Ijue sanaa ya wezi (Vibaka na majambazi)

Ijue sanaa ya wezi (Vibaka na majambazi)

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Je, ulishawahi kutumia japo dakika chache kuwaza 'Saikolojia ya wezi?

Wizi ni sanaa ya kuchukua kisicho halali yako! Wizi ni sayansi ya kujimilikisha visivyo vyako!

Je; Inakuwaje mtu anakua mwizi?

Chimbuko kuu la wizi ni DHIKI, TAMAA au MATATIZO YA KISAIKOLOJIA

Chimbuko la kwanza la wizi (DHIKI) limeonekana kuwa chanzo kikuu cha TAMAA na TATIZO LA KISAIKOLOJIA!

DHIKI ni ile hali ya ufukala kiasi cha kukosa mahitaji mhimu! Miongoni mwa mahitaji hayo ni pamoja na chakula, mavazi na vileo!
Kundi hili la wizi wa DHIKI unahusisha matumizi ya MWILI ni kwa asilimia 80% na akili ni asilimia 20% tu

Matumizi ya MWILI katika wizi wa DHIKI yanahusisha UMRI Wenye nguvu ambapo utaona VIJANA wengi wataangukia kwenye kundi hili!

Katika kundi hili Vijana wa kiume wanaonekana kuwa HATARI zaidi kuliko wanawake kutokana na KUJERUHI katika majukumu yao , hii ni kwasababu ya kwamba VIJANA wa kiume hujihusisha na matumizi ya nguvu (Roba) na ukwapuaji ili kujipatia kipato.

Na wanawake hutumia miili yao kingono kama sehemu ya kujipatia kipato!
Lakini wote kwa pamoja katika kundi hili matumizi ya MWILI huwa ni makubwa zaidi kuliko akili (80% kwa 20%)

Wizi wa TAMAA Ukoje?

Aina hii ya wizi ni steji ya pili baada ya mtu kuwa na DHIKI!
Ni rahisi sana kumbadilisha MWIZI akiwa katika steji ya DHIKI kuliko akiwa steji ya pili ya TAMAA!

Vijana walio kwenye kundi la DHIKI wakipatiwa kazi ya kufanya wanauwezekano mkubwa wa kuacha wizi kwa 95%!

Pia inaelezwa wanawake walio bahatika kuolewa wakiwa katika steji ya kwanza ya DHIKI hubadilika na kuwa na tabia njema sana hata kushangaza wengi!!

Lakini WIZI WA TAMAA ni hatua ngumu kidogo!

Bila shaka ulishawahi kuona mtu mwenye uwezo akaiba kitu cha kipuuuzi kabisa ambacho hata hawezi kukitumia!

Ukipita kwenye sherehe wizi wa namna hii utaukuta sana! Watu huiba masufulia, vikombe, pombe, vijiko hata chakula!

Wanapoiba haina maana hawajala au wana njaa sana, basi tu hukwapua ili mradi tu wasitoke mikono mitupu!
Wengine huiba hata pombe wasizo tumia!

Kundi hili huwa haliaminiki (ni vidokozi)
Katika kundi hili WATU WAKE Wanajulikana kama watu wasiyo na HAYA!
Inatamkwa kwamba mtu aliye kwenye kundi hili ni HODARI sana wa kufanya UKUWADI na UDALALI!

Anaweza akakudalalia ukiwa umekaa naye pembeni almradi tu katangaziwa dau.

Hata kwenye mambo mhimu na nyeti! mfano; Anaweza hata KUDALALIA manunuzi ya Jeneza endapo akishilikishwa kwenye mipango ya mazishi! Kiufupi kundi hili la WIZI WANA TAMAA! ukiwapa nafasi yoyote tu HESABU MAUMIVU (wanaiba chochote machoni)

Ni afadhali ukutane na Mpenzi akiwa STEJI ya DHIKI kuliko akifika STEJI YA TAMAA! (Aaweza kukuibia hadi Viza card wakati haitamsaidia popote, anaweza kuiba heleni, wigi au chochote wakati ni mwanaume) n.k

Wizi wenye chimbuko la KISAIKOLOJIA

Hapa ili mada isiwe ndefu nitaeleza kwa ufupi!
TATIZO la KISAIKOLOJIA linachangia sana WIZI hii inatokana na makuzi, tamaduni na Mapokeo ya Jamii inayotuzunguka. Kundi hili machoni ni kama watu wema na Huifumba jamii kuwa ni wema!
Kundi hili linafanya kazi kwa mfumo (Team work au System connected)

Kundi hili la wizi hutumia akili 80% na nguvu 20%

Katika Kundi hili wakiamua kutumia IMANI hufanikisha mambo yao kwa USTADI WA KUTUMIA SANAA NA MAANDIKO MATAKATIFU (Sitaeleza sana hapa)

Kundi hili limegawanyika katika makundi mawili ( UJAMBAZI kwa walio inje ya mfumo rasmi, Na UFISADI kwa walio ndani ya mfumo)

Kundi hili pia huweza kujumuisha Imani za kishirikina yote ni katika kukamilisha matumizi ya akili kwa wingi 80%, na inapobidi matumizi ya nguvu (SUMU na BUNDUKI) kwa 20% hufanyika ili kufanikisha jambo! Lakini hilo hutokea baada ya matumizi ya akili kushindikana!

Katika matumizi ya nguvu huondoa kikwazo chochote kinachoonekana kukwamisha matumizi ya akili!

Kikwazo hiko kinaweza kuwa Mlango, mtu, mlinzi, kiongozi au afisa yoyote anayeonekana kukwamisha mipango yao kutimia!

Aina hii ya watu ni hatari zaidi duniani kuliko Wizi aina ya DHIKI/TAMAA

Bahati mbaya sana WEZI aina hii imepenya hadi kwenye MAMLAKA MBALIMBALI! .........Itaendelea!

