Iko Siku Tutaamka na Kusikia Wananchi Wameamua Kujichukulia Ikulu na Kuiongoza!

Iko Siku Tutaamka na Kusikia Wananchi Wameamua Kujichukulia Ikulu na Kuiongoza!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2006
Posts
4,526
Reaction score
1,540
Leo hii, nimesoma habari kuwa Wafanyakazi wa TRL, wameamua kujichukukulia majukumu ya kuendesha na kuongoza TRL baada ya Rites kutoa notisi ya siku 60 kujitoa na Serikali kukaa kimya bila kutoa kauli inayoeleweka.

Ukimya wa Serikali ya Tanzania katika mambo ya msingi na kutatua kero za Wananchi unatisha!

Uongozi wa Serikali ya Tanzania inaelekea umelala usingizi wa Pono kama si kuamua kuwa haujali yule mpiga kura aliyeipa Serikali hii dhamana ya kuliongoza Taifa la Tanzania.

Anzia Ajira, Elimu, Afya, Usalama wa Wananchi, Maji Safi, Umeme, Msongamano wa Magari, kukosekana kwa Uwajibikaji, kuongezeka kwa Uhujumu na Ufisadi, ni kero kila kona na napenda kukataa na kuipinga kauli yangu ya wiki tatu zilizopita kuwa Tumeridhika na dhiki, tabu na mateso.

Ujasiri wa wafanyakazi wa TRL, hata kama tutadai eti haukuwa wa halali, naupongeza kwa kuwa tangu awali, Serikali yetu ambayo ni mbia mkubwa wa mkataba huu wa Shirika la Reli, imefumbia macho malalamiko ya Wananchi na hata mradi wenyewe wa Uwekezaji TRL haukufanyika kwa unyoofu pamoja na Serikali kuelezwa.

Wakati unaanza wadia ambapo Wananchi wanaamua kujichukulia hatua mkononi. Wanaamua kufanya kazi na kuchukua dhamana ya kuongoza na kuendesha nchi yetu kutokana na kukosa uaminifu na uvumilivu kutoka kwenye kauli hasi za Viongozi na Serikali.

Inasikitisha, inatisha na inadhalilisha, lakini itakapobidi, sitashangaa kusikia siku moja asubuhi kuwa Wananchi wamejitwalia Ikulu na Bunge na kuamua kujiongoza kwa matakwa yao wenyewe kutokana na kuchoshwa na Viongozi wazembe na Serikali isiyojituma wala kuthamini dhamana iliyopewa kuongoza Taifa la Tanzania!

Sichochei machafuko au watu kuvunja sheria, lakini ikiwa leo haki ya Mtanzania inawekwa majaribu kutokana na kiburi, uvivu na dharau kutoka kwa wale walioaminiwa kuongoza na kulipeleka Taifa letu katika njia iliyo sahihi, Mchungaji hatashangaa, wala kuwasikitikia wale watakaoondolewa madarakani kutokana na uzembe wao!
 
Mkulu Rev,heshima mbele.Kile unachokiona/kifikiri kwa Tanzania ya leo ni ndoto,tena ya mchana.I mean wananchi wepi wa kuamua hayo?Hao waliowapokea kina Lowasa na Chenge kama mashujaa.Majority ni kwamba wapo usingizini na huenda wasiamke in a near future.Umenikumbusha wimbo flan tulikuwa tunauimba kwenye mchakamchaka kuwa'...jua lile literemke mama....'.
 
kwakweli kwa bongo ni kazi, ila hakuna marefu yasio na ..........ipo siku kitawaka tu usiwe na haraka.bado bongo tunaogopa ogopa risasi hivi,,ila zitazoeleka , kwani hukumbuki tulivyokuwa tunaogopa polisi zamani sikuhizi je...so worry not baby
 
Tusubiri tamko la serikali, ndo litatupa picha kamili juu ya jambo hili. Si ajabu kusikia inapiga magoti kwa wahindi na kuwasaliti watanzania.
 
