Iko wapi ya wana-udom

buhange

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2011
Posts
505
Reaction score
110
Habari wana-JF

Kwa kumbukumbu za haraka haraka ni kwamba pesa
( LOAN) zinazotowa na serikali kupitia HESLB kwa wanavyuo vya elimu ya juu ni kwa masharti ya kurudishwa baadae na wahusika(wanavyuo)

Sasa utaratibu mpya ulioanzishwa na bodi wa kuvipa-mandate Vyuo husika kuweka pesa kwa wanafunzi imeongeza uvivu,uzembe na hata ubadhirifu ktk Loan offices kwa baadhi ya Vyuo. Mathalani, Continuing students ktk vyuo vingi vikiwemo UD na UDOM wamekuwa wakilalamika kutopewa Mikopo yao mpaka leo tangu vyuo vimefunguliwa, wakiuliza sehemu husika(Loan office) utasikia Una-Incomplete mara Matokeo ya kozi yako tulichelewa kuyatuma bodi ya mikopo na wakikuhurumia sana watakwambia swala lako lipo ktk mchakato.

Hali ni tofauti zaidi ktk chuo kikuu cha Dodoma, maana kwa taarifa tuu ni kwamba baadhi ya wanafunzi ktk kozi kadhaa hawana hata matumaini ya kupata hizo pesa zao ktk SEMESTER hii. Vijana wanaishi ktk maisha ya kutisha na kusikitisha kama siyo kukatisha tamaa kabisa.

UDOM swala la BATCH ndilo lilotawala, utasikia vijana hawa wakifarijiana kwa maneno kama "JINA LANGU LIPO BATCH YA 14, LABDA ITATOKA WIKI IJAYO". Utakuta kijana huyu anazungumza maneno haya akiwa hana hata uhakika wa kupata kipande cha mkate ktk siku husika. Inatisha sana ndugu wana-JF

Sasa, hata hizo BATCH zitolewapo na wanafunzi wenye bahati ya mtende kupata fursa ya kusaini kwa ajili ya kuhakiki akaunti zao, hali huwa tofauti ktk kuwekewa hizo pesa. Mathalani, UNAWEZA KUSAINI LEO TAR.29/11 ILA UKAKAA WIKI TATU BILA PESA KUINGIA KTK AKAUNTI YAKO, Sasa Management na Loan Office UDOM wapo kwa ajili ya nini, bila ya hawa wanafunzi wanaowanyanyasa Leo hii kwa majibu ya kukatisha tamaa wao Wafanyakazi wangekuwepo kwenye hizo Office wanazolingia na viti vya kuzunguka? HUU NI UPUMBAVU NA UDHARIMU MKUBWA SANA

SOCIAL SCIENCE ni mfano wa wahanga wa swala hili, takribani 51% ya wanafunzi wa SOCIAL SCIENCE hawajapewa pesa zao, Sasa hawa watu

1.Wanakula na kunywa nini?
2.Wanaandika na kusoma kwa kutumia nini?
3. Kuna mwanafunzi kuelewa kipindi akiwa hana uhakika wa kula baada ya kipindi?
4.Taifa linaandaa wasomi wa aina gani au wanaandaa MAKOMANDOO, MA-MAFIA NA WAZAMIAJI?

Naomba Umma uelewe wazi kwamba ktk hali kama hii MIGOMO, FUJO NA HATA MAANDAMANO itabaki kuwa suruhu yetu ktk kutatua matatizo yetu, mpaka hapo Serikali watakapo elewa nini hasa tunamaanisha.

POSHO ZA WABUNGE HAZITOLEWI KWA BATCH WALA HAZICHELEWESHWI, MAFUTA YA (SU) NA (DFP) ZA SERIKALI HAYAKOSEKANI ILA MIKOPO YA WANAFUNZI TUU... HAIWEZEKANI.
 
Mpo karibu na bunge na makao makuu ya CCM wakija kikao kijacho wafuateni
Tatizo Udom wanafiki sana tulianzisha harakati wakafukuzwa wenzetu,ila kwenye kurudi watu wakajifikiria wao tu bila kukumbuka kuna waliofukuzwa
Udom haitakuja kua kama ilivyokua mwaka jana na mwaka huu mwezi wa sita
 
Kaka unafiki upo kila mahali, kama ni issue ya kubadilika ipo kwa kila anaejitambua. kwa kuwa mpigania haki huonekana kama ndo mvunja sheria hasa ktk nchi kama ya Tz, so funguka haka kadri ya uwezo na capacity of your thinking ktk hii thread.
 
Lianzisheni..msiwe waoga namna hyo vijana,maisha ya chuo magumu eti!
 
Kwa kweli wingi wa wana UDOM wameshindwa kuutumia ila ndo matunda ya usaliti.Kama hamkupewa hela hadi muda huu tena nusu yenu isitoshe mna matatizo kibao,kama bei ya chakula kupanda na mengine mnayajua.NI WAZI KUWA MTU AKIKUSHIKA MAKALIO bila Kumkemea basi ataingia ndani kabisa ya ....,.MATATIZO YA WANA UDOM YANATATULIWA NA WANA UDOM WENYEWE(Laleni mi simo)
 
Msosi siku hizi ni 1200 kwa plate na nyingine 1500, ila UDOM msiandamane tena maana hakuna umoja full usaliti tu. Handsome wa mama nawaomba wenye chuo chao waendelea kuwekeza hizo fweza kwenye ma fikisidi account wapate faida kama wanavyopata za wale 534 waliotimuliwa then tuone mtachukua aksheni ipi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…