Ijue Toyota Coaster new model Fourth Generation

NO4C ni engine za hino, ni kweli kabisa Toyota anaitumia sana hii engine kwenye masoko sensitive na emissions controls ,looks like engine za toyota hazipo vzr kwenye emissions
 
Wajapani wanaangalia soko gari iliyo kwenye demand kubwa bei inanyuka juu..mambo ya hii ngumu hii mbovu wanajua wanunuzi sio wauzaji...hata hizo Nisssan zikinunuliwa sana utaona bei itanyuka tuu kumbuka fusso zilianza kwa bei ya kawaida wateja walipoanza kuagiza kwa fujo wakazinyanyua bei...
 
Hiyo kama haijanunuliwa haijanunuliwa na Serikali, Basi tutegemee kuiona miaka kumi na tano ijayo, Tena na teknolojia itakuwa imebadilika, maana saa hizi wengi wanahamia kwenye renewable energy vehicles
Tayari zipo Tanzania na nyingine zinamilikiwa na ubalozi na serikali.
 
Huu uthibitisho wa Nissan Civilian ni gari mbovu, au Mitsubishi Rosa sio imara mmeutoa wapi?
Hakuna sehemu nimesema Nissan Civilian au Mitsubishi Rosa sio imara. Wabongo wanakimbia Nissan sababu ya kushindwa kuzihudumia kama zinavyotaka na spare zake Bei ipo juu.

Mitsubishi Rosa watu waliziogopa injini za 4D33 na 34 ndio ziliwashinda kwenye kuhudumia kutokana na kukosa utalaamu.
 
Mkuu Toyota Coaster injini za uzao wa 3B,13B waliachana nayo wakaja na 15B-T ambayo ipo kwenye Coaster Mayai nayo ni moto wa kuotea mbali hata kwenye Toyota Dayna new model ndio inatumika Sana.

Injini ya 1HZ-T hii ilikuwa ni modifications zinazofanya na watu wanaopenda off road huko Arabuni na Australia. Lakini baadae Toyota akazalisha official kwenye Toyota Coaster. Kwa bongo naona Team Cruiser Mechanics wamefanya mod ya 1HZ kuwa 1HZ- T ingawa sijajua Kama imefika Hp halali.

Pia kuna injini ilitumika kipindi kifupi kwenye baadhi ya Coaster na L/Cruiser series 76 inaitwa 1PZ hii ilikuwa 5-cylinder inline. Hii ilikuwa na gear box ya 4 speed, hii wengi waliogopa sababu ya maneno ya kuunguza cylinder head gasket.
 

Yes, watu waliweka tu turbo kwenye 1HZ. Ndio maana nikasema 1HZ-T haikutengenezwa. Baadae ndio Toyota wakatengeneza a turbocharged 1HZ wakaiita 1HD-T. Ila ikawa na shida nyingi, ndio maana ilidumu muda mfupi tu, wakaja na 1HD-FT, baadae 1HD FTE. Japo kiuhalisia hizi engines zinafeatures nyingi zinafanana.

15B-T ilitumika kwenye 3rd gen Coaster (Coaster mayai) miaka ya mwanzo ila kwenye hii 4th gen haijatumika.
 
Kweli Nissan hazihitaji ujanja ujanja. Sasa wengi wananunua Civilian zenye air suspension. Zikizingua wanashindwa kurepair mwisho wa siku unakuta Civilian kwa mbele imeinuka zaidi kuliko nyuma. Inakuwa kama fisi 😁😁
 
1HDT FT na 1HDT FTE ni engine moja , sema moja ni manual pump nyingine ni pump ya umeme.
Ile' E' pale mwisho ni kielelezo kuwa ni electronically controlled
 
Mkuu Toyota walizalisha 1HZ- Turbo na ikawekwa kwenye Toyota Coaster.
1HZ- T zipo ila chache Sana kwenye Coaster Box body, kwenye Land Cruiser Hard Top ndio zinafanyika mods kutoka 1HZ kavu kwenda 1HZ-Turbo.
 
Good
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…