Ijue nyota yako: Fahamu mengi kuhusu nyota yako

kwa hiyo Unatakiwa ufuatilie hayo masharti sijui rangi za nguo manukato n.k ndio ufanikiwe mkuu au inakuaje
Ukiwa upande wa pili namaanisha ule wa giza inabidi ufate hivyo vyote ili ufanikiwe, maana hata siku za wiki pia kuna namna zimegawiwa kwa wakuu wa mapepo wanaotawala siku hizo ili kukupa mafanikio au faida fulani kwa mtu anaefuata masharti kulingana na muongozo wa falaki, ndio maana zipo siku katika wiki ila sitazitaja ila kwa wajuvi wa mambo haya katika falaki wanazijua, kwa mfano ipo siku katika wiki kuna mtu huwa hakopeshi kitu chochote, hata kama unataka kufa hakupi maana katika falaki siku hiyo ukikupesha hutakaa ulipwe [emoji16], au tena kuna siku ukimtongoza mwanamke hata kama alikuwa anakataa lakini kwa sababu ya uvuvio uliopo katika hiyo siku kutoka kwa mapepo wanayoitawala atakubali tu ili mkazini maana ndio kazi yao kwenye hiyo siku, na pia ipo siku kwenye juma hata yule mchawi beginner akikupiga kombora linakupata kisawasawa pamoja na kuwa ana nguvu(aced) ndogo, ndio maana usione kakushindwa siku fulani halafu anakuambia ngoja utaona, ile ngoja maana yake anasubiri siku husika ambayo katika hiyo siku mtu ukirogwa kinakupata kisawasawa, Hata maneno hivyo hivyo kuna siku ukimtamkia mtu laana au baraka ya kichawi lazima impate effectively. Na ukienda extra miles utakuja kuona hata katika ajali nyingi kubwa au majanga fulani makubwa yanayotikisa utakuja kugundua mfanano wa miezi, siku na wakati mwingine masaa, ni kwa sababu ya kalenda shughuli ya upande wa giza.[emoji2960]

Ki ufupi ndugu yangu ingawa sijuwagi kuelezea kwa kifupi najikuta nishaandika essay [emoji3],

Ipo kalenda ya kichawi ambayo imepanga matukio yote yafanyikeje, yafanyikie wapi na kwanini, kuanzia mwaka, mwezi,siku,saa, dakika kila wakati kuna kitu cha kiroho katika ulimwengu wa giza lazima kifanyike au kutekelezwa ,na kupitia kalenda kama hii watu wa falaki hucheza nayo ili kujua mtu mwenye nyota ya aina fulani akifanya kitu fulani kwa siku fulani, (kwa sababu ya ule uvuvio wa kipepo katika ile siku) lazima afanikiwe au imwendee vizuri. Na akikosea hayo masharti ndio ataanza kuona mambo kama hayaendi, hasara zinakuwa nyingi na kadharika.

Lakini ndugu zangu haka nako ni ka namna fulani ka [emoji16]utumwa kwa wanadamu kutoka kuzimu ili kuwafanya wasiwe huru na kufurahia maisha yao kwa sababu watakuwa bize kuangalia rangi za nguo za kuvaa perfume, nk. Ili mambo yao yaende na ni kweli wala sio uongo ukifata hivyo vile vi uvuvio vya kipepo vinakufanikisha kwa sababu vinapenda hiyo rangi au hiyo harufu katika hizo siku zao za kazi.

Lakini katika upande wa nuru maandiko yanasema "Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli"
lakini pia "mtaifahamu kweli nayo kweli itawaweka huru",
swali la msingi kweli nini?
"Uwatakase kwa ile kweli neno lako ndio kweli"

Basi kama tumejua neno la Mungu ndio kweli kumbe vingine ni vya kubumba kwa hiyo kile alichosema Mungu ili mwanadamu afanikiwe ndio ukweli wenyewe kama alisema ili ufanikiwe kila jtatu mwanangu usivae kitu chochote cheusi [emoji16] basi tujue kuwa kila atakae vaa kitu cheusi hatafanikiwa, lakini kama halijasema basi hicho ni cha kubumba na kinafanya kazi katika upande wa giza tu lakini katika nuru tuna kitu kinaitwa neno la Mungu huu ndio msingi wa mafanikio ya mwanadamu ambayo atayafurahia kwa amani, maana yapo mafanikio yanayopatikana lakini wenye nayo hawana furaha wala amani kwayo, yamejaa masharti ya ajabu Sana, usione watu wamefanikiwa kaka wana siri nzito sana wamebeba, hawana furaha na Amani katika mali zao wenyewe.
Basi tuone Mungu anasemaje kuhusu mafanikio ya mtu au mwanadamu" "Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana".