Nimegundua kitu kimoja...kama kweli macho yangu yana machozi basi bora niyaache nije kujililia mwenyewe maana kila mtu ana kila sababu ya kubeba mzigo wake.
 
...jua lile literemke mama....'.
ngoja nikusiadie......!...aiyaiyaaa iya iya mama!....mwezi nao uteremke mama......nyota nazo ziteremke mama..aiyaiyaiya iya mama.....!

Baba Paroko....! ''Liwalo na liwe kila mmoja na lwake''!
 
We all wish wish wish wish......and wish......and wish.....and write....it ends here...
 
poleni kwa maumivu makali yasababishwayo na mfisadi wa nnchi hii, poleni, iko siku, yana mwisho haya. Tusikate tamaa.
 
REV huchochei machafuko. Wanasiasa na viongozi wetu wabovu ndio watakaotuletea machafuko. Wala usijitetetee.
 
Rev, jogoo akiwika uje kumepambazuka. TRL ni jogoo awikaye kulipopambazuka, uliyosema ni sahihi kabisa. Kwa mwendo huu wa usingizini usishangae siku moja watu wakaichukua hiyo Ikulu na Bunge lao na kuendesha watakavyo kuliko hii style ya mipasho na taarabu zisizo na melody
 
Rev. I dare anyone in Tanzania to do so;
Tunashindwa kumsaidia jirani hata akiingiliwa na vibaka
Tunashindwa kutetea haki za watoto na wanawake
Tunashindwa kumuondoa afisa mtendaji bazazi
Tunashindwa kumuondoa mwalimu mbakaji
Tunashindwa kumuondoa mchuna ngozi

Tunashindwa kujiandikisha kupiga kura
tunashindwa kuhoji matumizi ya fedha za wafadhili
tunashindwa kuhoji lead time iliyotumika kuleta mafuta ya IPTL tunajua wiki tatu huwezi kuagiza, kupaki na kusafirisha
Tunashindwa kuhoji kikao cha bunge cha november 2009 kimedeliberate nini
tunashindwa kudai kodi zinazokatwa isivo na utaratibu

Tunashindwa kuhoji mapato ya madini, ardhi, misitu na maliasizi nyongine
tunashindwa hata kuhoji wanaopiga raia
Tunashindwa kuhoji haki za mama njamzito clinic
Tunashindwa hata kusaidia usafi wa mitaa yetu
Tunashindwa hata kusaidiana basic needs

Tunajali mazishi kuliko uzazi salama
Tunajali harusi kuliko elimu
Tunajali send of kuliko kupokea bwana harusi
tunajali kitchen party kuliko misa za shukrani

Tunashindwa hata kumzuia askari asimpige polisi
tunashindwa kuhoji baadhi ya wabunge mafisadi
tunashindwa kuhoji nguvu ya rushwa
tunashindwa kuhoji uhalali wa uwepo wa mawaziri


I dare anyone kuchukua nchi... NINAOMBA NIWE HAI NA NIBEBE BENDERA ZA WANAMAPINDUZI AU NGOMA ZA SHEREHE

Peace
 
mkataba ulishapigiwa kelele muda mrefu na waheshimiwa lakini ikulu wanakwambia mkataba safi pamoja na kuambiwa kasoro kibao.........tatizo hata rais mwenyewe huwa anahusishwa kwenye mikataba yote hewa na huwa anajua kuwa mkataba hauna maslahi ila kwa kuwa kauli mbiu ya chama chetu ni chukua chako mapema hivyo rais anajitahidi angalau ajichotee kupitia mikataba hii mibovu kwa kutumia watu wengine na ndio maana hawezi kuwawajibisha,kama isingekuwa hivyo angekuwa anachukua hatua fasta ili kunusuru wananchi wanaoteseka bila sababu......
Nchi iliisha oza,mwl.nyerere alishatutadhadharisha kuhusu lundo la watu waliokuwa wakiutaka yongozi wa juu wa nchi kwa udi na uvumba....sasa dhambi aliyosema itatufuata kama tukipuuza ushauri wake ndio hiyo tunayoiona sasa..........kwa kweli haya mabo yanakera sana.
 