Huko China walifanikisha kupitisha sheria ya KUNYONGA na KUFILISI YOYOTE ALIYETHIBITIKA KUFANYA UFISADI na MATUMIZI MABAYA OFISI

Ni imani yangu uchambuzi huu umekusaidia kujua ni kwa kiasi gani jamii imezungukwa na WEZI
Kama kuna swali au maoni weka komenti hapa chini utajibiwa!
 
Ebu niulize mfano Mimi uwa sichukui kitu cha mtu nikiwa mzima ila nikinywa tu asubuhi najikuta na glass za bar kwenye gari Kuna siku nishawai beba king'amuzi Cha bar na kiukweli Sina kazi navyo...am i fall into that categories?
We akili huwa inavurugika na kujiona ufanyalo sawa tu.Kwakuwa umejijuwa jirekebishe.
 
Kuna jamaa ni mwiz mwiz,kuna siku alinishangaza aliiba kufuri la elfu 30 wakati halikuwa na ufunguo
 
Kuna mwizi nilikuwa namkubali zamani kidogo aliitwa Paulo Sergio De Souza, ila nikaja kugundua hakuwa kichwa kama nilivyodhani.

Watu kama Dan (D.B.) Cooper, na Barefoot Bandit, ndio wanastahili kuiita fani yao sanaa.
 
Ebu niulize mfano Mimi uwa sichukui kitu cha mtu nikiwa mzima ila nikinywa tu asubuhi najikuta na glass za bar kwenye gari Kuna siku nishawai beba king'amuzi Cha bar na kiukweli Sina kazi navyo...am i fall into that categories?
Huenda unahistoria ya udokozi, Hivyo maisha yalikubadilisha! Lakini unapolewa pombe huwa Ina tabia ya KU-default akili. Hivyo ukilewa huifanya akili yako I we halisi kabla ya kubadilika!
Ndiyo maana kama mtu ni Malaya mstaafu akilewa huwa anaopoa, kama alikuwa mgomvi akabadilika akilewa anafanya ugomvi n.k
 
Aisee hawa wanaotumia ushirikina kiboko anaingia kwako anafungua, anakula, anashiba than anaiba anachotaka hata ukimuona anaiba kazi bure ukimfukuza akila kona humkamati[emoji38][emoji38]
 
Aisee hawa wanaotumia ushirikina kiboko anaingia kwako anafungua, anakula, anashiba than anaiba anachotaka hata ukimuona anaiba kazi bure ukimfukuza akila kona humkamati[emoji38][emoji38]
Wanatumia sumu aina ya chloroform! Hii huipuliza madirishani ili hewa yake inapovutwa inamfanya aliyelala kuwa Nusu kaputi!
Ukitaka kuzuia hili WEKA NDOO YA MAJI ILIYO WAZI KANDO YA DILISHA hii itasaidia sumu ya chloroform kukimbilia kwenye ndoo ili kufanya REACTION!
 
Wanatumia sumu aina ya chloroform! Hii huipuliza madirishani ili hewa yake inapovutwa inamfanya aliyelala kuwa Nusu kaputi!
Ukitaka kuzuia hili WEKA NDOO YA MAJI ILIYO WAZI KANDO YA DILISHA hii itasaidia sumu ya chloroform kukimbilia kwenye ndoo ili kufanya REACTION!
Hivi hii makitu ni kweli ukiweka ndoo ya maji au besen iliyo wazi inanyonya iyo makitu? Au ni porojo ya mmatumbi?

Je mmatumbi ashafayna riseech nakujiridhiha hii makitu inanyonya na ndoo au ni porojo tu kwenye vijiwe vya umbea kustarehesha vibaraza?
 
Hivi hii makitu ni kweli ukiweka ndoo ya maji au besen iliyo wazi inanyonya iyo makitu? Au ni porojo ya mmatumbi?

Je mmatumbi ashafayna riseech nakujiridhiha hii makitu inanyonya na ndoo au ni porojo tu kwenye vijiwe vya umbea kustarehesha vibaraza?
Ulishawahi kujiuliza kwanini panya akila sumu then maji hupona?
Sumu ya chloroform inapendelea zaidi kukimbilia kwenye maji ambako ni rahisi Ku dissolve, (slightly soluble in water)
 
Ulishawahi kujiuliza kwanini panya akila sumu then hupata kiu ya maji hupona?
Sumu ya chloroform inapendelea zaidi kukimbilia kwenye maji ambako ni rahisi Ku dissolve!
Iyo ya panya kunywa maji baada ya sumu ni muendelezo tu wa porojo ya mmatumbi vijiweni wakishashiba na kuvimbiwa na viporo vya kande.
 
Iyo ya panya kunywa maji baada ya sumu ni muendelezo tu wa porojo ya mmatumbi vijiweni wakishashiba na kuvimbiwa na viporo vya kande.
Porojo unaleta wewe mkuu Ila sayansi iliyounda Sumu hiyo inathibisha Chloroform is slightly soluble in water!

hii inamaanisha ni rahisi kunyonywa ndani ya maji, Ifahamike sumu zote zenye mtindo wa BENZINI, GONGO, spirit hunyonywa kirahisi kukiwepo maji kando
 
Porojo unaleta wewe mkuu Ila sayansi iliyounda Sumu hiyo inathibisha Chloroform is slightly soluble in water!

hii inamaanisha ni rahisi kunyonywa ndani ya maji, Ifahamike sumu zote zenye mtindo wa BENZINI, GONGO, spirit hunyonywa kirahisi kukiwepo maji kando
Achana naye hyo mla burger za Wazungu hapo Copenhagen
 
Back
Top Bottom