Ndugu zangu mafanikio katika njia ya nuru ni ya hakika sema watu wengi tumepofushwa na giza ili kuiona njia hii ni ngumu na ni ya muda mrefu lakini sio kweli huko gizani ambapo wengi hukimbilia ni pagumu hujawahi ona, lakini huku kuna furaha ya ajabu na amani isiyo ya kidunia, unaweza usiwe na gari na umepanga lakini furaha na Amani yako kuna tajiri mmoja ana hotel na magari ya kutosha hajawahiipata, na hata wakati wako ukifika ukapata hiyo gari, ndugu yangu nashindwa nikuambieje lakini utaenjoy na kuifurahia bila masharti ya kulala kwenye ngozi, sijui usilale na mke wako siku fulani sijui asipande mtu wa aina fulani, maana haya ndio baadhi ya masharti yao na yapo mengine magumu ya ajabu. Lakini pia kumbuka mali iliyopatika kwa ghafla ndivyo pia itakavyoondoka, Mungu wetu huwa ni wa utaratibu, na akikupa amekupa kweli hatakuja kukunyanganya, ila sio wale wakulungwa wapo chap [emoji16][emoji1787] kidogo kuchukua kilicho chao ukikosea masharti yao.

Wengine wanasema eti upande wa giza hujibu kwa haraka sana na mali zao hupatikana kwa haraka zaidi kuliko kutegemea neno la Mungu,

Mwingine nakumbuka humuhumu JF akawa anasema eti mfano mtu akiibiwa kitu mwingine akaenda kuomba kwa mizimu mwingine kwa Mungu wa kweli wa mizimu atajibiwa haraka sana kuhusu mwizi wake na huenda huyu wa kwa Mungu asijibiwe.

Lakini alikuwa anazungumza kitu asichokijua, watu wengi wanaojiita au kujifanya wanamtumikia Mungu wa kweli hawamtumikii ipasavyo kama wanavyofanya wa upande wa pili(giza) na hii ndio sababu inayopelekea wasisikilizwe na hivyo kuonekana upande wa pili unajibu kwa haraka lakini kwa mtu anayejua nini anafanya na anatimiza kila takwa la Mungu wake, usije kujaribu matokeo yake ni papo kwa papo, maana ile akipiga tu magoti kukushtaki ushapotezwa zamani (najua kuna mtu anashangaa hii inawezekanaje) Ila ndio iko hivyo sema wengi wa hawa waaminifu hawana roho za visasi na huomba mema hata kwa adui zao ndio maana wanaonekana wadhaifu na wengine hawaelewi kama wanaweza kutamka jambo likatokea kama wanavyotaka na hivyo kujikuta kama watu wasio na uwezo, na mizimu kuonekana inajibu haraka kuliko wao, lakini ukweli ni kwamba ni watu hatari katika ulimwengu wa roho maana akimwomba Mungu neno anasikilizwa na majibu ni dhahiri,sasa usiombe neno lenyewe likawa ni mashtaka dhidi yako, jua halitazama utakuwa umeshaanza ku experience matokeo ya ulichomfanyia, si tishi mtu ila naelezea ninachokijua.

Hivyo ndugu yangu kama upo upande wa nuru hayo masharti haya determine mafanikio yako, wewe unakuwa umeunganishwa na madhabahu tofauti na za kiganga, za wasoma nyota, za wafuga majini, kwa hiyo mafanikio yako yatategemea Mungu wako amesemaje,sio masharti ya falaki yanasemaje maana hiyo inafanya kazi kwenye madhabahu nyingine tofauti na uliyopo wewe ni hivyo tu.

Source: Elimu changa [emoji3]

#Zakuambiwachanganyanazako
 
Aise shukran sana Mkuu nimejifunza mengi kwa faida tu unaweza kunitajia hizo siku hebu ni PM
 
Mafunzo yanayohusisha WANADAMU kupata Suluhu au mwongozo wa maisha kupitia NYOTA ni mafundisho ya Giza na Shetani ndio baba yenu.

Ni DHAMBI na marufuku Kwa aaminie ktk MUNGU mmoja kuamini habar ya NYOTA.

Wamwaminio KRISTO YESU hutumia njia ya MAOMBI na maelekezo Kutoka Kwa ROHO wa YESU MTAKATIFU kupata solution ya changamoto wapitiazo au maelekezo juu ya namna Gani waendeshe maisha Yao.

Ukimia NYOTA mwisho wako ni KUZIMU na JEHANUM penye moto wa milele.

Ukimwamini YESU kuwa ni KRISTO na ni MWANA wa Mungu utaokoka, atakupa Roho wake Mtakatifu atakuongoza na utaingia MBINGUNI na utafurahi milele na milele.

