Ikiwa una dalili hizi unatakiwa kumuona Mwanasaikolojia

Dom2

Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
74
Reaction score
99
Afya ya akili ni hali ya ustawi ambao mtu anajua uwezo wake mwenyewe, anaweza kukabiliana na matatizo ya kawaida ya maisha, anaweza kufanya kazi kwa ufanisi na yenye matunda na anaweza kutoa mchango kwa jamii yake" mfano mawazao, maoni au mali".

Zifutazo ni baadhi ya dalili za kua na matatizo ya afya ya akili:
  • Kukosa usingizi au kulala sana
  • Kula sana au kukosa hamu kula
  • Kukosa hamu ya kazi au mambo ulizokua uliyokua unazifanya au unayafanya mwanzo mfano kucheza mpira au kuogelea au tendo la ndoa
  • Kuwa mpweke na huzuni za mara kwa mara
  • Kujitenga na kupenda kukaa peke yako
  • Kulia pasi na sababu
  • Kujihisi umeelemewa na mzigo kwenye fikra zako
  • Kuwa na mawazo hasi,mfano mimi nina mkosi, siwezi fanikiwa
  • Kuwa na wivu uliokuzidi uwezo kwenye mahusiano
  • Kuwa mtu wa kuwaza kulipa visasi kila mara
  • Kujihisi kuna watu wanakuchunguza
  • Kuona picha za watu kinyume na uhalisia
  • Kusikia sauti kinyume na uhalisia
  • Kuwa na hasira za haraka bila sabbu za msingi
  • Kupoteza kumbukumbu sana
  • Kushindwa kusamehe waliokukosea
  • Kuwa na mawazo hasi, unawaza mabaya tu kwenye akili yako, mfano, mimi siwezi pata kazi, mimi siwezi pendwa, mimi mbaya
  • Kuongea sana au mpole sana kinyume na uhalisia wako
  • Tabia ya kurudia rudia mambo au fikra mfano kuoga kila mara
  • Kuwaza kujiua mara kwa mara
  • Kuwa mnyonge
  • Kuchoka sana bila sababu
  • Kuumwa na kichwa mara kwa mara bila sababu
  • Kushindwa kujisamehe mwenyewe au kusamehe wengine

NB: Ukiona una dalili hizi Jua una shida kwenye afya ya akili, hivyo yakupasa kumuona Mwanasikolojia .
 
He kwasababu zote hizi basi dunia nzima tuna matatizo ya akili 🤣🤣
 
He kwasababu zote hizi basi dunia nzima tuna matatizo ya akili [emoji1787][emoji1787]
Kila binadamu anapitia Changamoto za afya ya Akili kila siku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…