiwachanganyanazako.
 
kwa hiyo Unatakiwa ufuatilie hayo masharti sijui rangi za nguo manukato n.k ndio ufanikiwe mkuu au inakuaje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…