Uchaguzi ni wako. Amen
 
Nataka kuijua nyota yangu kupitia Milango yote 12 .
Unaelekea kuwa mchawi ukijifunza hayo, stuka.

Mungu amekataza hayo, mwabudu, mwombe Mungu atakusaidia.

Moto wa Kuzimu ni mbaya sana, mafundisho haya yanakupumbaza Ili ufe baadae ukateketee ktk MOTO wa milele. Amen
 
Assalam Aleykum mimi naomba unipigie wewe kuhesabu upige nyota zangu zote tatu ipatikane moja peke yake mimi jina naitwa HASSAN ABDALLAH MOHAMED mamangu anaitwa khadija Mohamed Salim nilizaliwa tarehe 13-01-1992 naomba unipigie hesabu zote unipatie nyota moja peke yake ambayo inanihusu please mkuu
 
Mwanaume ana nyota ya mashuke na mwanamke wake ana nyota ya Inge hapo inakuaje mkuu?
 
Kwahyo kati ya herufi ya jina na tareh ya kuzaliwa ipi inafaa
 
Aliyeziumba hizo nyota alikuwa ni Shetani?
Aliyetambua kuwa huyu ni christo roho ya Mungu alikuwa ni Shetani?
Aliyechambua unajimu alikuwa ni shetani?
Au unachanganywa unajimu na ramli kijana wangu?

Rakims
 
Unaelekea kuwa mchawi ukijifunza hayo, stuka.

Mungu amekataza hayo, mwabudu, mwombe Mungu atakusaidia.

Moto wa Kuzimu ni mbaya sana, mafundisho haya yanakupumbaza Ili ufe baadae ukateketee ktk MOTO wa milele. Amen
Sasa hapo unamshtua au unamtokomeza kwa maombi?
Unajua vitu vingine vinaweza kufanya watu wahisi mtu umevuta kitu ambacho hawajawahi kusikia hata jina lake.

Rakims
 

Waaleykum salaam, japo kwa kukushauri si vema sana kutoa details zako zote za kuzaliwa kwenye social network hivi ni bora ungetuma PM kisha hapa ukaja kusema teyari, pia kwa sasa sifanyi uchambuzi hadharani mkuu japo nitakusaidia kwa uchache,

Unaonekana kuchomozewa na nyota ya Ng'e kwa maana herufi ya kwanza ya jina lako ni H ambayo thamani yake kinajimu ni 8 (scorpio) na thamani ya jina lako na la mama ujazo wake ni 740 ambayo ni thamani ya 8 (scorpion) vile vile hivyo nyota yako ni Capricorn yaani mbuzi na ascendant yako ni Scorpio (yaani nge)

Hapo unakuwa na tabia za nge na nyota yako ni mbuzi

Kwa uchambuzi zaidi na malipo wasiliana nami kupitia

Whatsapp: +255 783 930 601

Rakims
 
Mwanaume ana nyota ya mashuke na mwanamke wake ana nyota ya Inge hapo inakuaje mkuu?
Wana asilimia 73 tu za mahusiano yao japo mapenzi yao yana usaliti chungu mzima ndoa yao huchelewa sana na ikiwahi basi huwahi kuvunjika vile vile na ikichelewa huvunjika pia.
Hawa nj wasafiri wawili kwenye safari moja wakifika kituoni kila mtu huenda zake.
"Endae tezi na omo atarejea ngamani"
Kupotezeana muda na kudanganyana tu hapo matokeo yao ni kudumazana unless maombi yapite.

Rakims
 
Aliyeziumba hizo nyota alikuwa ni Shetani?
Aliyetambua kuwa huyu ni christo roho ya Mungu alikuwa ni Shetani?
Aliyechambua unajimu alikuwa ni shetani?
Au unachanganywa unajimu na ramli kijana wangu?

Rakims
Mungu ndiye muumba wa mbingu na Nchi na vyote vilivyomo.

Mungu aliweka mipaka, Si vitu vyote vinaruhusiwa kuvifundisha au kuvigusa.

Miti yote Edeni aliumba Yeye bt alizuia mti wa ujuzi wa mema na mabaya usiguswe.

Mungu amekataza kujifunza na kubashiri kupitia nyota.

ELIMU ya Unajimu ni uchawi, Malaika waasi walipotupwa duniani ndo waliwafundisha WANADAMU habari hizo.

Najua unajua nachosema, wewe U Mchawi na Mganga pia.
 
Kila moja inafaa kwa upande wake
Mkuu mnatuchanganya asee

Ni ipi njia sahihi ya kuijua nyota yako je ni kwa kuangalia tarehe yako ya kuzaliwa au hiyo ya mahesabu ya jina lako na la mama yako

Ni ipi ya uhakika kabisa
 
Je, Kuna Faida gani zinapokutana nyota ya samaki na mbuzi kimapenzi???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…