HIvi pale watu wa Tanesco walipojifanya wanaleta mapinduzi dhidi ya wakaburu serikali ya Mkapa ilifanya nini?
 
HIvi pale watu wa Tanesco walipojifanya wanaleta mapinduzi dhidi ya wakaburu serikali ya Mkapa ilifanya nini?
mwanakiji wawekezaji wale waliingizwa ofisini kwa mtutu wa Bunduki, walikula wee wakashiba, kisha wakaondolewa, lakini ujumbe ulifika.
Pamoja na nguvu zao, kama umma wote utaamka kweli SMG zao hazitzfua dafu, kwani Suharto wa Indonesia hakuwa na Bunduki, aah wapi, watu wakichoka ni hatari.
 
kwakweli kwa bongo ni kazi, ila hakuna marefu yasio na ..........ipo siku kitawaka tu usiwe na haraka.bado bongo tunaogopa ogopa risasi hivi,,ila zitazoeleka , kwani hukumbuki tulivyokuwa tunaogopa polisi zamani sikuhizi je...so worry not baby
Tunamuhitaji mtu kama Kinjeketile Ngw'ale ambaye atatutia ujasiri kuwa risasi zitageuka maji.
Nadhani wananchi wameanza kuzoea risasi - ebu kumbuka matukio ya wananchi kuvamia vituo vya polisi; si risasi zinapigwa lakini wananchi wanasonga mbele hadi walilokusudia litimie!
Iko siku kweli na si mbali sana.
 
Naam inawezekana kabisa siku hiyo tukaiona. Maana watu wamevumilia vya kutosha na uvumilvu una kikomo chake. Kulikuwa na nafasi chungu nzima za kukatisha mkataba na matapeli hawa toka India ambao na wao tuliwaita "Wawekezaji" lakini Serikali ya Kikwete kama kawaida yake ikafumbua macho kasoro mbali mbali zenye uzito wa hali ya juu ambazo nyingi zilikiuka vipengele mbali mbali vya mkataba na matapeli hao.

Hongera Wafanyakazi wa Reli kwa kutuonyesha njia Watanzania ya kurudisha hadhi ndani ya nchi yetu labda siku za usoni mikakati yenu inaweza kabisa kutumika katika kuchukua Ikulu yetu toka mikononi mwa papa fisadi Rostam Aziz na kundi la mafisadi wenzie.
 
Rev. Watanzania bado hawana ujasiri huo. Mfano ni wa Walimu ambao wale waliolipwa madai yao wameshindwa kushirikiana/kushikamana na wenzao katika kuiadabisha Serikali ili isirudie tena mchezo wa kuwatumia walimu (na wananchi wengine) bila kujali maslahi na maisha yao. Wafanyakazi wa Kiwira nao ni mfano mwingine; walisahau machungu yote walipoambiwa na Ngeleja kwamba watalipwa malimbikizo ya mishahara yao na ajira zao zitaendelea k.k. Wakaamua kusukuma gari la Ngeleja na Mwakyembe kwa furaha na kusahau yote!

Serikali ya CCM inajua udhaifu wa wananchi. Mbinu za kuwaghilibu wananchi na kuwadanganyia 'pipi' zinatumiwa sana na Chama cha Mapinduzi. Bila kujali mustakabali wa wananchi, CCM na Serikali yake wanachukulia shida za wananchi kama mtaji wa kuendelea kuwa madarakani. Inasikitisha sana.

Wananchi kuamua kujichukulia Ikulu labda inaweza kutokea pale generation ya wazee waliopo madarakani sasa itakapoondoka na kwenda kwa Sir God!
 
Haki huinua Taifa, tunapoendelea kuwanyima Watanzania haki na kuwazereu, mwishowe ni kupigwa mawe!
 
Haki huinua Taifa, tunapoendelea kuwanyima Watanzania haki na kuwazereu, mwishowe ni kupigwa mawe!

Rev. je hauoni pia kwamba ni sisi ndio tunawapa hawa watawala haki ya kuchukua hta hazi zetu?? what a re we doing from grassroot level??
 
Back
Top Bottom